Uchaguzi Mkuu wa klabu ya Yanga, uliosimamishwa kutokana na baadhi ya wanachama kufungua kesi Mahakamani, sasa umepangwa kufanyika Machi 10, mwaka huu
Awali, uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Januari 13, 2019 lakini uliahirishwa baada ya baadhi ya wanachama wa klabu hiyo kuweka pingamizi Mahakamani
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Ally Mchungahela, amesema leo watakutana na kamati mpya ya Yanga kujadili kwa pamoja hatima ya uchaguzi huo