Uchakachuaji wa kura afrika: Uchaguzi ulioingia kwenye Guiness Book of Records

Uchakachuaji wa kura afrika: Uchaguzi ulioingia kwenye Guiness Book of Records

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2011
Posts
3,763
Reaction score
5,607
CBD_King_of_Liberia.jpg

Huyu mbabe hapo juu anaitwa CHARLES D.B KING
Katika uchaguzi unaoitwa wa kidemokrasia 1927 nchini LIBERIA jamaa alimshinda mpinzani wake THOMAS J FAULKNER kwa kura zilizokuwa nyingi kuliko idadi ya watu waliojiandikisha.
Watu waliojiandikisha walikuwa 15000, Mbabe huyu akajishindia kiti cha urais kwa kura 240,000 huku mpinzani wake akijichukulia kula 9000. Huu ulikuwa uchaguzi wa mara ya tatu jamaa akitetea kiti chake, kwa kituko hiki Jamaa aliingizwa kwenye record za dunia.

Tusishangae kwa nini Afrika ni vigumu kumtoa mtu ambaye Tayari ni Rais na anatetea kiti chake.
 
CBD_King_of_Liberia.jpg

Huyu mbabe hapo juu anaitwa CHARLES D.B KING
Katika uchaguzi unaoitwa wa kidemokrasia nchini RIBERIA jamaa alimshinda mpinzani wake THOMAS J FAULKNER kwa kura zilizokuwa nyingi kuliko idadi ya watu waliojiandikisha.
Watu waliojiandikisha walikuwa 15000, Mbabe huyu akajishindia kiti cha urais kwa kura 240,000 huku mpinzani wake akijichukulia kula 9000. Huu ulikuwa uchaguzi wa mara ya tatu jamaa akitetea kiti chake.

Tusishangae kwa nini Afrika ni vigumu kumtoa mtu ambaye Tayari ni Rais na anatetea kiti chake.
"nchini RIBERIA"- nina mashaka na hii taarifa...
 
Hahaha! Hakika Jamaa alifanya Kituko sana. Waliojiandikisha 15,000 huku waliopiga kura halali 249,000. Bado ambazo zimeharibika.

Ninachokiona hapa,mpinzani wake alipata hizo kura 9000 huku yeye akiambulia kura Pungufu ya 6000 sasa kucheza Mazingaumbwe akazidisha idadi.
 
Hahaha! Hakika Jamaa alifanya Kituko sana. Waliojiandikisha 15,000 huku waliopiga kura halali 249,000. Bado ambazo zimeharibika.

Ninachokiona hapa,mpinzani wake alipata hizo kura 9000 huku yeye akiambulia kura Pungufu ya 6000 sasa kucheza Mazingaumbwe akazidisha idadi.
Mkuu hii kitu hata kama wangekuwepo waangalizi kutoka nje kama miaka hii, wangezimia wote
 
"nchini RIBERIA"- nina mashaka na hii taarifa...
Ni kweli nchini Liberia. Najua unatia shaka sababu ya jina la huyo rais na picha yake. Huyo alikuwa Mliberia-Mmarekani. Yaani baba au mama yake alikuwa na asili ya Marekani.

Ikumbubwe kuwa Liberia ni nchi iliyoundwa na jamii ya waliokuwa watumwa nchini Marekani ambao walirudi/walirudishwa Afrika baada ya kukoma kwa biashara ya watumwa.
 
Duuu....sijui tumerogwa nani yaani aliona ahaa unashinda Enhe basi nazidisha kura tuone ...kama mchezo wa watoto hivi
 
ha ha ha
hesabu zina wenyewe ye kazoea siasa, lbd na wafu walimpigia kura..!!
 
CBD_King_of_Liberia.jpg

Huyu mbabe hapo juu anaitwa CHARLES D.B KING
Katika uchaguzi unaoitwa wa kidemokrasia 1927 nchini LIBERIA jamaa alimshinda mpinzani wake THOMAS J FAULKNER kwa kura zilizokuwa nyingi kuliko idadi ya watu waliojiandikisha.
Watu waliojiandikisha walikuwa 15000, Mbabe huyu akajishindia kiti cha urais kwa kura 240,000 huku mpinzani wake akijichukulia kula 9000. Huu ulikuwa uchaguzi wa mara ya tatu jamaa akitetea kiti chake, kwa kituko hiki Jamaa aliingizwa kwenye record za dunia.

Tusishangae kwa nini Afrika ni vigumu kumtoa mtu ambaye Tayari ni Rais na anatetea kiti chake.
Nimemkubali kwenye huo mustachi..ha ha ha ha ha!
 
Haya mambo kwetu anayaweza j£¢ha kszi hii kwake ilikuwa rais yeye aliufuta kabisa uchaguzi
 
Si kituko kwani hata pale jirani wa marudio inasemaekana waliopiga kura ni 50000 ila mshindi katangazwa kwa kura 250k plus !
 
Back
Top Bottom