MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,104
- 6,827
Tume ya Uchaguzi nchini Kenya imetangaza kuahirishwa kwa uchaguzi wa marudio katika majimbo manne magharibi mwa nchi hiyo ambayo ni ngome ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga aliyetoa wito kwa wafuasi wake kususia uchaguzi wa leo.
Watu wawili wameuawa kwa kupigwa risasi wakati wa makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani katika maeneo hayo.
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati amesema tume imechukua hatua hiyo baada ya upigaji kura kutatizwa na ukosefu wa usalama.
Katika majimbo hayo ya Kisumu, Siaya, Migori na Homa Bay, wafuasi wa upinzani walifunga barabara za kuelekea katika vituo vya kupigia kura na kukabiliana na maafisa wa polisi siku yote.
Katika baadhi ya maeneo, makarani na maafisa wengine wa kupigia kura hawakufika vituoni kutokana na kile mmoja wa wasimamizi alisema ni kuhofia usalama wao.
Serikali ilikuwa imewatuma maafisa wa polisi katika maeneo mbalimbali kushika doria.
Gavana wa jimbo la Kisumu Prof Anyang' Nyongo amewatuhumu polisi kwa kutumia "magenge ya watu" kuwashambulia wafuasi wa upinzani.