Soko la ndani ni dogo sababu ya uwezo mdogo wa wananchi kununua bidhaa. Uwezo mdogo wa wananchi kujiwekea akiba inapelekea uwekezaji mdogo na viwanda kutokukua n.k.
Ugumu wa upatikanaji mitaji na riba kubwa huwezi kuzaa viwanda. Serikali inahadaa wananchi waliokosa matumaini wanaona kama kuna mwanga kumbe ni giza.
Nashauri SACCOS na VICOBA na vyama vya wananchi wa chini kila kata viwezeshwe kuchanga mitaji pamoja kufungua viwanda kwa pamoja au kuingia ubia na wawekezaji binafsi wa ndani au nje ya nchi na hata serikali za nje au hii yetu.