WildCard, hata usisumbue akili yako...huyu mchochezi
Mohamed Said ni mtu wa ajabu sana na hatari lakini taratibu wengine tunaanza kuigundua janja yake na hila zake...kamwe si bure.
- Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu mwanzilishi na Raisi wa kwanza wa AA mwaka 1929, Mwalimu Cecil Matola wala msaidizi wake Makamu wake Ramadhani Ali! Cha ajabu anamtambua katibu wake Kleist Sykes na kumpa heshima zote za uasisi eti toka akiwa Burma!
- Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu muasisi na Raisi wa kwanza wa TAA wa kuchaguliwa mwaka 1950 Dr. Vedasto Kyaruzi wala Makamu wake! Cha jabu anamtambua katibu wake Abdulwahid Sykes mtoto wa Kleist Sykes na kumpa sifa zote za kuongoza mabadiliko ndani ya TAA!
- Kwa makusudi kabisa hamtambui kiongozi mkuu muasisi na Raisi wa kwanza wa TANU mwaka 1954 Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wala Makamu wake John Rupia na badala yake sifa zote zinaelekezwa kwa katibu Abdulwahid Sykes, kipenzi cha wengi aliyekuwa na mvuto wa pekee!
Sasa hapa swali linakuja, kwa nini ameamua kupindisha mambo hivyo? Huyu
Mohamed Said, mtoto wa Kimanyema, mbona anawatetea sana hawa Wazulu ambao hata kwenye Uislaam hasemi waliingia lini na kwa sababu zipi? Ana uchungu gani? Uhusiano kati ya koo hizi mbili unatokana na nini?
Kwa nini anafanya sana jitihada za kuwaengua viongozi wa juu waanzilishi wa
AA, TAA na
TANU na badala yake anawapa sifa wasaidizi wao? Toka lini Katibu anakuwa na nafasi ya juu kuliko Raisi/Mkurugenzi? Kwa mfano;
- Amewahi kudai kuwa pamoja na msomi Mwalimu Cecil Matola kuwa Raisi muasisi wa AA hakuwa chochote bali ni katibu wake Kleist Sykes aliyepanga na kuiendesha AA.
- Amewahi hata kudai kuwa mwaka 1950 ni katibu wa TAA Abdulwahid Sykes ndiye alimteua bosi na Raisi wake Dr Vedasto Kyaruzi kwenye kamati iliyoandaa mikakati na malengo ya TAA.
- Amewahi kudai kuwa pamoja na Mwalimu Nyerere kuchaguliwa kuwa Raisi muasisi wa TANU mwaka 1954 ni katibu wake Abdulwahid Sykes ndiye aliyesimamia mipango yote ikiwa ni pamoja na kumuandalia hotuba aliyoisoma UN.
- Amewahi kudai kuwa pamoja na Makamu wa TANU mwaka 1954 kuwa mfanya biashara mkuu mwenye uwezo mkubwa kifedha, John Rupia lakini ni Abdulwahid Sykes na ndugu zake ndio waliokuwa wakitoa fedha zao kuiendesha TANU.
- Amewahi kudai kuwa pamoja na Mwalimu Nyerere kulipwa mshahara mkubwa wakati huo, hakuweza kujitosheleza hata kwa nauli achilia mbali kununua mboga hadi mchuuzi wa Kariakoo Mshume Kiyate alipomfadhili.
- Amewahi kudai kuwa pamoja na msomi Mwalimu Nyerere kuanza siasa toka akiwa chuoni Makerere kwenye miaka ya 1940s ilibidi apigwe msasa, kupewa shule na kufundishwa ustaarabu na wazee wa Gerezani kuhusu siasa!
Huyo ndiye Mohamed Said anayepiga lecture ughaibuni kuhusu harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na wazee wake walivyosahauliwa na kunyanyaswa baada ya uhuru na Mwalimu Julius Nyerere! Kwa nini, huyu Abdulwahid Sykes anayemuongelea sana na kupiga kelele, watoto wake wako kimya! Je kulikoni?
Mohamed Said ni mjanja sana, katoka mbali toka wakati wa WARSHA na MSAUD akiwa na Pro. Njozi na Dr. Dau. Bahati mbaya nyumba waliyoijenga ya theluji wanashuhudia kwa macho yao ikianza kuporomoka kwani jua linaanza kujitokeza! It is just a matter of time, njama na hila zake zote zitaanikwa.