Uchanganyaji wa lugha

Fubu G

Senior Member
Joined
Oct 7, 2012
Posts
110
Reaction score
18
Utasikia mtu anachanganya kiswahili na lugha zngne za kigen kwa nn.? Msaada tafadhali
 
Mkuu Fubu G,

Nadhani kuna sababu nyingi,

1. Mtu kutofahamu lugha nyingine vyema(yaani anaongea kiswahili, lakini ni lugha yake ya pili au ya tatu).

2. Mtu ambaye lugha yake ya Kiswahili ni ya kwanza lakini bado ina mapungufu(ukosefu wa maneno kwa ufasaha zaidi).

3. Tabia: Kwa wale wenye tabia ya kuongea lugha ya kigeni(mf. Kiingereza/Kifaransa/Kihispania/Kidachi n.k) kwa kuhisi itawafanya wawe katika tabaka fulani(hasa watu wa juu/wenye uelewa n.k) katika jamii.

4. Mazoea: Yaani mtu kutumia maneno kwa kusikia kila mara mtu akiyatumia bila kuwa na uelewa au ufahamu kuwa ni maneno ya lugha ya kigeni.

na sababu nyingine nyingi mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…