Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,234
- 1,815
Kitabu.Mossad
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Dibaji.
mwandishi anasema kuwa hiki kitabu ni mchanganyiko wa kazi za kutukuka zilizofanywa na Mossad,nafanikio na changamoto moto,mkusanyiko wa operesheni mbalimbali ambazo zimefanywa maeneo mbalimbali Duniani.
Mossad ni shirika la ujasusi la Uisraeli,ambalo ni miongoni mwa mashirika bora kabisa na ya kisasa katika mambo ya ujasusi.Shirila hili limefanya kazi kubwa ya kuifanya Israeli iwe ilivo leo,na limekuwa likilinda maslahi ya Uisraeli na mataifa ya magharibi hasa USA.
Novemba 12 mwaka 2011 ilitokea mlipuko mkubwa kwenye moja ya vinu vya kutengeneza silaha za maangamizi na masafa marefu Jijini Tehran nchini Iran.Mlipuko ule uliua baadhi ya wanajeshi wa Revolutionary Guards wa Iran,ingawa lengo la mlipuko halikulenga kuua binadamu tu bali kuharibu mfumo mzima wa mradi huo.Mradi huu ulilenga kuendeleza silaha za masafa marefu ambazo zingeweza kuipiga Marekani kutokea hapo jijini Tehran.Kwa muda mrefu sana Iran imekuwa na mradi mkubwa wa kuwa Taifa la kwanza la Mashariki ya Kati kuwa na silaha za kivita za masafa marefu(long-range misiles).Hivo Mossad walilipua hivo kuchelewesha kwa zaidi ya mwaka mpango huo
Wakati wa arab spring Misaada walionya nchi za Magharibi kuwa wasishangilie na kufikiri kuwa ni neema imewaangukia,Mossad walionya kuwa huo utakuwa mwanzo wa makundi yenye misimamo mikali,na mwanzo wa USA kukataliwa na wananchi kwenye eneo la mashariki ya kati,USA ulifurahi anguko la Mubarak huko Misri,lakini wale waandamanaji waliokusanyika Taharir square walikuwa wa kwanza kuchoma bendera ya Marekani,na uchaguzi uliofuatia ulishuhudia kundi la hasimu la USA kuingia madarakani yaani Muslimu brotherhood.Hata Libya baada ya kuangushwa kwa Gharadi makundi hasimu wa USA amezaliwa mengi,ndio kusema bora shetani unayemjua kuliko malaika usiyemjua
Chapter 1
King of shadows
Hili ni jina alipewa ofisa mmoja wa Mossad aliyekuwa anaitwa Meir Dagan.Huyu ofisa alikuwa na akili ya ziada katika kupambana na adui wa Israeli,alizaliwa mwaka 1945 ndugu zake wengi waliuwawa kwenye kambi za mateso na mauaji zama za chama cha Nazi huko Ujerumani.Wakati akikuwa alijiapiza kulinda Taifa la Israeli kwa gharama yoyote ile.
(kwa miaka mingi Waisrael wametumia mauaji hayo kupata public sympath) kama huku Afrika tunavyotumia Ukoloni kama sababu kuu ya kutokuendelea)
Huyu Bwana Degan alikuwa na kipaji cha kipekee sana katika uwanja wa vita.Miaka ya 1971 ni miaka ambayo Wapalestina walikuwa wanafanya mashambulizi ya kushtukiza kuwaua Waisraeli,walitumia mabomu ya kurusha kwa mikono,kujitoa muhanga,milipuko na njia yoyote ambayo waliona ni sawa,hii hali iliwalazimu Mossad kuanzisha kitengo kisicho rasmi kilichoitwa Rimon,hiki kitengo cha vijana werevu kiliundwa na Ariel Sharon alikuwa mkuu wa Mossad wakati huo,na Dagan akawa mmoja wa vijana wake. (Ariel Sharon alikuja kuwa waziri mkuu wa Israel,alieshinda iwa kura nyingi sana lakini akaharibu kwa kuwaondoa Waisraeli Gaza,baada ya hapo alikaa ICU akiwa mgonjwa sana kwa miaka nane,ndio binadamu mwenye rekodi ya kukaa ICU kwa muda mrefu zaidi tangu zamani za Pontio Pilato hata sasa)
Sasa huyu jamaa Dagan alifanya operesheni mbalimbali kwa mafanikio makubwa.Alikuwa na uwezo wa kujibadili kutokana na mazingira kama kinyonga.Mwaka 1971 Januari 2 aliongoza operesheni kinyonga.Operesheni hii ililenga kuwaua jamaa fulani hatari wa kundi la PLO,sasa hawa Mosad wakiongozwa na Mosad walikuwa na boat mbili moja ikiwa kama inakimbiza ingine kuelekea kwenye kambi ya wakimbizi wa Kipalestina,hii kambi ilikuwa jirani na fukwe yenye kijiji cha wavuvi..kwenye boat ya mbele alikuwa Degan aliyejifananisha na wapiganaji wa Wapelestina alipofika ufukweni alikimbia kuingia kambini kuomba msaada wa maficho,ile boat ya pili ilisimama majini.Sasa huyu bwana Degan alipata hifadhi huku alijitambulisha kwa majina ya Kipalestina na kuwa ametoka Lebanon kwenye kambi ya mafunzo(hawa wapalestina hawakutambuana kwa sura bali kwa ishara fula ni na majina ya viongozi wao)Degan alitumia udhaifu huo kujifannanisha na kupata fursa ya kujichanganya akiwa huko na bastola ambazo hazitoi sauti aliuwa yule aliyemkusudia kisha kutoroka kurudi kwenye eneo lake la kazi
Mwandishi anasema bwana Degani alipanda vyeo hadi kuja kuwa ndio kiongozi wa Rimon,alifanya Rimon kuwa tishio sana kwenye eneo la mashariki ya kati,wakuweza kupenya kwenye ngome ya adui kwa mtindo wao huo huo wa kinyonga.Wakati mwingine wakivaa kama adui na kuishi na adui.Hii iifanya wafanikiwe sana katika kuzuia mashambulizi yaliyokuwa yanafanywa kila siku na makundi mbalimbali ya wapelestina
Chapter 2
FUNERALS IN TEHRAN
Mwandishi anasema kuwa siku ya July 23, 2011, 1630 P.M.zilitokea pikipiki mbili katika viunga vya Jiji la Tehran wakampiga risasi mwanamume aliyekuwa herini kwake,akisubiri geti ufunguliwe aingie,kisha zile pikipiki zikatokomea kusikojulikana.Aliyeuwawa alikuwa niv Darioush Rezaei Najad, aliekuwa na miaka 45 profesa wa chuo kikuu.Huyu jamaa alikuwa mmoja wa wataalamu wa mpango wa Siri wa utengenezaji wa silaha za nyuklia nchini Iran.Kuuwawa kwa huyu mtaalam ulikuwa mwendelezo wa mauaji kadhaa ya watalaam wa mpango huu wa Iran,mauaji haya yalifanywa na Magharibi pamoja na washirika wake.
November 29, 2010, Mwanasayansi mwingine aliuwawa kifo cha ajabu tena,yeye akiwa barabarani na gari ikiwa inatembea ilitokea pikipiki ikapachika kifaa fulani kwenye kioo cha nyuma ya gari ya huyu mtaalamu,baada ya dakika chache ile gari ikalipuka ikiwa inatembea.Huyu profesa nae akasambaratika kabisa,kumbe ile pikipiki iliweka kifaa kilichosababisha huo mlipuko,Serikali ya Iran iliwanyooeshea mkono Mossad.Idadi ya waandamanaji waliouawa ilizidi kuongezeka na ilizidi kuwachanganya Iran maana baadhi ya waliouwawa walikuwa wanasayansi ambao Serikali iliwapa kazi nyingine hasa Uhadhiri wa vyuo vikuu,na huko walitakiwa kuwa wakosoaji wakubwa wa Serikali ili waonekane wapinzani wa utawala wa Irani.Mfano kuna jamaa aliitwa Mahmud Mohamed ambaye aliuwawa kwa mlipuko uliotegwa kwenye gari yake,baada ya kuuawa wengi wa rafiki zake walishindwa kuelewa lakini baadae kwenye mazishi nusu ya waombolezaji walikuwa maofisa wa Revolution Guard!
Kwa mujibu wa gazeti la London Telegraph mwaka 2007 liliripoti kuwa mauaji ya hawa wanasayansi wa Iran yalifanywa na Mossad ambayo kwa kipindi hicho Mkurugenzi wake alikuwa yule kijana matata Meir Dagan.Hii yote ikifanyika na vijana wa Dagaa kwa kutumia kitu walichoita Double Agent na Sleeping Agents.Mosad walifanikiwa kuweka mawakala wa Siri sana ambao walikuwa raia wa Iran na wengine walikuwa hao hao wanasayansi ambao walilipwa pesa nyingi ili kutoa taarifa
Hatua ya kwanza Mosad waliamua kuwaua kabisa wanasayansi wa Iran kama njia ya kuhujumu mpango wa Nyuklia wa Iran.Mosad walitumia njia kadhaa ikiwepo hujuma,operesheni za siri,mauaji,hadi ile maarufu ya kutengeneza virusi
Ni muhimu kukumbuka kuwa miaka ya 70 Iran ikiwa chini ya utawala wa Shah ilikuwa mshirika muhimu wa Ustawi,wakati wa vita ya Iran na Iraq Israel ilisaidia Iran sana hasa kijeshi,bahati mbaya utawala wa. Shah uliangushwa na Ayatollaa Khomein ambao hawakutaka ushirika na Israel hadi leo.Kufuatia kuuwawa kwa Wanasayansi wake wengi Iran ilibadilika mbinu ya urutubishaji wa Vinu hivi vya Nyukilia kwa kutengeneza vinu bandia ili kumchanganya adui,mbinu hii ilifanikiwa kwa kiasi fulani,mashirika ya Magharibi na Mosad hawakuweza kung'amua mara moja nini hasa kiliendelea Tehran
Wakati wa anguko la Soviet Irani ililitumia kama fursa kwa kuwanunua wanasayansi wa Soviet,kipindi hicho ilitokea wanasayansi wengi kutoweka nyumbani kwao hasa wanasyansi wa silaha za kibaolojia na silaha nyingine.Iran ilitumia fursa hii ya anguko la Soviet kimkakati sana
Mashirika mengi ya kijasusi yana mbinu ya kisasa sana ambayo huanzisha makampuni ya kutoa huduma mbalimbali haya makampuni yanaitwa Front companies sasa kazi ya haya makampuni ni kutafuta kazi mahususi kabisa kisha kutumia kazi hiyo kufanya upelelezi,kukusanya taarifa au kutengeneza vifaa hafifu kumshughulikia adui.Sasa basi Mosad walitengeneza kampuni ambayo ilikuwa iko Urusi ikimilikiwa na jamaa mmoja Mrusi na Mu Iran hii kampuni iliitwa Eastern European hii kampuni ilikubali kutengeneza vifaa kwa ajili ya Kinu cha Nantaz hiki kilikuwa Kinu kikubwa kuliko vyote,Iran ililazimika kutumia kampuni za Siri kwa kuwa walikuwa wamewekewa vikwazo.kumbe hii walikuwa wanajiweka mdomoni mwa adui,hii kampuni wamiliki wake walikuwa mawakala wa siri wa Mossad waliosambazwa Ulaya yote,hii Eastern European ilitengeneza vifaa vya maabara ya siri kisha kwenye hizi vifaa wakaweka shoti ya umeme,wanasayansi wa Iran hawakugundua hilo,hivi siku waliyopanga kuzindua rasmi,wakawasha ghafla kompyuta zote zenye taarifa maalum zikapigwa shoti na kulipuka,safari hii hakuna kifo ila mifumo yote iliharibika vibaya
Kwa miaka saba mfululizo Mossad waliendelea kufanya hujuma kwenye vinu na maabara za siri za Urai,pamoja na kuua watalaam,katika kipindi hiki zaidi ya wataalam wa hali ya juu wa Iran 240 waliuwawa kwa milipuko na njia mbalimbali ambazo hazikuacha alama.Mwaka 2007 Rais Bush wa USA alisaini mpango wa siri wa Rais wa kuruhusu CIA ianze operesheni mahususi kuzuia Iran isiendelee na mpango wake wa Nyukilia
Mwandishi anasema kuwa mwaka 2010 ulikuwa mgumu zaidi kwa Iran,uliosababishwa na vikwazo vilivyowekwa na UN hivo kusababisha Iran kushindwa kupata spea kwa ajili ya vifaa mbalimbali kwenye mpango wao wa Nyukilia. Mwaka huu 2010 Kirusi *Stuxnet virus* kilishambulia maelfu ya Komputa kwenye vinu vya Iran na kusababisha madhara na uharibifu mkubwa sana,kirusi hiki ni matokeo ya hujuma za Mossad na kilikuwa kirudi hatari zaidi kwenye mifumo ya Komputa Duniani,kwa kuwa kulikuwa hamuwezi wa kushambulia Komputa fulani..yani kilitumwa kwa komputa fulani,na kwenye hiyo Komputa kilielekezwa kuharibu nini,so kiliweza kuharibu mafaili fulani na kuacha faili fulani hata kwenye komputa moja.Ilikuwa pia vigumu kujulikana kikishaingia kwenye komputa
Mwandishi angurumisha chapter hii iwa kusema kuwa Magharibi na Mossad walifanikiwa tu kuchelewesha mipango ya Iran lakini sio kuiharibu kabisa,kwani walikuja kuendelea na mipango yao hasa baada ya shirika la UN la Nguvu za Atomic kuwachunguza na kusema kuwa hawakukuta kinu kwa matumizi ya kijeshi bali kiraia ambayo yanakubalika kisheria
Kitabu.Mosad
Mwandishi
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 3
A HANGING IN BAGHDAD
Mwandishi anasema kuwa kabla ya uhuru wa Taifa la Israel mwaka 1948,waisrael wengi walikuwa wanaishi kwenye jumuiya ndogo ndogo kwenye miji mingi Duniani.Ujerumani ilikuwa na Waisraeli wengi kuliko nchi nyingine yoyote ile.Katika hizi jumuiya walifundishana mambo mengi hasa ya ujasusi huku wakiwa na matumaini makubwa ya kurejea nchini kwao siku moja.Nchini Iraq kilikuwa kituo kikubwa baada ya Ujerumani ambako mto wa Bagdad ulijaa Waisrael wengi wakiwa katika idara nyeti za serikali na binafsi,kutokea Baghdad ambako waliishi kwa majina bandia ili wasijulikane walisambaa kwenye miji mbalimbali ya Mashariki ya Kati kwa lengo la kufunza kuhusu eneo hilo,ndio maana baada ya uhuru wameendelea kushinda vita kadhaa kutokana na kuwa na intelijensia ya kutosha kuhusu eneo hilo
Baada ya uhuru ilitokea vita kati yao na mataifa ya Kiarabu iliyodumu kwa mwaka mmoja,na Israel kupata waziri mkuu wa kwanza aliyeitwa Ben Gurion.Kipindi hiki walianzisha idara ya siri ya ujasusi,iliyoongozwa na Isser Beer huyu jamaa aliongoza Idara hii kwa mfano wa KGB ya Urusi.Kipindi hicho idara hii ilikuwa ikihisi kuna msaliti basi alikamatwa na kuhukumiwa kifo au kifungo cha maisha au kuuawa.Jamno hili lilikiuka msingi wa kuanzishwa kwa kwa Taifa changa la Israel.Hii iliwafanya watafakari njia mbadala ambayo itaheshimu utu wa watu wao hata pale wanapokea Taifa lao,ikaonekana kujenga mapenzi ya kweli kwa Taifa pamoja na uwajibikaji wa hali ya juu ndio vitakuza mapenzi na hivi kuondoa uwezekano wowote wa kununuliwa na nchi nyingine.
Baadaye sana iliundwa chombo kilichoitwa political research ambacho kilikuwa idara ya ujasusi,na baada ya ufanisi wakaja kuunda Mossad ambayo iliundwa kwa mujibu wa kitabu cha Bibilia takatifu
*Mithali:11.14
Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.*
ingawa mwandishi anasema hawafuati misingi tajwa
Chapter 4
A SOVIET MOLE AND A BODY AT SEA
Mwandishi anasema kuwa uanzishwajinwa Mossad haukuwa mrahisi hata kidogo,kulikuwa na watu wa ile idara ya siasa ambao hawakuafiki wazo la kuwa idara moja,maana walizoea kula.Pia kulikuwa na kusalitiana kwingi mno,ambako idara kama M16 ilikuwa inapambana kuweka watu wake ndani ya Mossad.Sovieti hawakuwa mbali pia!anatoa mfano wa jamaa mmoja Mwisarael aliyeitwa,Avin ambaye alikuwa na moyo wa kujitolea sana,kwenye Mossad na baadae akawa mwajiriwa wa sasa huyu bwana aliwekwa kituo cha kazi Yugoslavia ya zamani,kwa miaka mingi alikuwa anashawishi wakubwa zake wafungue kituo kikubwa hapo Yugoslavia bila mafanikio,aliporejea kwao ghafla alienda makao makuu ya Mossad ili aonane na Mkurugenzi kwa wakati huo alikuwa Bwana Harel ili kumshawishi kuwa wafungue kituo,alipofika ofisini alikutana nae sasa huyu Mkurugenzi hisia zake zikamwambia huyu ni msaliti,hapo hapo akamweka chimbua ulinzi na kumhoji baada ya kubanwa sana alikiri kuwa wakala wa Soviet,alifungwa miaka 14 hii ilikuwa miaka ya 1956
Mwandishi anasema kisa kingine ni cha kijana Israel huyu alikulia Sofia na baadaye akarejea Israel ambako alijiunga na jeshi la majini.Huyu kijana alikuwa na tabia za wakora,muhuni na mtu wa wanawake,alipokuwa Sofia alikutana na mchumba wa kikiristo aliyemtaja abadili dini ndio atamkubali bwana Israel hakusita mara moja akabadili dini kuwa Mkiristo kutoka dini yao ya Uyuda.Sasa aliporeja akamtelekeza huyu mchumba wake huko Sofia akiwa mjamzito,alifanya kazi jeshini lakini alikuwa mkora pia,akiwa Jerusalem alipata mchumba wa Kiisrael ambaye waliooana lakini baadaye miezi mitatu akampata mfanyakazi wa ubalozi wa Italy akamtaka tena huyu mtaliano akamtaka abadili dini jamaa akaenda kufoji jina akapewa jina la ambalo alikuwa mkiristo sasa akiwa nyumbani kwake ana jina la Kiisrael akiwa mtaani kwa mchumba ni Alexender Ivor mkiristo.Alipewa na pasipoti kupitia kina la pili ambalo halikufahamika kwa wengi.
Bwana alitoroka kwenda Roma bila kumwaga yeyote sio nyumbani wala kwa Bi wa Kiitaliano.Akiwa Roma alikutana na maofisa wa Ubalozi wa Misri wanaoshughulika na mambo ya kijeshi ambako walimpa dola elfu moja na mia tano(1500)akawapa taarifa muhimu za jeshi la Israel,hapo Roma wakala wa Mossad alikuwa na *connection* kubwa hivo haikupita muda akajulishwa kuwa kuna mtu anauza ramani ya jeshi,bila kupoteza kuda akatuma cable kwa wakubwa zake,ambao nao mara moja waliagiza afuatiliwe mara moja na kurudishwa Tel aviv.Hii ni moja ya operesheni yenye mafanikio makubwa na ambayo kwa mara ya kwanza Mossad walitoa kibali cha kukamata au kuua ikibidi!
Bwana Isirael alikuja kukamatwa jijini Paris baada ya kukubali lift tax aliposhuka uwanjani akitokea Austria.Alipelekwa kwenye moja ya nyumba hapo Paris na baada ya mahojiano alikiri kuuza taarifa kwa Misri na alikuwa aende Misri kukutana na wakuu wa serikali huko ili apate hela zaidi.Ikaamuliwa asafirishwe hadi Tel Aviv akashtakiwe.Alipandishwa kwenye ndege ya shirika la ndege la Israel ambayo ingesimama kujaza mafuta Roma,kisha Athens ndio itue Tel Aviv,ili kupandisha ndege ilibidi afungwe kwenye box kama kifurushi.Akiwa angani Mossad walikuwa na daktari ambaye alikuwa akimchoma sindano za usingizi!bahati mbaya zile sindano na hali ya hewa vilimzidia hivo akafa,licha ya jitihada za kuokoa maisha,ndege ilitua Tel aviv na baada ya kushusha mizigo na abiria wote,wakuu Wa Mossad walielekeza hiyo ndege ipae na hiyo mauti hadi baharini kwenye kina kirefu kisha waitupe huko baharini! Ndio ilifanyika hivo
Mwandishi.Michael Bar Zohar & Nissim Mishal
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Dibaji.
mwandishi anasema kuwa hiki kitabu ni mchanganyiko wa kazi za kutukuka zilizofanywa na Mossad,nafanikio na changamoto moto,mkusanyiko wa operesheni mbalimbali ambazo zimefanywa maeneo mbalimbali Duniani.
Mossad ni shirika la ujasusi la Uisraeli,ambalo ni miongoni mwa mashirika bora kabisa na ya kisasa katika mambo ya ujasusi.Shirila hili limefanya kazi kubwa ya kuifanya Israeli iwe ilivo leo,na limekuwa likilinda maslahi ya Uisraeli na mataifa ya magharibi hasa USA.
Novemba 12 mwaka 2011 ilitokea mlipuko mkubwa kwenye moja ya vinu vya kutengeneza silaha za maangamizi na masafa marefu Jijini Tehran nchini Iran.Mlipuko ule uliua baadhi ya wanajeshi wa Revolutionary Guards wa Iran,ingawa lengo la mlipuko halikulenga kuua binadamu tu bali kuharibu mfumo mzima wa mradi huo.Mradi huu ulilenga kuendeleza silaha za masafa marefu ambazo zingeweza kuipiga Marekani kutokea hapo jijini Tehran.Kwa muda mrefu sana Iran imekuwa na mradi mkubwa wa kuwa Taifa la kwanza la Mashariki ya Kati kuwa na silaha za kivita za masafa marefu(long-range misiles).Hivo Mossad walilipua hivo kuchelewesha kwa zaidi ya mwaka mpango huo
Wakati wa arab spring Misaada walionya nchi za Magharibi kuwa wasishangilie na kufikiri kuwa ni neema imewaangukia,Mossad walionya kuwa huo utakuwa mwanzo wa makundi yenye misimamo mikali,na mwanzo wa USA kukataliwa na wananchi kwenye eneo la mashariki ya kati,USA ulifurahi anguko la Mubarak huko Misri,lakini wale waandamanaji waliokusanyika Taharir square walikuwa wa kwanza kuchoma bendera ya Marekani,na uchaguzi uliofuatia ulishuhudia kundi la hasimu la USA kuingia madarakani yaani Muslimu brotherhood.Hata Libya baada ya kuangushwa kwa Gharadi makundi hasimu wa USA amezaliwa mengi,ndio kusema bora shetani unayemjua kuliko malaika usiyemjua
Chapter 1
King of shadows
Hili ni jina alipewa ofisa mmoja wa Mossad aliyekuwa anaitwa Meir Dagan.Huyu ofisa alikuwa na akili ya ziada katika kupambana na adui wa Israeli,alizaliwa mwaka 1945 ndugu zake wengi waliuwawa kwenye kambi za mateso na mauaji zama za chama cha Nazi huko Ujerumani.Wakati akikuwa alijiapiza kulinda Taifa la Israeli kwa gharama yoyote ile.
(kwa miaka mingi Waisrael wametumia mauaji hayo kupata public sympath) kama huku Afrika tunavyotumia Ukoloni kama sababu kuu ya kutokuendelea)
Huyu Bwana Degan alikuwa na kipaji cha kipekee sana katika uwanja wa vita.Miaka ya 1971 ni miaka ambayo Wapalestina walikuwa wanafanya mashambulizi ya kushtukiza kuwaua Waisraeli,walitumia mabomu ya kurusha kwa mikono,kujitoa muhanga,milipuko na njia yoyote ambayo waliona ni sawa,hii hali iliwalazimu Mossad kuanzisha kitengo kisicho rasmi kilichoitwa Rimon,hiki kitengo cha vijana werevu kiliundwa na Ariel Sharon alikuwa mkuu wa Mossad wakati huo,na Dagan akawa mmoja wa vijana wake. (Ariel Sharon alikuja kuwa waziri mkuu wa Israel,alieshinda iwa kura nyingi sana lakini akaharibu kwa kuwaondoa Waisraeli Gaza,baada ya hapo alikaa ICU akiwa mgonjwa sana kwa miaka nane,ndio binadamu mwenye rekodi ya kukaa ICU kwa muda mrefu zaidi tangu zamani za Pontio Pilato hata sasa)
Sasa huyu jamaa Dagan alifanya operesheni mbalimbali kwa mafanikio makubwa.Alikuwa na uwezo wa kujibadili kutokana na mazingira kama kinyonga.Mwaka 1971 Januari 2 aliongoza operesheni kinyonga.Operesheni hii ililenga kuwaua jamaa fulani hatari wa kundi la PLO,sasa hawa Mosad wakiongozwa na Mosad walikuwa na boat mbili moja ikiwa kama inakimbiza ingine kuelekea kwenye kambi ya wakimbizi wa Kipalestina,hii kambi ilikuwa jirani na fukwe yenye kijiji cha wavuvi..kwenye boat ya mbele alikuwa Degan aliyejifananisha na wapiganaji wa Wapelestina alipofika ufukweni alikimbia kuingia kambini kuomba msaada wa maficho,ile boat ya pili ilisimama majini.Sasa huyu bwana Degan alipata hifadhi huku alijitambulisha kwa majina ya Kipalestina na kuwa ametoka Lebanon kwenye kambi ya mafunzo(hawa wapalestina hawakutambuana kwa sura bali kwa ishara fula ni na majina ya viongozi wao)Degan alitumia udhaifu huo kujifannanisha na kupata fursa ya kujichanganya akiwa huko na bastola ambazo hazitoi sauti aliuwa yule aliyemkusudia kisha kutoroka kurudi kwenye eneo lake la kazi
Mwandishi anasema bwana Degani alipanda vyeo hadi kuja kuwa ndio kiongozi wa Rimon,alifanya Rimon kuwa tishio sana kwenye eneo la mashariki ya kati,wakuweza kupenya kwenye ngome ya adui kwa mtindo wao huo huo wa kinyonga.Wakati mwingine wakivaa kama adui na kuishi na adui.Hii iifanya wafanikiwe sana katika kuzuia mashambulizi yaliyokuwa yanafanywa kila siku na makundi mbalimbali ya wapelestina
Chapter 2
FUNERALS IN TEHRAN
Mwandishi anasema kuwa siku ya July 23, 2011, 1630 P.M.zilitokea pikipiki mbili katika viunga vya Jiji la Tehran wakampiga risasi mwanamume aliyekuwa herini kwake,akisubiri geti ufunguliwe aingie,kisha zile pikipiki zikatokomea kusikojulikana.Aliyeuwawa alikuwa niv Darioush Rezaei Najad, aliekuwa na miaka 45 profesa wa chuo kikuu.Huyu jamaa alikuwa mmoja wa wataalamu wa mpango wa Siri wa utengenezaji wa silaha za nyuklia nchini Iran.Kuuwawa kwa huyu mtaalam ulikuwa mwendelezo wa mauaji kadhaa ya watalaam wa mpango huu wa Iran,mauaji haya yalifanywa na Magharibi pamoja na washirika wake.
November 29, 2010, Mwanasayansi mwingine aliuwawa kifo cha ajabu tena,yeye akiwa barabarani na gari ikiwa inatembea ilitokea pikipiki ikapachika kifaa fulani kwenye kioo cha nyuma ya gari ya huyu mtaalamu,baada ya dakika chache ile gari ikalipuka ikiwa inatembea.Huyu profesa nae akasambaratika kabisa,kumbe ile pikipiki iliweka kifaa kilichosababisha huo mlipuko,Serikali ya Iran iliwanyooeshea mkono Mossad.Idadi ya waandamanaji waliouawa ilizidi kuongezeka na ilizidi kuwachanganya Iran maana baadhi ya waliouwawa walikuwa wanasayansi ambao Serikali iliwapa kazi nyingine hasa Uhadhiri wa vyuo vikuu,na huko walitakiwa kuwa wakosoaji wakubwa wa Serikali ili waonekane wapinzani wa utawala wa Irani.Mfano kuna jamaa aliitwa Mahmud Mohamed ambaye aliuwawa kwa mlipuko uliotegwa kwenye gari yake,baada ya kuuawa wengi wa rafiki zake walishindwa kuelewa lakini baadae kwenye mazishi nusu ya waombolezaji walikuwa maofisa wa Revolution Guard!
Kwa mujibu wa gazeti la London Telegraph mwaka 2007 liliripoti kuwa mauaji ya hawa wanasayansi wa Iran yalifanywa na Mossad ambayo kwa kipindi hicho Mkurugenzi wake alikuwa yule kijana matata Meir Dagan.Hii yote ikifanyika na vijana wa Dagaa kwa kutumia kitu walichoita Double Agent na Sleeping Agents.Mosad walifanikiwa kuweka mawakala wa Siri sana ambao walikuwa raia wa Iran na wengine walikuwa hao hao wanasayansi ambao walilipwa pesa nyingi ili kutoa taarifa
Hatua ya kwanza Mosad waliamua kuwaua kabisa wanasayansi wa Iran kama njia ya kuhujumu mpango wa Nyuklia wa Iran.Mosad walitumia njia kadhaa ikiwepo hujuma,operesheni za siri,mauaji,hadi ile maarufu ya kutengeneza virusi
Ni muhimu kukumbuka kuwa miaka ya 70 Iran ikiwa chini ya utawala wa Shah ilikuwa mshirika muhimu wa Ustawi,wakati wa vita ya Iran na Iraq Israel ilisaidia Iran sana hasa kijeshi,bahati mbaya utawala wa. Shah uliangushwa na Ayatollaa Khomein ambao hawakutaka ushirika na Israel hadi leo.Kufuatia kuuwawa kwa Wanasayansi wake wengi Iran ilibadilika mbinu ya urutubishaji wa Vinu hivi vya Nyukilia kwa kutengeneza vinu bandia ili kumchanganya adui,mbinu hii ilifanikiwa kwa kiasi fulani,mashirika ya Magharibi na Mosad hawakuweza kung'amua mara moja nini hasa kiliendelea Tehran
Wakati wa anguko la Soviet Irani ililitumia kama fursa kwa kuwanunua wanasayansi wa Soviet,kipindi hicho ilitokea wanasayansi wengi kutoweka nyumbani kwao hasa wanasyansi wa silaha za kibaolojia na silaha nyingine.Iran ilitumia fursa hii ya anguko la Soviet kimkakati sana
Mashirika mengi ya kijasusi yana mbinu ya kisasa sana ambayo huanzisha makampuni ya kutoa huduma mbalimbali haya makampuni yanaitwa Front companies sasa kazi ya haya makampuni ni kutafuta kazi mahususi kabisa kisha kutumia kazi hiyo kufanya upelelezi,kukusanya taarifa au kutengeneza vifaa hafifu kumshughulikia adui.Sasa basi Mosad walitengeneza kampuni ambayo ilikuwa iko Urusi ikimilikiwa na jamaa mmoja Mrusi na Mu Iran hii kampuni iliitwa Eastern European hii kampuni ilikubali kutengeneza vifaa kwa ajili ya Kinu cha Nantaz hiki kilikuwa Kinu kikubwa kuliko vyote,Iran ililazimika kutumia kampuni za Siri kwa kuwa walikuwa wamewekewa vikwazo.kumbe hii walikuwa wanajiweka mdomoni mwa adui,hii kampuni wamiliki wake walikuwa mawakala wa siri wa Mossad waliosambazwa Ulaya yote,hii Eastern European ilitengeneza vifaa vya maabara ya siri kisha kwenye hizi vifaa wakaweka shoti ya umeme,wanasayansi wa Iran hawakugundua hilo,hivi siku waliyopanga kuzindua rasmi,wakawasha ghafla kompyuta zote zenye taarifa maalum zikapigwa shoti na kulipuka,safari hii hakuna kifo ila mifumo yote iliharibika vibaya
Kwa miaka saba mfululizo Mossad waliendelea kufanya hujuma kwenye vinu na maabara za siri za Urai,pamoja na kuua watalaam,katika kipindi hiki zaidi ya wataalam wa hali ya juu wa Iran 240 waliuwawa kwa milipuko na njia mbalimbali ambazo hazikuacha alama.Mwaka 2007 Rais Bush wa USA alisaini mpango wa siri wa Rais wa kuruhusu CIA ianze operesheni mahususi kuzuia Iran isiendelee na mpango wake wa Nyukilia
Mwandishi anasema kuwa mwaka 2010 ulikuwa mgumu zaidi kwa Iran,uliosababishwa na vikwazo vilivyowekwa na UN hivo kusababisha Iran kushindwa kupata spea kwa ajili ya vifaa mbalimbali kwenye mpango wao wa Nyukilia. Mwaka huu 2010 Kirusi *Stuxnet virus* kilishambulia maelfu ya Komputa kwenye vinu vya Iran na kusababisha madhara na uharibifu mkubwa sana,kirusi hiki ni matokeo ya hujuma za Mossad na kilikuwa kirudi hatari zaidi kwenye mifumo ya Komputa Duniani,kwa kuwa kulikuwa hamuwezi wa kushambulia Komputa fulani..yani kilitumwa kwa komputa fulani,na kwenye hiyo Komputa kilielekezwa kuharibu nini,so kiliweza kuharibu mafaili fulani na kuacha faili fulani hata kwenye komputa moja.Ilikuwa pia vigumu kujulikana kikishaingia kwenye komputa
Mwandishi angurumisha chapter hii iwa kusema kuwa Magharibi na Mossad walifanikiwa tu kuchelewesha mipango ya Iran lakini sio kuiharibu kabisa,kwani walikuja kuendelea na mipango yao hasa baada ya shirika la UN la Nguvu za Atomic kuwachunguza na kusema kuwa hawakukuta kinu kwa matumizi ya kijeshi bali kiraia ambayo yanakubalika kisheria
Kitabu.Mosad
Mwandishi
Mchambuzi.Nanyaro EJ
Chapter 3
A HANGING IN BAGHDAD
Mwandishi anasema kuwa kabla ya uhuru wa Taifa la Israel mwaka 1948,waisrael wengi walikuwa wanaishi kwenye jumuiya ndogo ndogo kwenye miji mingi Duniani.Ujerumani ilikuwa na Waisraeli wengi kuliko nchi nyingine yoyote ile.Katika hizi jumuiya walifundishana mambo mengi hasa ya ujasusi huku wakiwa na matumaini makubwa ya kurejea nchini kwao siku moja.Nchini Iraq kilikuwa kituo kikubwa baada ya Ujerumani ambako mto wa Bagdad ulijaa Waisrael wengi wakiwa katika idara nyeti za serikali na binafsi,kutokea Baghdad ambako waliishi kwa majina bandia ili wasijulikane walisambaa kwenye miji mbalimbali ya Mashariki ya Kati kwa lengo la kufunza kuhusu eneo hilo,ndio maana baada ya uhuru wameendelea kushinda vita kadhaa kutokana na kuwa na intelijensia ya kutosha kuhusu eneo hilo
Baada ya uhuru ilitokea vita kati yao na mataifa ya Kiarabu iliyodumu kwa mwaka mmoja,na Israel kupata waziri mkuu wa kwanza aliyeitwa Ben Gurion.Kipindi hiki walianzisha idara ya siri ya ujasusi,iliyoongozwa na Isser Beer huyu jamaa aliongoza Idara hii kwa mfano wa KGB ya Urusi.Kipindi hicho idara hii ilikuwa ikihisi kuna msaliti basi alikamatwa na kuhukumiwa kifo au kifungo cha maisha au kuuawa.Jamno hili lilikiuka msingi wa kuanzishwa kwa kwa Taifa changa la Israel.Hii iliwafanya watafakari njia mbadala ambayo itaheshimu utu wa watu wao hata pale wanapokea Taifa lao,ikaonekana kujenga mapenzi ya kweli kwa Taifa pamoja na uwajibikaji wa hali ya juu ndio vitakuza mapenzi na hivi kuondoa uwezekano wowote wa kununuliwa na nchi nyingine.
Baadaye sana iliundwa chombo kilichoitwa political research ambacho kilikuwa idara ya ujasusi,na baada ya ufanisi wakaja kuunda Mossad ambayo iliundwa kwa mujibu wa kitabu cha Bibilia takatifu
*Mithali:11.14
Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.*
ingawa mwandishi anasema hawafuati misingi tajwa
Chapter 4
A SOVIET MOLE AND A BODY AT SEA
Mwandishi anasema kuwa uanzishwajinwa Mossad haukuwa mrahisi hata kidogo,kulikuwa na watu wa ile idara ya siasa ambao hawakuafiki wazo la kuwa idara moja,maana walizoea kula.Pia kulikuwa na kusalitiana kwingi mno,ambako idara kama M16 ilikuwa inapambana kuweka watu wake ndani ya Mossad.Sovieti hawakuwa mbali pia!anatoa mfano wa jamaa mmoja Mwisarael aliyeitwa,Avin ambaye alikuwa na moyo wa kujitolea sana,kwenye Mossad na baadae akawa mwajiriwa wa sasa huyu bwana aliwekwa kituo cha kazi Yugoslavia ya zamani,kwa miaka mingi alikuwa anashawishi wakubwa zake wafungue kituo kikubwa hapo Yugoslavia bila mafanikio,aliporejea kwao ghafla alienda makao makuu ya Mossad ili aonane na Mkurugenzi kwa wakati huo alikuwa Bwana Harel ili kumshawishi kuwa wafungue kituo,alipofika ofisini alikutana nae sasa huyu Mkurugenzi hisia zake zikamwambia huyu ni msaliti,hapo hapo akamweka chimbua ulinzi na kumhoji baada ya kubanwa sana alikiri kuwa wakala wa Soviet,alifungwa miaka 14 hii ilikuwa miaka ya 1956
Mwandishi anasema kisa kingine ni cha kijana Israel huyu alikulia Sofia na baadaye akarejea Israel ambako alijiunga na jeshi la majini.Huyu kijana alikuwa na tabia za wakora,muhuni na mtu wa wanawake,alipokuwa Sofia alikutana na mchumba wa kikiristo aliyemtaja abadili dini ndio atamkubali bwana Israel hakusita mara moja akabadili dini kuwa Mkiristo kutoka dini yao ya Uyuda.Sasa aliporeja akamtelekeza huyu mchumba wake huko Sofia akiwa mjamzito,alifanya kazi jeshini lakini alikuwa mkora pia,akiwa Jerusalem alipata mchumba wa Kiisrael ambaye waliooana lakini baadaye miezi mitatu akampata mfanyakazi wa ubalozi wa Italy akamtaka tena huyu mtaliano akamtaka abadili dini jamaa akaenda kufoji jina akapewa jina la ambalo alikuwa mkiristo sasa akiwa nyumbani kwake ana jina la Kiisrael akiwa mtaani kwa mchumba ni Alexender Ivor mkiristo.Alipewa na pasipoti kupitia kina la pili ambalo halikufahamika kwa wengi.
Bwana alitoroka kwenda Roma bila kumwaga yeyote sio nyumbani wala kwa Bi wa Kiitaliano.Akiwa Roma alikutana na maofisa wa Ubalozi wa Misri wanaoshughulika na mambo ya kijeshi ambako walimpa dola elfu moja na mia tano(1500)akawapa taarifa muhimu za jeshi la Israel,hapo Roma wakala wa Mossad alikuwa na *connection* kubwa hivo haikupita muda akajulishwa kuwa kuna mtu anauza ramani ya jeshi,bila kupoteza kuda akatuma cable kwa wakubwa zake,ambao nao mara moja waliagiza afuatiliwe mara moja na kurudishwa Tel aviv.Hii ni moja ya operesheni yenye mafanikio makubwa na ambayo kwa mara ya kwanza Mossad walitoa kibali cha kukamata au kuua ikibidi!
Bwana Isirael alikuja kukamatwa jijini Paris baada ya kukubali lift tax aliposhuka uwanjani akitokea Austria.Alipelekwa kwenye moja ya nyumba hapo Paris na baada ya mahojiano alikiri kuuza taarifa kwa Misri na alikuwa aende Misri kukutana na wakuu wa serikali huko ili apate hela zaidi.Ikaamuliwa asafirishwe hadi Tel Aviv akashtakiwe.Alipandishwa kwenye ndege ya shirika la ndege la Israel ambayo ingesimama kujaza mafuta Roma,kisha Athens ndio itue Tel Aviv,ili kupandisha ndege ilibidi afungwe kwenye box kama kifurushi.Akiwa angani Mossad walikuwa na daktari ambaye alikuwa akimchoma sindano za usingizi!bahati mbaya zile sindano na hali ya hewa vilimzidia hivo akafa,licha ya jitihada za kuokoa maisha,ndege ilitua Tel aviv na baada ya kushusha mizigo na abiria wote,wakuu Wa Mossad walielekeza hiyo ndege ipae na hiyo mauti hadi baharini kwenye kina kirefu kisha waitupe huko baharini! Ndio ilifanyika hivo