Ni biashara za network marketing. Mimi sijawahi fanya ila mtu wangu wa karibu anazifanya. Zina faida ila inabidi u link na watu wenye kipato cha kati na cha juu na wenye matatizo ya kiafya. Kwa matabibu wanaweza fanya biashara maana mteja akienda na pressure au tatizo lolote, then anamwambia ajaribu hiyo nayo ni tiba m-badala.
Vinginevyo haina tofauti na forever living products, network yake inavyoundwa. Kadiri unavyoingiza watu wengi kwenye network, na wakawa active nao wakaingiza watu, nao wakawa active ndivyo unavyokuwa. In short uwe na muda wa kutosha, na uwajue potential customers, na ujitahidi kuwaweka watu nao waingize watu, nao waingize watu to infinity!!!