Uchunguzi wa mlipuko wa bomu arusha umefikia wapi?

Uchunguzi wa mlipuko wa bomu arusha umefikia wapi?

kizazi kipya

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2010
Posts
327
Reaction score
62
Mara tu baada ya mlipuko wa bomu katika mkutano wa chadema arusha zilitoka kauli nyingi kutoka kwa wahusika.Sijui kama zilikuwa kweli au ulikuwa unafiki.Iliundwa tume ya kipolisi ikiongozwa na chagonja ambaye alianza na mikwara mingi sana arusha.Tabu ilianza baada ya mbowe kutangaza kwamba polisi inahusika.Nadhani kazi yote ya upelelezi iliishia hapo na kilichofuata ni kumwandama mbowe alete ushahidi.Chagonja aliibuka na mikwara mingi sana.
Baadae kidogo tukaambiwa FBI wapo arusha suala lililokanushwa na ubalozi wa marekani.Swali :kwa nini tulidanganywa kwamba FBI wapo arusha?kulikuwa na lengo gani?Baadae mkuu wa mkoa wa arusha aligeuka msemaji wa polisi kwa kutangaza kwamba uchunguzi unaonesha mipango ya ulipuaji bomu ilipangwa arusha.Na kwamba wachina wanachunguza bomu hilo kujua liliingiaje nchini.
Cha kushangaza toka hapo kumekuwa kimya.Polisi wanamfwatilia mbowe awape ushahidi wa wao kuhusika.Lakini hawatuambii uchunguzi wao umefikia wapi?na kama sio wao nani anahusika?Je ni kweli intelijensia ya polisi imeshindwa kubaini waliolipua bomu?
Mbona wauaji wa kamada barlow walipatikana.Kwa nini anaandamwa mbowe na hatupati maendeleo ya tume ya mgonja?Kwa nini hawataki kuunda tume ya kijaji kwa suala nyeti kama hili?kwa nini mwigulu haambiwi kupeleka ushahidi wa kuwa chadema ilihusika?Na je ni lini tutapata majibu ya tume ya chagonja?
Tutafakari....
 
Kudhani polis haihusiki ni upuuuzi, hapa swala ni namana gani polisi watajisafisha, na kama polisi wenyewe ni dhahifu kiasi hiki kushindwa kumkamata mtu aliye lipua bomu mbele yao...JK anajigambaje nchi iko salama? wamarekani wana jua hawa mabwana walivyo wazembe ndiyo maana akitia timu, wna watimulia mbali kabisa, wamebaki kuvimbisha matumbo cha maana wanachofanya hakuna
 
Kudhani polis haihusiki ni upuuuzi, hapa swala ni namana gani polisi watajisafisha, na kama polisi wenyewe ni dhahifu kiasi hiki kushindwa kumkamata mtu aliye lipua bomu mbele yao...JK anajigambaje nchi iko salama? wamarekani wana jua hawa mabwana walivyo wazembe ndiyo maana akitia timu, wna watimulia mbali kabisa, wamebaki kuvimbisha matumbo cha maana wanachofanya hakuna
UMENENA VYEMA... VIONGOZI WA MAREKANI WAKIFIKA BONGO SI POLISICCM WALA JWTZCCM HUKAA PEMBENI. WALISHAJUA UDHAIFU WAO. KAZI KUTUNGA NGONJERA ZA KAULI MBIU MFU...Ohh...UTII SHERIA BILA 'SHUGHULI'. UTATII VIPI SHERIA BILA SHERIA KUZINGATIWA NA KILA MMOJA? POLICCM WENYEWE HAWATII SHERIA KAZI KUVIMBA MATUMBO KWA KODI YANGU.
 
Uko kwenye dawati la Mkuu wa Mkoa na FBI wa kuchonga.

Watawala Wanacheza na damu za watu. It won't let them free. Always hunted by guilty concsiounsness kwa muda mfupi waliobakiza kuwa madarakani kisheria (si kihalali), kabla kila mtu hajabebeshwa mzigo wake, kwa matendo yake na kauli zake.

Watoto wadogo wale, wakitoka madarasa, wameuwawa kikatili, wengine wanaugulia majeraha na vilema vya maisha, huku wengine wakiathirika kisaikolojia na kuhitaji msaada mkubwa...kilio chao hakiwezi kwenda bure.

Damu ya kamanda Judith William itaendelea kudai haki na utu wa mwanadamu. Watawala wana kihoro. Zaidi ya mwezi mzima sasa hakuna taarifa yoyote, no even a preliminary report, why?!

Machozi, jasho na damu...hazitawaachia, hata kama wataficha ukweli kwa muda wa kibinadamu.

Serikali inayoshindwa kuwajibika kwa uhai na maisha ya raia wake...ina uhalali gani machoni pa waliopatia dhamana hiyo?
 
Hivi sheria bila shuruti maana yake nini? tatizo polisi wameisha zoea au wamefundishwa kupelekeshwa bila kuhoji ata kama ni kitu cha kijinga sasa upuuzi wao wa sheria bila shuruti wana taka watuletee na sisi, hili nalo inabidi liangaliwe kwa upana, kwanza ni nani kapima hii ni sheri a na huu ni uonezi? au sheria iko kwenye mikono ya polisi kwamba wanacho amua wao kwa matakwa yao ndiyo sheria?
 
Tetesi zilizopo ni kuwa yule askari anayedaiwa kuhusika na tukio hilo ameuawa kupoteza ushahidi. Inadaiwa askari huyo ni wa mkoani Morogoro na ameuwawa kwa kupewa sumu. NAJARIBU KUFUATILIA UKWELI WA TAARIFA HII.
 
Back
Top Bottom