Udaku Special 2nd Edition!! Limesheheni....

kiwatengu

Platinum Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
18,585
Reaction score
16,780
Hili hapa linakuja...

1. Nawapongeza wale wote waliozaliwa mwezi huu wa 6.. Ntuzu wa tarehe ya leo, Passion Lady, kabanga, muuza ubuyu na wengine wote nawatakia maisha mema, marefu yenye mafanikio na furaha tele..

2. Yule dada maarufu kwa jina vaisley kaamua kum'bwaga rasmi kijana wa vipimio 7 5 mm, aonekana jukwaani akileta mirejesho ya kimchecheto, inasemakana hajawahi kukubaliwa.. siri yawekwa bayana.

3. Ndoa mpya ya Matola mashakani tena, bado haijafahamika vyema! Inasemekana kuna mrembo anayechepukiwa... Dada mwenye ndoa ang'ang'ana.
Baadhi ya kauli kama "kunguru hafugiki" za mletea shida.
Adai ye ni njiwa...kutulia anaweza.

4. Eiyer Paroko wa jimbo kuu, aachana na uparoko ni baada ya kuyumbishwa na kukubali kuonja penzi la mrembo 'Valentina' mwenyewe kanena u padre siyo deal,
Apanga njama za kumtorosha kwa mumewe rasmi.
janeth1 ahusishwa..

5. Khantwe aamua kuwatumia binti zake ipasavyo.
Wakwe walazimishwa kumnunulia gari ya kutembelea. First Born apanga kumkimbia mwanae, aonekana Newala akisaka nyumba ya kupanga.

6. Mr Rocky azua varangati ni baada ya kuexpose nia yake ya kumtaka miss chagga, afanikiwa na sasa yuko kwenye maandalizi ya kumpa mkewe. Dena Amsi talaka...

7. The Boss ahaha kutafuta mke chit chat, mpaka sasa haijajulikana ni wangapi wamekuwa short listed..kuitwa kwenye usahili..
jina na ushiriki wake MMU wawachanganya wengi...

8. Baba V aonekana Gamboshi akisaka ndumba..
yasemekana mapinduzi aliyotishiwa na vijana wa Arusha. Arushaone na Erickb52 yanampa shida!!
aapa kuwateketeza kwa gharama yoyote...

9. Utata waibuka juu ya ID ya Mom Fay na Arovera modes wapata shida kutrace IP Adress..
kuna uwezekano wa matumizi ya devices zinazotofautiana kwa kila ID...
snowhite na Dinazarde washtukia deal mapema.
Hali hii ya wakera wengi....

10. Mwali aibuka na kuomba mtongozo, vijana wajazana kwenye PM box yake..
atakayefanikiwa kuyafaidi maisha hukoToronto Canada, kipindi cha mwezi mtukufu..

11. Kasinde aonekana Dubai akizurura ovyo, inasemekana alikuwa na lengo la kwenda kwa Obama (USA).
mpaka sasa haijafahamika aliyempa huo msaada na kumtosea Dubai.


Cc: mwallu, Mentor, Kaizer, Karucee, Tized, utafiti sungura1980 n' et all..
Pata nakala yako..
 
Last edited by a moderator:
Nimecheka hapo kwa Kasinde kwa hiyo nae muda si mrefu ataomba tumchangie nauli najitoa kabisaa hata Bakhresa hachangii pesa ovyo ovyo seuse mim hata ubilionea sina wala hauniwaziiu akuuuu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kiwatengu Asante kwa pongezi zako!

Kweli nikuwahi nakala yako kabla hazijaisha

Baba V hiyo tena kiboko! Sasa Huko mitaa ya kwetu Ndio alikwenda kutafuta ndumba ??

Teh Teh Teh ile Kamera yako ya UDUKUZI haikubahatika kupata picha yake Mkuu?
 
Last edited by a moderator:
Kazi iko hapo kwa aliyemwangusha paroko,, inasemekana mapenz yao yalikolea hadharan huko JF group hapo mtumishi wa Mungu paroko akashindwa kuhimili mihemko ya mwili na kujikuta akisaliti utumishi na kuangukia kwenye penzi la mwanadada Valentina
 
Kazi iko hapo kwa aliyemwangusha paroko,, inasemekana mapenz yao yalikolea hadharan huko JF group hapo mtumishi wa Mungu paroko akashindwa kuhimili mihemko ya mwili na kujikuta akisaliti utumishi na kuangukia kwenye penzi la mwanadada Valentina

ha ha ha asante kwa kuishibisha habari..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…