Uelewa unahitajika hapa

Possibles

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2011
Posts
1,933
Reaction score
2,439
Wadau nimekuwa nikilisikia kwa muda mrefu kidogo neno 'fedha haramu' na mara nyingine 'biashara ya fedha haramu'.
Tafadhali mnisaidiwe kuelewa maana ya hayo maneno.
Natanguliza shukrani
 
Mkuu hicho unachouliza kina maana moja na money laundering?
 
Mkuu hicho unachouliza kina maana moja na money laundering?
Exactly, fedha chafu na Money Loundering ni Samaki na maji.

Kwa ufupi fedha haramu ni fedha yoyote ambayo imepatikana kwa njia zisizo halali kama vile Ujambazi, Ufisadi, Madawa ya kulevya, uhujumu uchumi, kukwepa kodi etc!

Mtu anayemiliki fedha za aina hii huwa hawezi kuanza kuzitumia moja kwa moja kwa hofu ya kustukiwa.
Atakachofanya ni kwamba atatafuta namna yoyote ya kuzi'invest katika mradi fulani iili zionekane zimejizalisha na kukuza mtaji.

Kitendo cha kujaribu kuwadanganya watu kuwa ni fedha halali zinazozalishwa kwa huo mradi ndio hUitwa KUTAKATISHA FEDHA, au MoneY Loundering!
Nadhani uko sawa!

 

Asante kwa maelezo yako mazuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…