Udhamini mpaka uwe mfanyakazi wa serikali ?

Udhamini mpaka uwe mfanyakazi wa serikali ?

Likasu

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2011
Posts
855
Reaction score
438
Nianze kusema kuwa mimi sina utaalam wa mambo ya sheria. Siku hizi kumezuka mtindo wa mahakama zetu kumdhamini mtuhumiwa mahakani eti ni mpaka aje mdhamini ambaye ni mfanyakazi wa serikali. Huwa najiuliza maswali kadhaa. Hivi raia hawezi tambulika mahakamani mpaka awe serikalini ? Wafanyakazi wa serikali wapo wangapi kutosha kudhamini watuhumiwa mahakani ? Serikali zetu za mitaa ambazo hutoa uthibitisho wa mkazi wake mahakamani haziaminiki tena na mahakama zetu ? Naomba wataalam wa sheria mtujuze kuhusu haki ya kumdhamini mtuhumiwa mahakani.
 
hiyo inatokana na uzoefu, wameshawapokea wadhamini wengi ambao si wafanyakazi, address yao haijulikani vizuri, washitakiwa wengi wakawa wanalala mbele, ikabidi mahakama waangalie njia nyingine. chukulia mfano, mtu ameiba gari yako wewe hiyo unayoendesha kama unayo, anakuja mahakamani, kosa hili ni bailable, anapata dhamana kwa mtu asiye na address ya kueleweka, analala mbele na kesi inaharibikia hapohapo kwasababu unaweza kukesha miaka kadhaa bila kumkamata, utajisikiaje? mahakama nafikiri wamefanya hivyo ili kulinda maslahi pia ya victim aliyetendewa kosa, usiangalie tu upande wa mshitakiwa, angalia na kwa muathirika aliyedhurika na kosa lililotendeka.
 
Hii ni kwa sababu mtu akidhaminiwa na mfanyakazi wa serikali security inakuwa kubwa sana. Watu siku hizi wanahama hama sana so hata akipata udhamini wa serikali za mtaa security inakuwa ndogo. Pia kumbuka endapo kutatokea default yoyote anayepata hasara ni yule ambaye anadai haki yake, ndiyo maana mahakama inaangalia wapi kuna security kubwa. Pia kwenye kuna matukio mengi sana ambayo yametokea kwa mtu kukimbia pamoja na mdhamini kutoonekana na huku kuna waacha wengi wasiwe na la kufanya.
 
Back
Top Bottom