UEFA kuiondoa sheria ya goli la ugenini

UEFA kuiondoa sheria ya goli la ugenini

denooJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
18,509
Reaction score
68,228
Sheria ya goli la ugenini iliyokuwa inaipa nafasi ya kusonga mbele timu iliyofunga magoli mengi ya ugenini kwenye mashindano ya UEFA hivi karibuni itaondolewa.

Sheria hiyo inayotumika kwenye mashindano ya UEFA kama Champions League, Europa League, na Europa Conference League na iliyoanza kutumika tangu mwaka 1965 inatarajiwa kuondolewa kwenye kikao cha UEFA cha hivi karibuni.

Natumai na shirikisho la mpira barani Afrika CAF nalo litaiondoa sheria hiyo inayotumika kwenye mashindano ya vilabu barani Afrika CAF Champions League, na kombe la shirikisho.
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini

Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je, hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
 
Faida ya kucheza mechi mbili ugenini na nyumbani itakua hipi? Ikitokea team moja ikashinda goli 3 ugenini thn nyumbani ikafungwa goli moja au mbili bila nini kitafata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini
Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
Penalti.
 
Na sheria ya aggregate itolewe
Aggregate score wanaangalia timu yenye magoli mengi kwenye mechi mbili za home and away ndio inaendelea na mashindano, lakini hayo magoli sasa itabidi yawe yalifungwa kiuhalisia sio ile style ya kusema goli moja la ugenini ni sawa na mawili, hiyo ndio inaondolewa.
 
Faida ya kucheza mechi mbili ugenini na nyumbani itakua hipi? Ikitokea team moja ikashinda goli 3 ugenini thn nyumbani ikafungwa goli moja au mbili bila nini kitafata

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo timu iliyoshinda 3-0 ugenini itaendelea, wanachoondoa UEFA ni ile ya kusema mfano ufungwe ugenini 2-1, halafu kwako ukashinde 1-0 then uwe umemtoa mwenzako kama ilivyo sasa, sasa kwa hii sheria kuondolewa matokeo yatakuwa ni 2-2, hivyo kitafuata extra time au penalti.
 
Ambaye hajakuelewa achana naye .
Hiyo timu iliyoshinda 3-0 ugenini itaendelea, wanachoondoa UEFA ni ile ya kusema mfano ufungwe ugenini 2-1, halafu kwako ukashinde 1-0 then uwe umemtoa mwenzako kama ilivyo sasa, sasa kwa hii sheria kuondolewa matokeo yatakuwa ni 2-2, hivyo kitafuata extra time au penalti.
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini
Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
Hapo Ni 3-3
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini
Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
Unaelewa maana ya aggregate? Hapo si ni sare gemu inaendelea hadi apatikane mshindi
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini
Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
Ac Milan atatokaa
 
Sasa utamu wachii league utakua uko wapi binafs naona waache Kama ilivo maana ndo inakera hamasa ya game kupigwa
Hamasa gani, hiyo sheria ilikuwa inazibeba timu mbovu, lazima ucheze na ushinde in clear aggregate
 
Itapunguza ladha ya soka, watu wataona Ni rahisi kupindua meza
 
Kwa hiyo ikitokea Ac Milan Kashinda goli tatu kwa moja ugenini
Halafu marudio kafungwa goli mbili kwa bila nyumbani keake. Je hapo atayesonga mbele ni yupi? Au nini kitafuata?
Kama sheria ikifutwa hapo aggregate ni 3-3 hivyo muda wa nyongeza unahusika.
 
Back
Top Bottom