ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha kuona elimu yetu ambayo ilijengewa misingi bora na imara sasa inaangamia. Ikumbukwe kuwa mwalimu julius kambarage aliifanya elimu ya tanzania kuonekana nzuri na yakuigwa na mataifa mengne ya jumuia ya afrika mashariki mfano, uganda, kenya nk. Lakini leo unapoongea elimu ya tanzania imekuwa ikiangamia kila leo kwani imejaa siasa na kuonekana ni kichwa cha mwendawazimu, kila mtu anaiona elimu hii ni kitu cha kawaida. Serikali ijitathimin upya ili iweze kuokoa elimu yetu.