Ufafanuzi kiatu cha dhahabu EPL 2018/19

Ufafanuzi kiatu cha dhahabu EPL 2018/19

marcoveratti

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2017
Posts
1,019
Reaction score
1,824
Kutokana na sheria za EPL kuwa tofauti kidogo na zile za Kombe la Dunia kuwa wafungaji vinara wakiringana magoli basi kiatu huamuliwa Kwa pasi za mwisho "assist" na Kama nazo Zita lingana kitaamuliwa Kwa nafasi zilizo tengenezwa("chance created ")

EPL inapokuwa Hivyo, Kama jinsi ilivyo msimu huu 2018/19 ambapo Kuna vinara watatu wa magoli wenye magoli 22 kila mmoja,
Sheria ya EPL inasema Wote watapewa kiatu tena kila mtu cha Kwake,
Na kila mmoja amepewa kiatu chake.

Hii ilishatokea hapo awali wakati Chris Sutton, Michael Owen na Dion Dublin wakiringana magoli mwaka 1997-98 na tena ikatokea mwaka 1998-99 wakati Jimmy Floyd-Hasselbaink, Michael Owen na Dwight Yorke wakiringana magoli . Pia ilitokea kwa Dimitar Berbatov na Carlos Teves mwaka 2010/11 wakati nyakati zote hizo vinara Hawa wa kuzifumania nyavu walipewa kiatu kila mmoja sawa na ilivyo mwaka huu 2018/19 Kwa Aubameyang,mane na Mohamed salah.

Chanzo Soka_app instagram
IMG_20190513_031302_525.jpeg
 
Utaratibu wa fifa wanaangalia idadi ya dakika mlizocheza kama mmelingana sio Assist kama mtoa mada ulivyosema
 
Hii ilishatokea hapo awali wakati Chris Sutton, Michael Owen na Dion Dublin wakiringana magoli mwaka 1997-98 na tena ikatokea mwaka 1998-99 wakati Jimmy Floyd-Hasselbaink, Michael Owen na Dwight Yorke wakiringana magoli .


Naam mkuu.. Hizi zilikua nyakati bora kabisa za EPL
 
Hii ilishatokea hapo awali wakati Chris Sutton, Michael Owen na Dion Dublin wakiringana magoli mwaka 1997-98 na tena ikatokea mwaka 1998-99 wakati Jimmy Floyd-Hasselbaink, Michael Owen na Dwight Yorke wakiringana magoli .


Naam mkuu.. Hizi zilikua nyakati bora kabisa za EPL
Hakika hzo zilikua nyakati bora Sana EPL ilikua bora na yenye mvuto wa kipekee Sana lakini Pia timu kongwe Ndio zilikua ziki Shika hatamau Kama vile United Liverpool na arsenal
 
Back
Top Bottom