Uchaguzi wa CHADEMA ngazi ya Taifa Sasa ni dhahiri timu mbili za Heche na Mbowe zaanza kutoshana nguvu moja yasikika toka Arusha nyingine toka Singida

John Heche ni mtu sahihi sana kwa nyakati hizi.

Freeman ni GOAT, ila ni wakati wa Heche kupokea vijiti,

Note: Kumpa mikoba Heche haimaanishi kuwa Freeman hafai LA HASHA, bali ni wajibu unaotokana na muda.
 
Kila la heri kwao kwa uchaguzi mkuu wa chama chao. Wamchague Mtu makini asiyenunulika na asiye mropokaji.
 
Swali ni moja kuna haja gan ya Mbowe kugombea tena ?

Haijalishi ni bora au sio bora vipindi vitatu vya uongozi vinatosha apishe aachie wengne waje na mawazo mapya
 
Uzi umekaa kinafiki sana, sema umecheza vizuri nimeshindwa kujua wewe ni chawa wa Mbowe au unamkejeli🤣
 
Heche hatoboi ila kiukweli ndiye anatufaa kwa sasa.
 
Tangu niwe na ufahamu kamili Sijawahi kuamini kama Mbowe ni Mpinzani, nadiriki kusema pia kuwa hata Lema anaweza asiwe Mpinzani wa Kweli!. Hawa ndugu wapo Kimaslahi zaidi, Mbaya zaidi hata kwenye Mazungumzo hawana hoja za kushawishi masikio ya watu (Nikosolewe if i am wrong).

Lissu ama Heche nikiri hawa Wanavutia kusikilizwa, wana hoja thabiti na mara nyingi hawatumii Matusi na Mihemko, akili zao zimetulia katika Kujenga hoja, Misimamo yao haiyumbishwi na Vipande vya Fedha ama dhahabu, Hawa wapo katika Njia ya Dr. Slaa, (Bahati Mbaya alikengeuka ingawa tunaweza kujustify kukengeuka kwake)!

Kwa upinzani Imara na kuondoa sintofahamu ya Demokrasia na Ukabila ndani ya Chama ni Vema Heche awe Mwenyekiti!

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!
 
MBOWE NI CHAWA WA MAMA
 

Ni muda sasa Mbowe awaachie wenzake kistaraabu na kuwaunga mkono kwa dhati kuendeleza chama. Hebu fikiria kama Chadema ingekuwa chini ya Lissu kuelekea 2025. Hizi ni faida:-

Chadema ingekuwa na misimamo thabiti.

Chadema ingekuwa na sera za kueleweka.

Asingekubali kurubuniwa na maridhiano, kwenda ikulu kupewa asali baada ya kutoka jela, kumkubali Sumaye na Lowassa.

Lissu asingekubali kuacha kudai katiba mpya mara baada ya kutoka jela na kukutana na SSH.

Chini ya Lissu naamini Chadema wasingekubali wagombea wao kuenguliwa na kubaki kimya. Pasingekalika.

Muhimu kuruhusu fikra mpya, wengine waongoze chama. Hiyo ndio demokrasia yenyewe. Angatuke kama Nyerere anaweza kuendelea kuwa Mshauri mkuu wa Chadema kama Nyerere alivyokuwa kwa CCM.
 
Bila Mbowe hakuna CHADEMA, Hakuna CHADEMA bila Mbowe sasa endeleeni kuijaribu sumu kwa kuilamba🐼
 
Bila Mbowe hakuna CHADEMA, Hakuna CHADEMA bila Mbowe sasa endeleeni kuijaribu sumu kwa kuilamba🐼
Kwahiyo unasemaje? Ni chama cha wanachama au chama cha Mbowe binafsi?

Bahati mbaya, akiumwa au akifariki na Chadema itakufa siku hiyo hiyo?
 
Mistake kubwa sana hii katika siasa za Mbowe!
Hata ile kutoka jela aliofungwa na Samia kwa makosa ya uongo ya ugaidi, wakati kosa lake la ukweli lilikuwa kudai katiba mpya na tume huru.

Alikuwa kwenye mkutano Mwanza kudai katiba mpya, tume huru alikuwa anaungwa mkono na Watanzania wengi. Wengi walimpigania atoke jela.

Sasa anatoka jela stop ya kwanza ikulu. Picha, asali, nusu mkate akaacha kupigania katiba mpya, tume huru akaingia kuwa chawa wa Samia kusifia, kutukuza, kumpa tuzo.

Hakukuwa na tofauti yoyote kati ya Mbowe, Kinana, Makamba, Nape, Lema, Mrema wote walikuwa worship and praise team ya Samia adui wao wore ilikuwa awamu ya tano. Hapo ndipo Mbowe alipoteza credibility yake yote kwa watu makini. Hayo ndio yalikuwa matunda, na makubaliano yao ya maridhiano.
 
Hii ndio maana ya uzalendo
 
well said Mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…