snow snow
Senior Member
- Sep 12, 2014
- 118
- 88
WAKATI Uganda inapata Uhuru wake mwaka 1962, akili za wakubwa wawili wa serikali mpya zilikuwa zinawaza mambo tofauti kuhusu muundo wa Jeshi la Uganda.
Rais wa kwanza, Edward Mutesa, kutoka kabila la Waganda na Waziri Mkuu wake, Apollo Milton Obote, walikuwa na picha tofauti kuhusu jeshi litalolinda Uhuru wa Uganda mpya.
Wanajeshi wengi walitoka Kaskazini mwa Uganda ambako alikuwa anatoka Obote. Watu wa kabila la Baganda anakotoka Mutesa hawakuwa na mahaba na kazi ya jeshi.
Kwa hiyo, Mutesa alitaka maofisa wa Kiingereza waendelee kubaki - akijua kwamba endapo wataondoka, nafasi zao zitachukuliwa na wanajeshi kutoka Kaskazini; jambo ambalo lingemwongezea nguvu zaidi Waziri Mkuu wakati huo ,Bwana Obote.
Kwa mujibu wa maandishi mbalimbali ya kihistoria, yalipotokea maasi ya wanajeshi ya mwaka 1964 - yaliyotokea pia Tanganyika na Kenya; askari wakidai malipo zaidi na wakitaka wazungu na watu wa rangi nyingine waliokuwa wakipendelewa na wakoloni kuondoka, Mutesa akawa katika wakati mgumu na Obote akatumia mwanya huo kwa faida yake.
Ni maasi hayo ndiyo yaliyokuwa chanzo cha kupandishwa cheo kwa Jenerali Idi Amini ambaye alikuwa kipenzi cha askari enzi hizo.
Ni huyuhuyu Amin ambaye baadaye alikuja kumpindua Obote, wakati alipokuwa rais wa Uganda. Amin naye akaja kupinduliwa na ushirikiano wa wanajeshi wa Tanzania na vikundi vya kijeshi vya Uganda.
Baadaye Uganda ikaja kuongozwa na Tito Okello aliyempindua mtawala wa kiraia, Godfrey Binaisa. Okello alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni kupitia vita vya msituni.
Hii ndiyo historia fupi ya makabila, jeshi na siasa za Uganda. Kujua hapa tulipo sasa, ni muhimu kurejea nyuma zaidi.
Hiba ya Wakoloni
Uganda ina makabila zaidi ya 20. Miongoni mwa makabila hayo, kabila la Baganda ndilo linaloongoza kwa kuwa na watu wengi, wasomi wengi zaidi na matajiri wengi kuliko makabila mengine ya taifa hilo.
Kabila hilo lina misingi yake katikati ya taifa hilo na liko katika eneo lenye rutuba ya kutosha na shughuli nyingi za kiuchumi.
Hata kabla Uganda haijapata Uhuru wake, watu wa kabila la Baganda tayari walikuwa wanamiliki shule, hospitali na taasisi nyingine za huduma za kijamii.
Wakati huohuo, wakati Waingereza wanaitawala Uganda, wakipendelewa sifa kadhaa za aina ya watu waliotaka wawe askari. Sifa kubwa ilikuwa kwenye maumbile na hawakuangalia sana uwezo wa kiakili.
Aina ya maumbile waliyokuwa wakiyapenda Wakoloni yalikuwa zaidi Kaskazini mwa Uganda kwenye makabila kama Langi (la Obote), Acholi na kabila la Lugbara ambako mama mzazi wa Idi Amin alikuwa anatokea.
Ni sawa tu na namna wakoloni haohao walivyofanya Tanganyika kwa kupendelea watu kutoka mkoani Mara kwa sababu za maumbile na ujasiri wao katika nyakati hizo.
Rais wa kwanza, Edward Mutesa, kutoka kabila la Waganda na Waziri Mkuu wake, Apollo Milton Obote, walikuwa na picha tofauti kuhusu jeshi litalolinda Uhuru wa Uganda mpya.
Wanajeshi wengi walitoka Kaskazini mwa Uganda ambako alikuwa anatoka Obote. Watu wa kabila la Baganda anakotoka Mutesa hawakuwa na mahaba na kazi ya jeshi.
Kwa hiyo, Mutesa alitaka maofisa wa Kiingereza waendelee kubaki - akijua kwamba endapo wataondoka, nafasi zao zitachukuliwa na wanajeshi kutoka Kaskazini; jambo ambalo lingemwongezea nguvu zaidi Waziri Mkuu wakati huo ,Bwana Obote.
Kwa mujibu wa maandishi mbalimbali ya kihistoria, yalipotokea maasi ya wanajeshi ya mwaka 1964 - yaliyotokea pia Tanganyika na Kenya; askari wakidai malipo zaidi na wakitaka wazungu na watu wa rangi nyingine waliokuwa wakipendelewa na wakoloni kuondoka, Mutesa akawa katika wakati mgumu na Obote akatumia mwanya huo kwa faida yake.
Ni maasi hayo ndiyo yaliyokuwa chanzo cha kupandishwa cheo kwa Jenerali Idi Amini ambaye alikuwa kipenzi cha askari enzi hizo.
Ni huyuhuyu Amin ambaye baadaye alikuja kumpindua Obote, wakati alipokuwa rais wa Uganda. Amin naye akaja kupinduliwa na ushirikiano wa wanajeshi wa Tanzania na vikundi vya kijeshi vya Uganda.
Baadaye Uganda ikaja kuongozwa na Tito Okello aliyempindua mtawala wa kiraia, Godfrey Binaisa. Okello alikuja kupinduliwa na Yoweri Museveni kupitia vita vya msituni.
Hii ndiyo historia fupi ya makabila, jeshi na siasa za Uganda. Kujua hapa tulipo sasa, ni muhimu kurejea nyuma zaidi.
Hiba ya Wakoloni
Uganda ina makabila zaidi ya 20. Miongoni mwa makabila hayo, kabila la Baganda ndilo linaloongoza kwa kuwa na watu wengi, wasomi wengi zaidi na matajiri wengi kuliko makabila mengine ya taifa hilo.
Kabila hilo lina misingi yake katikati ya taifa hilo na liko katika eneo lenye rutuba ya kutosha na shughuli nyingi za kiuchumi.
Hata kabla Uganda haijapata Uhuru wake, watu wa kabila la Baganda tayari walikuwa wanamiliki shule, hospitali na taasisi nyingine za huduma za kijamii.
Wakati huohuo, wakati Waingereza wanaitawala Uganda, wakipendelewa sifa kadhaa za aina ya watu waliotaka wawe askari. Sifa kubwa ilikuwa kwenye maumbile na hawakuangalia sana uwezo wa kiakili.
Aina ya maumbile waliyokuwa wakiyapenda Wakoloni yalikuwa zaidi Kaskazini mwa Uganda kwenye makabila kama Langi (la Obote), Acholi na kabila la Lugbara ambako mama mzazi wa Idi Amin alikuwa anatokea.
Ni sawa tu na namna wakoloni haohao walivyofanya Tanganyika kwa kupendelea watu kutoka mkoani Mara kwa sababu za maumbile na ujasiri wao katika nyakati hizo.