KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,147
Mfadhili wa zamani wa Simba, Azim Dewji amesema alichokieleza kuhusiana na njama za TFF kutaka kumrudisha madarakani, Michael Wambura kimekamilika.
Lakini akasisitiza, kukamilika kwake kumekuwa na uwazi na kuonyesha hakukosea hata kidogo.
"Nani anaweza kupinga tena kwamba Wambura amerudishwa kwa hila kama nilivyoeleza.
"Suala la sheria na upigaji kura linatokea wapi, sheria inaamuliwa kwa vipengele.
"Ndiyo maana nilisema TFF ni kawaida yake kufanya maamuzi ambayo yanaiumiza Simba, hii si mara ya kwanza.
"Wao waliofanya hivyo wanajua kuwa walichofanya si sahihi, lengo ni urafiki na kusaidiana.
"Kwa nini kusaidiana kwa maslahi ya watu binafsi badala ya kufuata sheria na kanuni ambazo ziko wazi.
"Sasa hakuna anayeweza kusema nilikuwa nafanya fitna, nilichozungumza nilikuwa nakijua na watu wanielewe vizuri. Sasa imebaki kidogo tu, TFF kuchagua nani awe Rais wa Simba," alisema Dewji.
Wiki iliyopita, Dewji ambaye alichangia kwa kiasi kikubwa Simba kufika fainali ya Kombe la Caf mwaka 1993, alisema kuwa lazima kamati ya rufaa ya TFF itamrudisha Wambura kugombea nafasi ya urais Simba baada ya kuwa amekatwa na kamati ya uchaguzi ya Simba.
maoni yangu:Azim Dewji,kassim Dewji na wengine wafunge midomo yao wakati huu kuelekea uchaguzi,wajikite katika kumfanyia kampeni mgombea "wao" badala ya kutumia nguvu nyingi kupita kiasi kuhakikisha mgombea "wao" anapita bila challenge,kama walikua hawamuamini mgombea wao huyo kwanini mmoja wao kati ya Azim Dewji na Kassim Dewji hakuchukua fomu za kugombea urais wa simba,kwanini wanajaribu kutaka kuvuruga mchakato wa uchaguzi kwa kuingilia maamuzi ya vyombo husika viliwekwa kwa mujibu wa katiba ya tff,cuf na fifa??wakumbuke kwamba mwisho wa siku wanachama wa simba ndio wenye maamuzi ya mwisho.
Lakini akasisitiza, kukamilika kwake kumekuwa na uwazi na kuonyesha hakukosea hata kidogo.
"Nani anaweza kupinga tena kwamba Wambura amerudishwa kwa hila kama nilivyoeleza.
"Suala la sheria na upigaji kura linatokea wapi, sheria inaamuliwa kwa vipengele.
"Ndiyo maana nilisema TFF ni kawaida yake kufanya maamuzi ambayo yanaiumiza Simba, hii si mara ya kwanza.
"Wao waliofanya hivyo wanajua kuwa walichofanya si sahihi, lengo ni urafiki na kusaidiana.
"Kwa nini kusaidiana kwa maslahi ya watu binafsi badala ya kufuata sheria na kanuni ambazo ziko wazi.
"Sasa hakuna anayeweza kusema nilikuwa nafanya fitna, nilichozungumza nilikuwa nakijua na watu wanielewe vizuri. Sasa imebaki kidogo tu, TFF kuchagua nani awe Rais wa Simba," alisema Dewji.
Wiki iliyopita, Dewji ambaye alichangia kwa kiasi kikubwa Simba kufika fainali ya Kombe la Caf mwaka 1993, alisema kuwa lazima kamati ya rufaa ya TFF itamrudisha Wambura kugombea nafasi ya urais Simba baada ya kuwa amekatwa na kamati ya uchaguzi ya Simba.
maoni yangu:Azim Dewji,kassim Dewji na wengine wafunge midomo yao wakati huu kuelekea uchaguzi,wajikite katika kumfanyia kampeni mgombea "wao" badala ya kutumia nguvu nyingi kupita kiasi kuhakikisha mgombea "wao" anapita bila challenge,kama walikua hawamuamini mgombea wao huyo kwanini mmoja wao kati ya Azim Dewji na Kassim Dewji hakuchukua fomu za kugombea urais wa simba,kwanini wanajaribu kutaka kuvuruga mchakato wa uchaguzi kwa kuingilia maamuzi ya vyombo husika viliwekwa kwa mujibu wa katiba ya tff,cuf na fifa??wakumbuke kwamba mwisho wa siku wanachama wa simba ndio wenye maamuzi ya mwisho.