Uchaguzi 2020 Uchaguzi unatakiwa kuwa wa uwazi usio na shaka yoyote ile

Uchaguzi 2020 Uchaguzi unatakiwa kuwa wa uwazi usio na shaka yoyote ile

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete alipotoka Nigeria kushuhudia zoezi la upigaji kura, uhesabuji kura na utangazaji matokeo, alisema kuwa angependa siku moja nasi Tanzania tufikie kiwango cha Wanigeria.

Mojawapo ya jambo alilolitamka ni kuwa kura zilikuwa zinahesabiwa eneo la wazi huku wapiga kura wakishuhudia. Kura zikiwa zinaoneshwa kwa wapiga kura na mawakala.

Jambo la ajabu hapa kwetu, Tume ya Uchaguzi ya Mahera, msisitizo umekuwa eti mpiga kura akishapiga kura, aende nyumbani, yaani akimaanisha kuwa asishuhudie zoezi la uhesabuji wa kura. Huu nauita ni upuuzi. Unawalazimisha watu waende nyumbani, wasishuhudie process nzima, unataka kuficha nini?

Mtu mwadilifu, ungependa zoezi liwe la wazi sana ili hata mwenye kulalamika akose sababu, na watu wote au wengi inavyowezekana, wawe mashahuda wako kwa jinsi kila hatua, kila kitu kilivyofanyika kwa haki na kwa uwazi.

Wananchi tukatae amri ya kuondoka vituoni baada ya kupiga kura. Wapiga kura wawe huru kuondoka au kusalia maeneo ya upigaji kura alimradi wawe kwenye umbali ambao hauiingilii uhuru wa mtu kupiga kura au watendaji wa Tume kufanya shughuli zao.

Kwa nini tusiige mambo mazuri kama huo mfumo wa Nigeria wa kuhesabia kura hadharani? Kwa nini tunapenda kuiga mambo ya hovyo lakini tunakuwa na kigugumizi cha kuiga mambo mema na yenye tija?

Kama vyombo vya Serikali na taasisi zake, ikiwemo NEC, hawataki kuiga mambo mazuri, sisi wananchi tuna haki ya kuwalazimisha kwa namna zozote tunazoona ni sahihi.

Hata huko kwenye mataifa yaliyoendelea ambako wananchi wanathaminiwa sana katika maamuzi ya Serikali, siyo kwamba Serikali zilikuwa takatifu toka mwanzo, bali wananchi ndio waliozilazimisha ziwe kwa namna ambayo zipo leo. Hapa kwetu wananchi wanalazimishwa mambo ambayo Serikali inayataka. Hilo tulikatae kwa nguvu zetu zote.

Tunapoyakataa mabaya, huku tukiwa na dhamira njema ya kulifanya Taifa letu liwe imara zaidi, na upendo zaidi na umoja zaidi, lazima tutashinda. Siku zote Mungu husimama na watu wema, lakini hakudondoshei, bali hubariki jitihada zako unapopambania haki na wema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kuna alama ya ? Na ndiyo maana'wanawahitaji wapiga kura kwenye kupiga kura lakini kwenye kuhesabu eti hapana wadau wanauzoefu Wa kutosha
 
Hili Chama tawala hawatakubali..nashindwa kuelewa kwanini sheria inashindwa kutamuka kuwa Mara baada ya uchaguzi kuisha ni jukumu la tume kuhakikisha wananchi wanatangaziwa kwa kipaza Sauti matokeo yao kila kituo!

Pili nashindwa kuelewa kwnn sheria haitamuki wazi kuwa mfanyakazi wa tume hairuhusiwi kuwa mwanachama wa Chama chochote.
Nashindwa kuelewa wasomini watunga sheria kwnn elimu zao hazjamulika udhaifu huu.

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Hili Chama tawala hawatakubali..nashindwa kuelewa kwanini sheria inashindwa kutamuka kuwa Mara baada ya uchaguzi kuisha ni jukumu la tume kuhakikisha wananchi wanatangaziwa kwa kipaza Sauti matokeo yao kila kituo!

Pili nashindwa kuelewa kwnn sheria haitamuki wazi kuwa mfanyakazi wa tume hairuhusiwi kuwa mwanachama wa Chama chochote.
Nashindwa kuelewa wasomini watunga sheria kwnn elimu zao hazjamulika udhaifu huu.

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Chama tawala/NEC kama hawakubali basi wana dhamira chafu. Na sisi ni wajibu wetu nk kugomea dhamira hiyo dhamira mbaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu pamoja na hivo wameshachanganyikiwa , kwa panic walizonazo polepole na magu jinsi wanavyomwaza lissu wanaweza kumpigia kura wao wenyewe tar 28
 
Kikwete amewekwa sole-tape mdomo ni na ule ujenzi wa hekalu Kawe Beach.
 
Ni muhimu sana kuhakikisha mawakala wa Chadema hawafanyiwi figisu katika kituo chochote kile cha kupigia kura. Ikitokea mawakala wanafanyiwa figisu basi Wananchi wasimamishe upigaji kura mpaka pale watakapohakikishiwa mawakala wa Chadema wapo kutimiza wajibu wao bila figisu za aina yoyote ile.
 
Uchaguzi huu CCM inakwenda kushinda kwa kishindo kwakua upinzani nidhaifu kuliko wakati wowote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi.
 
Hawa majamaa huwa kama wako na chumaulete vile, awamu hii malaika wa vita wahusike katika hili ili kila atakaye jaribu kuchakachua akutane na bonge la kofi hata asijue lilikotoka.
 
Huu ni mwaka ambao CCM wamepiga kampeni wakiwa wame relax kwakua wamekosa ushindani.
 
Uchaguzi huu CCM inakwenda kushinda kwa kishindo kwakua upinzani nidhaifu kuliko wakati wowote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi.

Ww nakufananisha na vile vispika vidogo vidogo vya kutangazia bidhaa, vinarudia tangazo hilo hilo siku nzima. Haya maneno kayaongea Bashiru na ww unayarudia hivyo hivyo kama zuzu.
 
Hili Chama tawala hawatakubali..nashindwa kuelewa kwanini sheria inashindwa kutamuka kuwa Mara baada ya uchaguzi kuisha ni jukumu la tume kuhakikisha wananchi wanatangaziwa kwa kipaza Sauti matokeo yao kila kituo...
Wanasiasa wanatunga Sera ili wafanye siasa 'politicians they make policies to make politics'
 
Back
Top Bottom