Uchimbaji wa Visima Virefu vya Maji Umeanza Ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini

Uchimbaji wa Visima Virefu vya Maji Umeanza Ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

UCHIMBAJI WA VISIMA VIREFU VYA MAJI UMEANZA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Jumatatu, 26.8.2024, Mkuu wa Wilaya ya Musoma (DC), Dkt Khalfany Haule amepokea na kushuhudia gari lenye mtambo wa uchimbaji wa visima virefu vya maji ukianza kazi kwenye Kata ya Bugwema ya Jimboni mwetu.

Jimbo letu litachimbiwa visima vitano (5) - taarifa kutoka kwa Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Musoma, Injinia Edward Sironga

Baadae, maji kutoka kwenye visima virefu vinavyochimbwa yatasambazwa kwa mabomba ndani ya vijiji venye visima hivyo.

Mbali ya upatikanaji wa maji kutoka visima virefu, vijiji vyetu vyote 68 vinayo miradi ya kusambaziwa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria. Miradi hii iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji wake.

CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa:
Tafadhali sikiliza shukrani nyingi za wananchi kwa Serikali yetu kutoka kwenye CLIP/VIDEO hii - muongeaji wa hitimisho kwenye CLIP/VIDEO hii ni DC Mhe Dkt Khalfany Haule.

Soma Pia: Vijiji vya Jimbo la Musoma Vijijini Vyaendelea Kusambaziwa Maji ya Bomba Kutoka Ziwa Victoria

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
26.8.2024

 
Na uchaguzi ni 2025. Mlikua wapi kabla?
All the best
 

UCHIMBAJI WA VISIMA VIREFU VYA MAJI UMEANZA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Jumatatu, 26.8.2024, Mkuu wa Wilaya ya Musoma (DC), Dkt Khalfany Haule amepokea na kushuhudia gari lenye mtambo wa uchimbaji wa visima virefu vya maji ukianza kazi kwenye Kata ya Bugwema ya Jimboni mwetu.

Jimbo letu litachimbiwa visima vitano (5) - taarifa kutoka kwa Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Musoma, Injinia Edward Sironga

Baadae, maji kutoka kwenye visima virefu vinavyochimbwa yatasambazwa kwa mabomba ndani ya vijiji venye visima hivyo.

Mbali ya upatikanaji wa maji kutoka visima virefu, vijiji vyetu vyote 68 vinayo miradi ya kusambaziwa maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria. Miradi hii iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji wake.

CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa:
Tafadhali sikiliza shukrani nyingi za wananchi kwa Serikali yetu kutoka kwenye CLIP/VIDEO hii - muongeaji wa hitimisho kwenye CLIP/VIDEO hii ni DC Mhe Dkt Khalfany Haule.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
26.8.2024
aibu kubwa sana, maji ya ziwa yamefika tabora hapo tu jirani unajitapa kuchimba visima
aibu sana
 
Back
Top Bottom