Huu uchaguzi haukupaswa kusimamiwa ngazi ya kitaifa kupitia TAMISEMI kama vile ambavyo imekuwa inafanyika au hata kupitia Tume Taifa ya uchaguzi kama ambavyo CHADEMA wanahitaji kuwa hivyo.
Huu uchaguzi ulipaswa kusimamiwa na Halmashauri za wilaya, miji na majiji kila moja ikifanya hivyo kwa wakati wake ndani ya miezi mitatu. Huo ndio ugatuzi wa madaraka na maana ya serikali za mitaa. Tofauti na hapo ni hadaa tu.