Uchaguzi TFF 12/08/2017 Dodoma: Kauli mbiu ya karia na vipaumbele vyake 11

Uchaguzi TFF 12/08/2017 Dodoma: Kauli mbiu ya karia na vipaumbele vyake 11

JINOME

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2017
Posts
958
Reaction score
1,427
Mgombea Urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambaye pia ni Kaimu Rais wa Shirikisho hilo, leo amehojiwa na TBC1 na kuelezea. Kauli mbiu yake na kufafanua vipaumbele vyake endapo atachaguliwa. Kauli Mbiu: UWAZI, UWADILIFU, UWAJIBIKAJI NA MAENDELEO

VIPAUMBELE 11:
1. Nidhamu na Muundo wa mfumo wa TFF
2. Maendeleo ya Soka ya Wanawake, Vijana na soka ya Ufukweni
3. Mafuzo na ujenzi wa uwezo kwa Makocha, watawala, mafunzo ya utabibu, Waamuzi, wakufunzi wa kitaifa, watendaji na viongozi wa vilabu n. k.
4. Usimamizi na Nidhamu ya matumizi ya Mapato ya fedha.
5. Kutoa MIL. 15 ya Maendeleo kwa kila Mkoa
6. Kushirikiana na wadau wa viwanja Kama Chama cha Mapinduzi Halmashauri za mitaa ili kuboresha Viwanja hivyo na kuwekeza Katika vituo vya Karume na Tanga
7. Tathmini ya Muundo mzima wa Bodi ya Ligi na kuipa uhuru zaudi
8. Kushirikiana na Serikali , FIFA, CAF Wanahabari na Wadau wengine ili kuboresha mawasiliano kwa wanafamilia ya mpira.

9. . Kuboresha Kalenda ya Mashindano na usajili kitaifa.
10. Uimarishaji wa mifumo ya kumbukumbu
11. Kuanzisha mfumo wa kuwa na orodha ya Waamuzi inayozingatia ubora na weledi ili kukabiliana na changamoto za Waamuzi.

Nimejaribu kuorodhesha kwa kifupi yote aliyoyaongelea bwana Karia. Sina uhakika Kama Wagombea wengine wana vision na mission Kama ya KARIA. laiti Kama ningekuwa mmoja wa wapiga Kura hiyo tarehe 12/08/2017 Dodoma,. Ningetumia muda wangu kuwashawishi wapiga Kura wenzangu tumpe Kura huyu bwana, ana "focus" mbali katika kuendeleza Soka la Tanzania . Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, hii ni lulu msiiache ikapotea.
 
Mbona unampigia chapuo hivo, au nawewe umekula mlungula kama yule jamaa?
 
Mpeni Tembele hao wengine wa nini ?
 
  • Thanks
Reactions: GUI
Hatuelewi kitu
00ab729cee60dc2472973eb6ca7589e7.jpg
 
Vote for Ali mayay tembelea , tumewachoka wahuni, uyo karia ni sehemu ya uozo wa malinzi
 
Back
Top Bottom