Udsm inaelekea wapi? Barua hiyo soma mwenyewe na utoe maoni yako

Huu ni upuuzi,utawala hawataki kuwa questioned kwanini?
Kikwete tu kama raisi wa nchi kila siku anakuwa questioned iweje hawa
maprofesa wa kulalili madesa?
wizi mtupu,huu ni udikteta ulio pitiliza.

13 Expelled, kwamba hawatasoma tena udsm,...
86 Suspended, kwamba watarudi kusoma udsm,ila wamepoteza mwaka mmoja wa masomo.
Damn how fair is this?
Kwamba kudai walio fukuzwa walionewa ni kosa la kufukuzwa chuo mazima?
Kwanini waligoma in the first place?
Mmeondoa mazingira ya wanachuo kugoma?
Wapuuzi kweli,mbona mlipo cheleweshewa mishahara yenu 2010 mlijitia kugoma na nyie
nani aliwafukuza kazi?
 
Sikutegemea kama management ya chuo nao wangetumia nguvu badala ya hoja! This is a rotten systems. Naona sasa watawala wameamua kutumia mabavu na siku zote ukitumia mabavu kutatua migogoro siku zote utakuwa kwenye migogoro. Serikali ikae chini ijitafakari kwa nini inasuguana na wasomi? Ni juzi Muhimbili wamefukuzwa, leo mlimani. Siku zote na mara nyingi wanafunzi wa vyuo vikuu ni torch inayoimulika serikali na ukiona kila mara nguvu kubwa na adhabu zisizostahili zinatolewa dhidi ya wanafunzi basi serikali husika ina matatizo makubwa. Mimi kama raia nasema huu ni uonevu mkubwa ambao hauvumiliki, hatuwezi kufungwa midomo kwa jinsi hii.
 
Ngoja nisome vizuri attachment ntarejea tena.
 
Something deeply wrong kwa UD ya sasa miongoni mwa utawala na wanafunzi.

Kwa upande wa utawala, Jjnsi wanavyo handle matatizo ya wanafunzi lengo lao kuu ni kufurahisha mabosi wao wa Ikulu kulipa fadhila, yaani wako biased kiasi kwamba siku zote mwanafunzi ndiye anaonekana ana makosa yasiyosameheka -- hata kama wanafunzi wana haki kabisa katika madai yao.

Kwa upande wa wanafunzi, DARUSO ya sasa hawana umoja, wamekaa kinafikinafiki kama wanasiasa wa CCM. Juzi nimepita pale kwa misele yangu nikakuta wanafunzi wakinongona kwenye vimbwete vyao kwamba wamesalitiwa vibaya na wabunge wa DARUSO kiasi kwamba sasa hivi wamechoshwa na siasa uchwara za kuuma na kupuliza za DARUSO (wakienda kwa watawala wanawachongea baadhi ya wanafunzi, wakirudi kwa wanafunzi wanahamasisha maandamano). Matokeo yake vuguvugu la mgomo wa sasa hivi limewagawa vibaya sana wanafunzi kiasi kwamba baadhi ya wanafunzi hawataki kabisa kusikia neno mgomo na baadhi yao wako pale ReV Square kusikiliza sermons za wakereketwa.

Hii press release ya watawala ni matokeo ya ukandamizaji wa watawala wasio na huruma pamoja na DARUSO isiyo imara ya siku hizi.
 
Tanzania ya leo tuna tatizo moja KUBWA, nalo ni hili. Linapotokea tatizo au uvunjwaji wa sheria au suala lolote linaloonekana kuwa ni tatizo,basi solution au majibu au namna jinsi uamuzi unaotolewa ktk tatizo hilo huwa unakuwa ni TATIZO KUBWA kuliko hata tatizo lenyewe linalotatuliwa. Sasa mimi najiuliza, hawa wanaotoa maamuzi siku hizi, wanatumia nini kufikiri Kweli?? Tanzania tumekumbwa na nini?? Kuna mdudu gani kawaingia hawa wanaotoa maamuzi? au ndio matokeo ya ile Habari inayoendelea ambayo sasa iko PART 2? Hembu nijuzeni wanajamvi. Kwa sababu nacho kiona kinafuata ni hili: BORA wote tukose. Tusishangae tukaona hii mandhari nzuri ya maendeleo inayojichomoza sasa, ghafla ikawa ni magofu, ghafla tukasikia watua wanaanza kupotea, ghafla tukasikia mahali fulani siku hizi hakupitiki, ghafla tukasikia familia fulani fulani zimeshambuliwa. Hii yote ni kutokana na kushindwa KUFIKIRI kwa walio na nafasi za kutoa Maamuzi. Haya wee, endeleeni kuchochea tu moto na Petrol zenu.
 
Ninaomba niwape moyo wanafunzi wote wa UDSM nikiwa kama mhiyimu wa hapo UD. Wasiwababaishe mafala wanaotumwa na CCM ha kazeni buti, ingieni mitini wakiweza wawafukuze wote chuo wasome wao.
 
kazi mnayo na chuo chenu cha special kama special school lakini siasa zinawapeleka kubaya soon tu mtapotea kwenye ramani..
 
Ingekuwa Mods wanatoa japo dakika tano tu za uhuru wa kutukana bila ban, ningezitumia leo hapa dhidi ya huo uongozi wa chuo.

Wanajengea watu chuki na hasira, na hawakumbuki kuwa hasira hazina uoga
 
They must always know who are they fighting against. If they think they are fighting against Mukandala they are doomed.
 
Jaribuni kuicopy and paste,ili sisi wenye simu za kichina tuweze soma!
 
Mimi nafikiri kwa sasa mgt ya UDSM wanakwenda pabaya,wanalalamikia hao wanafunzi si wapewe? Wasitumie misuli kutatua tatizo la kutumia akili. Mtu anaposema jambo hadharani ni kwamba anatafuta audience.

MGT tumieni akili za kuona mbali msiwe wanasiasa wa kutazama 5years forward.
 
Ndio maana kiwango cha utendaji kimasomo UDSM kimeshuka hata sua kwenye top 50 kimo. UDSM hata top 200 hakipo kutoka kucheza double digit mpaka 3 digits. Nafikiri UDSM mfumo umekuwa wa "Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe" Acheni ujinga somesheni na kusoma wanazuoni, migomo mwisho wake ni mbaya sana kwa kuwa unawagawanya. Solidarity ni muwapo tu chuoni. Ukurudi uswahilini haifanyi kazi. Kazaneni kwenye madesa, acheni utani bana!
 
Kidumu Chama cha Mapinduziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Chuo hiki kimeshapoteza mwelekeo. Nilisikitika nilipomsikia Prof. Mukandara aliposema wanakusudia kutumia mambilioni ya shilingi kuzungushia ukuta chuo kizima...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…