Eti ndo mwalimu wako anakufananisha na Nguruvi3!
My foot!
wewe ni bure kabisa
Kichwa cha habari
"Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar."
Ila kama ungekuwa umenisoma tangu mwanzo ungenielewa.
Ngoja nijaribu
Katika huu uzi, mengi yameongelewa, na mimi katika kuufuatilia nikakuta kitu kilicho ni intrigue.
Madai ya dhulma kwa waislamu.
Ndo hilo lililo nileta hapa.kuja kuuona huo ushaidi wa dhulma kutoka kwa wale wanao dai upo. Mi nimesema sijaona bado hiyo dhulma lakini inawezekana ipo, ila mpka ushahidi usiopingika.
Sasa kama basi la mbagala nililodandia litageuza na kwenda Tegeta basi ntageza nalo. Si ili mradi kufika.
We umesema wakati Kambona akihutubia ulikuwa nje ya nchi mimi nilihudhuria mkutano wa Jangwani na Mwalimu alijibu hotuba ya Kambona na zaidi alimtetea Kawawa kwa shutuma hizo sasa ukiletewa ushahidi utaamini? mwaka 1999 Mkapa alitaka ushahidi wa kisayansi wa dhulma dhidi ya Waislamu na alipopewa hakuamini! hata mkipewa ushahidi hamtaamini kwani Mwenye enzi Mungu ktk kitabu chake kitukufu sura ya 2 mwanzoni kabisa mwa sura anasema Wasioamini hata ukiwathibitishia hawataamini!
Kama Bwana Mkubwa kasema hayo tutegemee haya toka kwenu!
tofauti yake ni nini?Darsa, si "darasa".
Darsa, si "darasa".
We umesema wakati Kambona akihutubia ulikuwa nje ya nchi mimi nilihudhuria mkutano wa Jangwani na Mwalimu alijibu hotuba ya Kambona na zaidi alimtetea Kawawa kwa shutuma hizo sasa ukiletewa ushahidi utaamini? mwaka 1999 Mkapa alitaka ushahidi wa kisayansi wa dhulma dhidi ya Waislamu na alipopewa hakuamini! hata mkipewa ushahidi hamtaamini kwani Mwenye enzi Mungu ktk kitabu chake kitukufu sura ya 2 mwanzoni kabisa mwa sura anasema Wasioamini hata ukiwathibitishia hawataamini!
Kama Bwana Mkubwa kasema hayo tutegemee haya toka kwenu!
P. Fm,
Mpuuze tu, yeye anakubali zaid tafiti za kina sivalon, van bargan, njozi, na mod said.
Hawezi kumkuli mushi na ivi anatokea kasikazini ndo balaa.
Hawa watu wanachuki kubwa na ukatoriki na wanachukia sana watu wa kasikazini bila sababu za msingi.
Achana nae.
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُواْ سَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ لاَ يُؤْمِنُونَHakika wale walio kufuru ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawaamini (Qur2:06)خَتَمَ اللَّهُ عَلَى قُلُوبِهِمْ وَعَلَى سَمْعِهِمْ وَعَلَى أَبْصَارِهِمْ غِشَاوَةٌ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa. (Qur2:07)
JEURI YA FIRAUNI ILIVYOSHINDWA
Firauni alitakabari na kujitangazia uungu.Kwa hofu ya kutokea mtu mwengine kuupinga uungu wake akawa anawachinja watoto wote wa kiume waliozaliwa kwenye nchi ya Misri.Kwa hekima za Mwenyezi Mungu hakuweza kumchinja Mussa (A.S) na bila kujua akamlea ndani ya nyumba yake.
Musa (A.S) alikuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu aliyepewa miujiza.Miujiza yake mikubwa ilikuwa kwenye fimbo yake.Akapewa amri aende yeye na nduguye Haruna kwa Firauni wakampe khabari za kuwepo Mwenyezi Mungu aliye mkuu na muumba wa kila kitu.Hii ikawa mwanzo wa ugomvi wake na Musa (a.s).Miujiza ya Musa (a.s) akaita ni uchawi tu.Ikiwa ni uchawi yeye aliamini ana wachawi wakubwa zaidi na wengi.
Upatu ukapigwa kote mjini watu waje uwanjani kushuhudia uchawi wa Musa (a.s) utakavyopondwa pondwa na kumaliza madai yake ya utume.Wachawi wa Firauni wakakusanywa na kualikana.Siku ilipofika Firauni akakaa kwenye kiti chake cha enzi kushuhudia pambano baina ya Musa a.s dhidi ya wachawi wa Firauni.
Uwanja ulikuwa umejaa kweli hata pa kutia mguu hakuna.Wachawi wa Firauni wakaanza pambano kwa kutupa fimbo zao zilizogeuka nyoka wa kutisha.Zamu ya Musa a.s ilipofika akatupa fimbo yake ikageuka joka kubwa likameza wale nyoka wote wa wachawi wa Firauni.
Wachawi hapo hapo wakageuka kuwa waumini wa Musa a.s..Firauni akafedheheka kwa kushindwa kuthibitisha kuwa Musa a,s ni mchawi.
Akahamaki na kuwaambiwa wachawi wake kwanini wamemuamini Mus a.s kabla ya idhini yake.Wachawi wakajibu IMANI KWA MWENYEZI MUNGU HAIHITAJI IDHINI KUTOKA KWA YEYOTE.
ukweli waliouona kwa macho yao unatosha.
Mwenye kujua kiarabu angalia VIDEO HAPA
Ritz
Sivalon na Van Bergen wakiandika habari za pwani ndio unaamini?
Mushi akiandika, inakuwa si kweli, sasa kwanini tuamini ngano za Mmanyema Moh Said kuhusu Tabora, Bukoba, Musoma, Mbeya??????
Tafakari! Jichukulie hatua!
Kadogoo
Moh Said ametoa kitabu chake mwaka 1998. Kambona according to you aliwaenzi wapigania uhuru wanaotajwa na Mohamed Said mwaka 1992.Sasa lawama za kusema hawa watu wamefutwa kwenye historia zinakujaje? Mbona kwenye thread hii na zilizotangulia, wafuasi wa Moh Said wanadai kuwa mashujaa hao wametajwa kwa mara ya kwanza na Moh Said? Au kwa sababu Oscar Kambona alikuwa Mgalatia, kwa hiyo hamtaki sifa ziende kwa mgala, sifa ni za Moh Said tu?
Mkuu kwa uelewa wangu nadhan unatakiwa kuangalia na kuthibitisha kilichoandikwa na Mushi ni sahihi au la. Mazingira anayotoka Mushi Au Mo Said hayathibitishi kile walichokiandika ni sahihi au la! Bali ni utafiti ndio unaothibitisha, Mtu anaweza akatoka mwambao akaenda kufanya utafiti machame na akathibitisha kilo alichofanyia kazi na vivyo hivyo wa Kaskazin anaweza enda kusini. Kwahiyo kitu cha msingi ni kuangalia hoja ina mashiko na si mazingira ambayo mtu ametokea.
Tatizo mnapenda kumeza ngano nzima nzima muulize huyo Mag3 alioleta ngano za Mushi.
Tumia akili yako tu Mushi anasema kabla ya uhuru madhebu ya Wakirsto yalikuwa yanashinda kusomesha. Swali baada ya uhuru Tanzania tulikuwa na wasomi wangapi wenye elimu ya chuo kikuu.
Watu wanapokea ngano za Mushi sababu Mkristo mwenzao.
Lawama zinakuja sababu kitabu kimeandikwa kivukoni na kutambulika kama historia rasmi ya wapigania uhuru! Kambona hakuandika kitabu bali aliwataja hao wazee ili kushawishi wakazi wa Dar wakiunge mkono chama chake tena aliwataja kwa majina lakini Nyerere alipowaaga Wazee wa Dar mwaka 1985 ktk hotuba yake hakuwataja wapigania uhuru kwa majina bali aliwaita Waislamu watupu! Mohamed Saidi kaandika kitabu ili kukanusha kitabu kilicho andikwa kivukoni! hoja sio kuwataja bali kuandika kitabu! nacho kimeandikwa na MS lakini hamkiamini! lakini Kambona na Nyerere wamewataja mnaamini kizungumkuti hicho!
kingine walikuwa hawataki vijana wao wale vyakula haramu, mfano Nguruwe maarufu kama kitimoto au mdudu.
Waislamu tusitafute mchawi nani kwenye huu mfumo uliopo, ni mlimbikizo wa makosa ya wazee wetu miaka mingi imepita sasa, naweza kusema, wachawi wa tatizo hili ni sisi wenyewe waislamu, hakuna swala la Mwl. Nyerere.
Kadogoo
Sehemu kubwa ya stories za Moh Said kuhusu matukio na majina ya watu, zinaweza kuwa factual na hatuna tatizo nazo.
Ritz,Kama wewe unavyouchukia Uislam na Waislam.
Kama ni hivyo unakubali kuwa Nyerere sio muasisi wa TANU? unakubali kuwa waasisi wengi wa TAA na TANU na wapigania uhuru walikuwa Waislamu? kitabu cha Kivukoni kinamtaja Nyerere ndie mwanzilishi wa Tanu na nyote mnaamini hivyo! kwanini tunawadanganya wa TZ kwa kuwalisha historia hewa?
Mohamed Said kaandika historia halisi lakini mnamwita mdini na mchochezi! sasa thibitisha udini na uchochezi wake!
Darsa, si "darasa".
Lawama zinakuja sababu kitabu kimeandikwa kivukoni na kutambulika kama historia rasmi ya wapigania uhuru!