Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

unaleta taarifa ambazo hujazifanyia utafiti.Labda utafiti wako unaufanyia hapa JF.haya maelezo yako yanaangukia neno lako kwamba ni ngano.Unachojaribu kuandika kipeleke kwa Mohamed Said akusahihishe kama anavyofanya hapa

Wewe nae ni mzigo hapa,bora ungekaa kimya na kufatilia huu mkanasha kwa karibu
 
Last edited by a moderator:

Asante sana mheshimiwa, kwakweli nimesoma hii makala nzuri na nimefarijika sana!

Yericko wewe ni mwanahistoria wa kweli uliyekuja kuzima kelele za wadini kama Mohamed Said.

Asante sana kkwa elimu hii isiyopatikana chuoni au popote pale isipokuwa JF
 
Hakika nafurahiiswa sana na weledi wako na majibu yako muruwa na wengi tunanufaika na darsa lako. Kama nilivyowahi bainisha huko awali kuwa Y Nyerere hajafanya utafiti wowote katika maandiko yake ndio maana yanakuwa na mashaka mashaka na kutofahamu vizuri hata wale anaowazungumzia majina yao na hata familia zao. nashukuru kwa msaada mkubwa unaompa kwa nia ya kumsaidia na hiyo kama atakuwa ametulia itambidi nae afanye utafiti wa kina na kuleta hoja mbadala kama atazipata. Shukran kwa darsa lako na Allah akuzidishie zaidi na zaidi
 
Mzee Mohamed Said,
Unachomkosea Mwalimu katika maandiko yako mengi ni kujaribu kuingia hadi akilini mwake na kueleza hisia zake kama vile wewe ni yeye. Hii sio sahihi hata kidogo. Haukuwahi kuwa karibu na Mwalimu. Wazee wako hawa ndio walookuwa karibu naye. Wao ndio waliokusimulia mengi kuhusu Mwalimu. Wewe kwa agenda yako hii ya UISLAM ukachagua ya kuandika na ukayaita historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
kama utamsoma Ahali yangu Mohammed Said kwa NIA ya kumuelewa basi utafahamu mengi sana kutoka kwake kwani ameshehemi weledi mkubwa katika historia ya Tanganyika hususan Dar es Salaam ambako kilitua kitovu cha harakati zote za uhuru wa Tanganyika. Lakin kama utamsoma kwa NIA ya kupinga hapo utapata taabu kubwa sana kwani yeye ni mtafiti naa kisa hicho cha miaka ya 50's sio tu amesikia kutoka kwa wazee wake laki naye aliona kwa macho yake. Hivyo utafiti wake ni wa kuona na kusimuliwa na wazee wake. hakuna agenda yoyote hapo zaidi ya UKWELI mtupu uliofichwa.
 


naam,ndugu moh' bin said anawapa fact kwa ushahid maridhawa,kwani hawakawii kusema wapewe miujiza kama walipewa wale wazee wa zama kwa zama waliotangulia na waliokawahi kuish ulimwenguni hapa kabla yao.,
na wao wanakiri wazi wazi manufaa ya darasa hili wanalopewa japo hawayakinishi kwa vinywa vyao hapa hadhwarani.
 

Ndugu yangu, bado hujapembuka katika mizania ya historia,

Tumia mda mwingi kujisomea hayo niliyokupa yatakupembua na kukupevusha!

Nilichokupa ni ushiriki wa kanisa katika harakati za ukombozi Tanganyika ambayo Mohamed Said aliyaghiribu katika kitabu chake,
 
Mkuu naomba utupe 'darsa' kwa faida ya wengi,kunaweza ibuka mkanasha mwingine hapa ninavyoona
Watu tunaongopeana sana humu wakati mwingine. Uliza tu swali hili dogo: Mwingereza alipigana na Mtanganyika yupi katika huko wanakoita "kupigania uhuru" wa Tanganyika? Tanganyika haikuwa koloni la Mwingereza. Mwalimu na wenzake walifanya kazi rahisi na ndogo sana ya kuikumbusha UN kwamba sasa tuko tayari kujitawala WATANGANYIKA wenyewe. Mwingereza wala hakuleta ubishi wowote.

Mwalimu alianza kutofautiana na wenzake kuanzia mwaka 1958 kwenye kura tatu na kabla ya hapo alipomwangusha Abdu kwenye kinyang'anyiro cha urais wa kwanza wa TANU. Watu wakaanza kutazama wapi pa kuangukia. Baadhi wakaona UISLAM wao ungeweza kuwaweka pamoja. Hawakuweza.
 
huyohuyo nyerere ndo aliyetoa kibari cha kukamatwa muft wa wakat huo kwa madai anataka kuihuju serikali hali iliyopelekea IGP wa wakat huo akatae na nyerere kuamuru maafisa usalama wamkamate. MFUMO SASA BASI
 

Karibu sana mkuu, tunahuisha kwa kifupikipifupi historia ya Uhuru wetu!
 
mbona povu linakutoka,vumilia utapona japo dawa chungu.Waite na wengine mje msome kwa mwanahistoria Mohamed Said,watu wanastafidi sana hapa jamvini.Mwenzio Yeriko kaja kulitetea kanisa nalo eti lilipigania uhuru wa tanganyika.Teh teh teh kazi kwelikweli,kapewa jina la sheikh hata hajulikani kajaribu kufananiza lakini kaumbuliwa
Wewe ni mpuuzi kama hujui kitu nyamaza, Yericko kawaumbueni kwa uongo wenu!
 
Last edited by a moderator:
Ni kupembuka gani huko unakodai?. Kwani kwa wasomi tunajibu TAFITI kwa TAFITI na wala sio TAFITI kwa kejeli au maneno ya mitaani. sasa nilichobainisha ni kuwa Unachoandika wewe kina mashaka mashaka na hakina utafiti wa aina yoyote ndio maana unakosema majina na hata status za watu mfano shaikh Idrisa bin Saad n.k Mimi nakushauri kama msomi fanya tafiti kidogo na wewe na kuja na paper ambayo utaweza kuitetea kwetu ili upingane na Mohamed said. Huo ni ushauri wangu kwako.
 

Sio muamini wa viroja, bali mimi ni muamini wa mang'amuzi ya nera!

Una haki yakutomjua Shehe Issa bin Amir kwakuwa umelishwa yamini kwa ngano za chukizo!

Shehe Issa mmoja wa wasomi wakiislamu wa mwanzo kabisa mwishoni mwa himaya ya dola ya kijerumani aliyejengwa kwa busara ya pwani, ndie aliyekuwa tunu ya hekima za waungwana mnamo miaka ya 1928 hadi miaka ya 1950!

Ikiwa utaonyesha nidhamu ya majadiliano,

Nikipata wasaa nitakupa habari za shehe huyu ambae alikuwa kiungo muhimu kati ya kanisa na uislam Tanganyika!
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said , mimi bado nipo kwenye papers zako..sijui mnaziitaje kwa kiarabu...
Nilikuwa naomba ufafanuzi kidogo kwenye kipande nilichoweka hapo chini. Umeelezea kifo cha Kighoma Malima halafu baada ya kifo tu ukaweka hiyo sentensi ya Cardinal Polycarp Pengo kutoa tamko kuhusu kumdhibiti Kighoma Malima kwa sababu uamuzi wake wa kugombea nje ya CCM.
Hii ni style ya uandishi wako tu au ulikuwa unalenga kulihusisha Kanisa na kifo cha Malima kwa kuchomeka hiyo sentensi ya mwisho?
Kwa sababu hilo tamko ni shutuma nzito kwa cardinal , unaweza ukatuonyesha ni wapi iwe kwenye gazeti au record yeyote aliposema hayo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…