Tanzania ni moja ya mataifa yanayoingia katika mageuzi ya uendeshaji wa vilabu vya mpira kufuata taratibu za kampuni. Ambapo maamuzi ya mwisho ya club yatafanywa na wenye hisa. Mfumo huu unaonekana kufanikiwa zaidi kwa mataifa ya ulaya, marekani na mabara mengine. Tanzania ndio tunaingia katika mfumo huu. Swali, Je wanamichezo wengi wa vilabu wanaelewa vizuri mfumo huu kwa mazingira ya kitanzania?. Je tunatarajia timu zetu kufanikiwa kwa muda mfupi kupitia mfumo huu? Je migogoro iliyokuwa inaendelea katika vilabu inaenda kwisha kwa mfumo huu. Wadau naomba udadavuaji wenu kidogo hapo?