Uchumi wa Urusi haujatetereka kama mataifa ya Magharibi na baadhi ya wadau walivyotabiri

Freddie uchumi wa US na Ulaya ukianguka hata nyie mtaathirika vibaya sana kwa sababu ni wadau wenu wakubwa zaidi.
Tutajua kwani hatuwezi shift to other blocks kwanza kwa sasa Mchina ndio kashika uchumi wetu kuliko hata hao wazungu
 
Naomba nikuulize mkuu....kwaiyo uchumi wa ulaya na marekani umeyumba iilihali wa Russia unaimarika?
Nakujibu kama unavyotaka.
Uchumi wa Urusi umeyumba sana,Tena sana,Tena toka alipoichukua Crimea kibabe.
Lakini haikuwa kutokea uchumi wa ulaya na USA kuyumba kwa miaka zaidi ya Arobaini,lkn Sasa Leo umeyumba.

Umeyumba sana kiasi ambacho wao waliomwekea vikwazo Urusi hawakutegemea.
Leo ulaya Wana mgao wa umeme,Urusi hakuna,
Ulaya bidhaa zimeadimika madukani Urusi zipo,
Ulaya bidhaa zimepanda Bei Urusi kwaida,ulaya viwanda vimefungwa Urusi havijafungwa.kwa yote hayo namaanisha baadhi.
Waliweka vikwazo ili kumuadhibu itokee kama Zimbabwe, lakini Hali Sasa ni tofauti.
Haya niyasemayo, pia yameshatamkwa na baadhi ya maraisi wa ulaya.,mfanoRais wa Hungary kama sikosei na juzi Macron.
Kwa kawaida anayeweka vikwazo lengo ni kumuumiza anaewekewa,lkn kwa Urusi imekua tofauti.wanaumia wote,West na Urusi.
Kwa muktadha huu anaeumia Sasa hapa, ni yule alieweka maana hakutegemea maumivu kumrudia.
 
Hivi Russia anapochoma gas yake ni kwa kupenda au Hana pa kuuza? Ikifikia hatua ya kichoma gas hua soko limeyumba na kama limeyumba je nchi haijapoteza mapato? Na kama imepoteza mapato je uchumi utabaki salama? Mtoa mada nisaidie kwa hili

Sijui chochote kuhusu kuchoma gesi.
Lakini majibu yangu Yako hivi,kama anachoma kwa kukosa soko maana yake anapata hasara.
Lkn anakosa soko kwa sababu wamemuwekea vikwazo asiuze kitu kwao wala asinnunue kitu kwao.

Sasa afanyeje? Ndio hivyo Tena kama Haina soko basi (anachoma).
Kwa kifupi Urusi havipendi vikwazo hivi na amewaomba mara kadhaa maraisi wa west wamuondolee vikwazo kwa sababu vinamuumiza.
Lkn vita ni vita Mura.
Kwa kua na yeye ameshajua kuwa nao wanaihitaji saaaana gesi yake naye Sasa anaitumia kama silaha ya kuwaumiza wao.
Waliamua kumwaga ugali yeye kamwaga mboga.vita maana yake piga nikupinge..

Uchumi wa Urusi hauwezi kuwa kama ambavyo ungekua kabla ya kuwekewa vikwazo aliwapenda sana ulaya alijenga Hadi Nordsteam2 kwa ajilia ya kufanya biashara na Ulaya,so hawezi kua mjinga Tena kuacha kuwauzia bila sababu za msingi.

Lkn Sasa afanyeje?
Mwenyewe umeona Sasa wanateseka wao na kuaanza kutumia Kuni badala ya gesi.najua watatafuta vianzo vingine,na yeye atatafuta masoko mengine.

Ni kweli nchi imepoteza mapato na haiwezi kua nauchumi sawa,lkn Sasa ifanyeje?

Mtu anaechochea mgogoro huu ni USA Nia ni
I)kuizunguka Urusi kijeshi,
Ii)kuidhoofisha kiuchumi,
III)kutaka itengwe kimataifa.

Lakini matokeo yamekua kinyume sana.
Ukweli Urusi ilizibembeleza sana nchi za west kuhusu Ukraine isijiunge na NATO na iache mienendo yake inayotishia amani ya Urusi,lkn wote tulikua tunaona jinsi walivyokua wanaipuuza Urusi.

USA pia alikua na wivu juu ya biashara kati ya Ulaya na Urusi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…