Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mwandishi mwenyewe unayemtarajia ni huyu anayewatukana wapigania uhuru kama alivyofany baba yake.Unadhani ataweza.Laana ya hao wazee itamwandama yeye na baba yake mpaka siku ya mwisho.
Na sidhani kuwa Mohammed atamjibu mjinga kama huyu.
Adabu ni kitu chamsingi sana katika mjadala huu, wengi wameadhibiwa hapa kwamjibu wa sheria za jf kwautovu wa nidhamu kama huo unaouonyesha hapa.


Mods wapo makini wanakuona kile ukisemacho.
 

Nguruvi,

Umeandika maneno mengi sana.
Ni vigumu kukujibu nukta kwa nukta.

Umezungumzia maandamano kuwa sishiriki maandamano.

Hunijui...
Na wala sina haja ya kukueleza.

Umezungumza mimi kupanda ndege kwenda nchi za nje na kuwaacha ndugu zangu.

Hili nitakujibu.

Maandamano ya kwanza tumetokea Mtoro 1993.
Mabucha ya nguruwe.

Siku chache kabla nilikuwa nimetoka safari...Dar- Paris - Le Havre - Paris - London - Cardiff - London -
Dar - Zanzibar.

Zanzibar ndiyo sakata la OIC nilikwenda kuchapa majibu kwa Kanisa na Serikali katika Khayria Press na
mimi ndiye nilorudi na majibu hayo ambayo tuliyagawa kwa Wabunge wakati huo Bunge linakaa
Karimjee Hall.

(Nina paper nzima kuhusu OIC Insha Allah kama wanaukumbi watapenda nitaiweka jamvini.)

Nimefika Dar nimearifiwa mkutano wa dharura wa kuwawekea dhamana masheikh wetu waliokamatwa kwa
kuvunjwa kwa mabucha ya nguruwe.

Sina haja ya kukeleza nini kilitokea siku ile katika msikiti wa Mtoro ambao mimi nikiswali pale toka utoto wangu.

Sheikh Waziri Ramadhani ex - police officer ndiye aliyewasomea Waislam Qur'an na alichagua aya mnasaba na
hali iliyokuwapo siku ile.

Ilisomwa dua kubwa na tuliondoka kwa maandamano kuelekea Central Police.

Mbele yetu ndugu yetu tukimwita kwa jina la Darwesh alikuwa amebeba bendera ya kitambaa cheusi imeandikwa:
Lailaha Ilallah Muhammad Rasulullah.

Allah siku ile alijibu dua yetu pale pale.
Tumeondoka msikitini jua kali.

Tunafika Uhuru na Titi Street mawingu yanatanda na mvua ikaanza kunyesha.
Tulipambana na polisi Clock Tower na mabomu ya machozi yalirindima.

Ile mvua na upepo ukawa unapeperusha mabomu yale mbali na Waislam.
Nilikuwapo pale.

Mwenzangu alikamatwa na ndiyo ikawa sababu ya yeye kufungwa na kupoteza kazi bank.

Mimi baada ya mapambano yale nilirudi nyumbani kubadili nguo na kujitayarisha zaidi nikaja Mtoro.

Mnazi Mmoja nikakutana na rafiki yangu akanisihi nisende msikitini Mtoro kwa kuwa FFU wamezingira msikiti.

Nilimjibu kuwa nachelea kukimbia vita Allah ananiona.
Sikuweza kufika msikitini kwa kuwa Mtaa wa Mahiwa, Livingstone, Narung'ombe yote ilikuwa imefungwa...

Huwa sipendi kusema haya lakini nimeona nikueleze unijue.

Uoga si katika sifa zangu na ndiyo maana unaona nimeingia hapa na jina langu kamili bila kificho.

Wakuogopewa ni Allah SW pekee na Yeye kaweka ahadi kuwa atakaemuogopa atamfanya asiogope
chochote duniani.

Nami natamani niwe katika wale wasiomwogopa yeyote katika binadamu.
Nadhani tumefahamiana.

Mengine ulosema ni yale yale majibu ni yale yale tunazungusha humo kwa humo.

Nguruvi,
Cheza na watu saizi yako.
 
Hahaahaa Mohamed Said kwa ngano wewe ni nooooooma!

Hayo unayoyanena kwamapambo ya lugha huku ukiweka ukubwa wa mapambano ambapo ni dhahiri unatushairisha kuwa ulipigana vita ya ardhini mpaka ukaenda kubadili nguo ni sehemu ya mafundusho ya kuwajasirisha vijana wako kupambana na dola.

Kwamwerevu atakuona unamatatizo ya kimfumo, hasa pale unapozidisha uongo wa eti mpaka ukaenda kubadilisha kombati, kisha ukarudi kwenye uwanja wa mapambano, watu wakakusihi usiende lakini ukaaoa kwa mungu wako, hata pale polisi walipouzingira msikiti wakizuia binadamu yoyote asiingie wala kutoka, lakini wewe uliufikia msikiti huo kwa mapambano na ukashinda.



Hahaas nabaki kucheka tu hizi ngano kwakweli,
 
Mzee Said, kwanini wewe hukwenda na kuwa shahidi wa kuwatetea hawa vijana walioambatana na Ponda? Kwanini mmemshakizia Mzee Waikela kufanya kile ambacho wewe ulitakiwa kukifanya? Ungeweza kuwa 'expert witness' kutokana na ujuzi wa 'historia' ya mgongano ndani ya Waislamu nchini.
 
 
Adabu ni kitu chamsingi sana katika mjadala huu, wengi wameadhibiwa hapa kwamjibu wa sheria za jf kwautovu wa nidhamu kama huo unaouonyesha hapa.


Mods wapo makini wanakuona kile ukisemacho.
Kumbe hukujuwa uzito wa tusi lako kwa wazee hao uliposema

Naomba kuwajua hao waislamu wanafiki ambao mzee huyo wa Tabora aliwataja wote hapo mahakamani.
Hii adhabu ya mods ikinipata sishangai.Tumezoea ya kule Mbagala,Mwanza na Changombe.
 

Maajabu nikuwa eti kila siku anapiga magoti akimuomba mungu ili awe shahidi,

Haya ni maajabu ya karne, hivi kwenda pale kisutu nakumuona hakimu ukamweleza kuwa unataka kuwa shahidi kuna ugumu gani?

Je ni kweli Mohamed anataka kutuaminisha kuwa ameshindwa kuwaambia mawakili wa Shehe Ponda kuwa anataka kuwa shahidi wa Ponda?
 
Kumbe hukujuwa uzito wa tusi lako kwa wazee hao uliposema


Hii adhabu ya mods ikinipata sishangai.Tumezoea ya kule Mbagala,Mwanza na Changombe.
Shehe Waikela ndiebkasema pale mahakamani kuwa kulikuwa na waislamu wanafiki, na Mohamed amesema wazi kuwa Mzee Waikela aliwataja, nami nikaomba atutajie hapa jamvini.

Kabla hujakurupuka kujibu kitu tulia na usome kwa uelewa sawia ndugu.
 
Hawa wazee ni hazina kubwa ya ukweli kwa Tanzania waliobakia.
Laiti serikali ingekuwa inatafuta ukweli basi kwa upande wa historia ya waislamu na kudhulumiwa kwao sheikh Waikela angewakilisha wale wengi waliotangulia.
Kwa upande wa muungano basi serikali ingetosheka kuwa haukuwa wa haki na ulikuwa ni ujanja na njama kwa kumsikiliza Hassan Nassor na mwenzake Abdulla Rashid.
Tatizo serikali imeshikilia kulinda mzimu hivyo ina vitu vyake mfukoni inavyopania kuvichomeka katikati ya matatizo yaliyopo nchini.
Kwanini hawa wazee wamepewa umru mrefu.Kwanini Mohammed na Alghasany wameweza kuandika historia si bure na si uhodari wao pekee.Hiyo ni mipango ya Mungu subhaanahu wa taala na huruma zake kwa walimwengu ili ukweli ujulikane na uongo ushindwe.
Ndio maana nazidi kumuasa sheikh wangu Mohammed azidi kushukuru na asijali kejeli za wanaJF waliotumwa na mfumokristo kukandamiza historia ya waislamu ili warudie uluwa wao ulio hatarini kupotea Tanzania baada ya kugundulika kwamba sasa waislamu wameamka.Wao wameogopa historia ya Mohammed zaidi na kusahau mambo mengine mengi yanayowapa ushujaa waislamu kujitetea.
 

Ngongo,

Sema utakavyosema.
Hivi wewe una makamu gani khasa ya kumfunza Sheikh Waikela?

Hivi kibri kimekufikisha hapo hata kuona hawa wazee waliopigania
uhuru hawajui kitu unakuja na maneno ya kutufunza sie kipi tuseme
mahakamani?

Ama kweli...

Wewe unajiona mjuzi wa kumfundisha Sheikh Waikela...
 

Ami,
Insha Allah.

Tutaelimishana taratibu.
Uzi huu naambiwa na wenyeji haujapatapo kutokea.

Nina mengi.
 
Mohamed, hivi maandamano ya kuvunja mabucha yalianzia kwa Mtoro?

Mimi nina temerity ya kusema mbona saizi yangu ni wewe!
 
 
Mohamed, hivi maandamano ya kuvunja mabucha yalianzia kwa Mtoro?
Mohamed, kuna swali hili naona unajaribu kulikwepa. Nikukumbushe kuwa umelileta wewe hivyo ufafanuzi tafadhali.

Maandamano ya kuvunja mabucha yalianza Msikiti wa Mtoro?
 
Mohamed, kuna swali hili naona unajaribu kulikwepa. Nikukumbushe kuwa umelileta wewe hivyo ufafanuzi tafadhali.

Maandamano ya kuvunja mabucha yalianza Msikiti wa Mtoro?

Maandamano ya kuvunja mabucha yalianza Msikiti wa Mtoro?[/QUOTE]

Nguruvi,

Siku vijana walipokwenda kuvunja mabucha hawakwenda kwa maandamano.

Mandamano yalianza Msikti wa Mtoro siku ya pili kwenda polisi kuwatoa masheikh
waliokamatwa usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi baada ya kuvunjwa mabucha.

Kuna pp niliwasilisha Chuo Kikuu cha Kenyatta kuhusu kuvunjwa kwa mabucha na
matokeo yake: Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the
Pork Riots of 1993.
(Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern
Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21[SUP]st[/SUP] Century 1[SUP]st [/SUP]- 3[SUP]rd[/SUP] August 2006,
Kenyatta University, Nairobi.

Kukwepa swali kwa kuogopa kitu gani?

Mimi nasimama kwenye vyuo kote huko najibu maswali ya watu wenye kujua nije
nikimbie swali hapa free for all?
 
Kumbe hukujuwa uzito wa tusi lako kwa wazee hao uliposema


Hii adhabu ya mods ikinipata sishangai.Tumezoea ya kule Mbagala,Mwanza na Changombe.

Ami,

Huyo mtoto ambaye anamsingizia Kambarage baba yeye anawatukana wazee wetu wala hakuna anayemkataza wewe kumwambia afanye adabu anakutisha na mods.

Unajua hawa wamezoea kubebwa kila sehemu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…