Udhibiti wa Rushwa Mahakamani, Mahakama za Mwanzo na Mkazi zisimamiwa na Halmashauri

Udhibiti wa Rushwa Mahakamani, Mahakama za Mwanzo na Mkazi zisimamiwa na Halmashauri

kanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2011
Posts
1,025
Reaction score
494
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande, amesema kuwa mahakama imeelemewa na mzigo wa kesi kutokana na uhaba wa majaji na mahakimu.

Amesema kuwa mahakama inakabiliwa na changamoto ya watumishi hali inayosababisha kasi ya kumaliza kesi kuwa ndogo.

Jaji Chande alisema idadi ya majaji waliopo bado ni ndogo na haikidhi mahitaji ya mashauri yaliyopo mahakamani.

Akizungumza jana katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini, jijini Dar es Salaam, Jaji Mkuu alisema kwamba katika majaji 65 wa Mahakama Kuu, kila mmoja anahudumia Watanzania 560,000, hali ambayo alisema kuwa inaonyesha bado
mahakama inaelemewa na kasi ya kumaliza kesi.

Hata hivyo, Jaji Chande alisema kutokana na mikoa 12 kutokuwa na Mahakama Kuu na ongezeko la watu kuwa kubwa katika mkoa wa Dar es Salaam, mahakama inakusudia kuigawa Kanda ya Dar es Salaam katika kanda tatu za Ilala, Temeke na Kinondoni.Source

source: Nipashe/7/2013

My Take.
Mahakama nchini bado zina utendaji wa kazi wa kijima sana na urasmi uliotawaliwa na rushwa.Pia jambo lingine ni kule kutegemea kufanya kazi kwa kutegemea posho za vikao au sitting allowance kwa majaji.Hivi kwa nini Majaji waendelee kufanya kazi kwa kutegemea posho wakati wanafanya kazi zao za kawaida zenye marupurupu mazuri na mafao bora zaidi?.

Pia muundo mbovu wa mahakama unahitaji ubadilishwe ili kupunguza urasmi na rushwa ilikomaa ndani ya taasisi hii muhimu.

Mahakama za mwanzo na mkazi/Wilaya zisimamiwe na Serikali za mitaa na kuwajibika kwa Halmshauri moja kwa moja na Mahakama kuu,rufaa zibaki kwenye serikali kuu kama vyombo vya rufaa na makosa maalum.

Hii itapunguza urasmi na rushwa.Katika tafiti za sasa mahakama na polisi ndizo zinashindania namba ya kul rushwa wakati serikali za mitaa na Halmashauri rushwa ni kidogo sana.

Jaji mkuu kulalama kote huko hata akipewa majaji na mahakimu wa kumwaga tatizo halitakwisha maana ni nature ya utendai kazi wa taasisi katika kutafuta kuneemeka na rushwa, Dawa ni kuunda upya mfumo mahakama za chini ziwajibike na zisimamiwe na Halmashauri moja kwa moja.
 
Hakutakuwa na Uhuru wa Mahakama na pia Mahakama ni mhimili mwingine unaojitegemea hauwezi kuwa chini ya Serikali na majukumu ya Halmashauri na Mahakama ni tofauti kabisa.
 
Hakutakuwa na Uhuru wa Mahakama na pia Mahakama ni mhimili mwingine unaojitegemea hauwezi kuwa chini ya Serikali na majukumu ya Halmashauri na Mahakama ni tofauti kabisa.

Sawa kabisa, Mabaraza ya kata yaimarishwe na mahakama za miji, majiji (kama ilivyo DSM) zianzishwe kupunguza kesi za makosa madogomadogo ya kuvunja sheria ndogo za maeneo husika
 
nikukosoe tena sana
mahakama ni mhimili huru hauwezi kusimamiwa na halmashauri hapo umekosea sana
Pili majaji hawategemei sitting allowance wana mishahara yao
wanapoenda kwenye mikoa mingine kusikiliza kesi lazima walipwe kama kawaida ya mtumishi wa serikali awapo nje ya kituo chake cha kazi
tatu halmahsuri ndizo zinaongoza kwa rushwa na watataka mahakama zifanye kazi kwa maslhi yao haki haitakuwepo
cha muhimu mahakama ipewe fungu sawa na bunge au executives ili waweze kuwalipa vema mahakimu, majaji wao wanalipwa vizuri haina shida.
hakuna mbadala wa hiyo ndugu lazima mahakama iwe huru na hata kamati ya maadili ya mahakimu bado ipo chini ya mkuu wa wilaya which is very wrong. mwanasiasa atamsimamiaje hakimu? jajio mkuu anapigania hili ili mahakimu wawe na kamati yao wenyewe ya maadili isiohusisha hawa jamaa wa CCM i mean wakuu wa wilaya.
nawasilisha
 
Mahakama iwe chini ya Halmashauri!you cant be serious,tatizo la watz wengi ni kujifanya wajuaji,we KANGA nenda kafanye utafiti ukishajua mhimili wa mahakama unafanyeje kazi ndiyo urudi tena........siyo lazima kucoment JF kama hujui kiundani unachozungumzia,Mahakama cyo askari wa jiji so refer somo lako la Civics kama ulipita pande hizo
 
Hapo katika kuanzisha kanda mpya katika wilaya za Ilala, Temeke na Kinondoni naomba nitofautiane na Jaji Mkuu. Ukiangalia High Court main registry inamajaji wengi kuliko kanda zote na kiukweli kuna mikoa ambayo ina kesi nyingi tu na inapaswa kupewa kipaumbele maana raia wanateseka sana kusubiria session za majaji mfano ni Morogoro, Mara, Shinyanga na Kigoma.

Pia kuna division kama ya Ardhi ambayo ina kesi nyingi mno na bado haijafanikiwa kusambaa nje ya mkoa wa Dar es salaam pamoja na ile ya biashara. Kutanua division hizi kwa maoni yangu yapaswa kuwa ni kipaumbele chenye uharaka zaidi.
 
Back
Top Bottom