UFAFANUZI: Kwanini Habib Kyombo amevaa jezi ya DTB FC badala ya Singida Big Stars?

UFAFANUZI: Kwanini Habib Kyombo amevaa jezi ya DTB FC badala ya Singida Big Stars?

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
IMG-20220621-WA0005.jpg

Watu wa Soka,

Juzi Jumanne 21/06/2022 saa 7:00 mchana tulimtambulisha rasmi mchezaji wetu mpya Habib Haji Kyombo ambaye tumemsajili kuja kuongeza nguvu kwenye safu yetu ya ushambuliaji.

Kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii (@singidabsfc) tulichapisha baadhi ya picha zake akiwa anasaini mkataba wa kuitumikia timu yetu kwa muda wa miaka miwili kuanzia msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2022/2023.

Hata hivyo, sintofahamu ikaibuka kwanini ameonekana na jezi za DTB FC badala ya Singida Big Stars?

Nimeona kipekee kabisa (exclusively) nifafanue mkanganyiko huo kupitia Jukwaa hili la JamiiForums kama ifuatavyo:

1. DTB FC ndiyo Singida Big Stars FC ya sasa. Taratibu zote za kisheria za kubadili jina zimeshakamilika na jina jipya linatumika kwenye mikataba na makubaliano yote ya kisheria ndani ya timu.

2. Habib Haji Kyombo tulimsaini mapema kabla hatujazalisha chapa/logo mpya ya Singida Big Stars pamoja na vifaa vingine kama jezi na kadhalika, hivyo kulazimika kumsaini akiwa na jezi yetu ya awali ya DTB FC.

3. Mkataba aliousaini Habib Haji Kyombo tayari ulikuwa na mabadiliko ya jina la timu, hivyo amesaini kama mchezaji wa Singida Big Stars FC na sio DTB FC.

4. Bado tunaruhusiwa kutumia chapa ya DTB katika kipindi hiki cha mpito (transition) kuelekea kubadilisha kila kitu kiwe Singida Big Stars FC.

5. Upo uwezekano jezi zitakapokamilika hivi karibuni, ataonekana kwenye picha nyingine akiwa na uzi mkali wa Singida Big Stars FC.

Asanteni sana.

IMG_20220621_132252_962.jpg
 

Attachments

  • 1655996337407.png
    1655996337407.png
    293.4 KB · Views: 15
Atacheza Simba SC bila hata ninyi kupewa 35M mnayodai. By the way, mnatakiwa mumdai mchezaji badaa ya Simba, tena kama mlimlipa kupitia mifumo rasmi (bank, receipts, etc) na tena kama mlilipia kodi hayo mapato. Vinginevyo mtakosa nguvu ya kumdai
 
Atacheza Simba SC bila hata ninyi kupewa 35M mnayodai. By the way, mnatakiwa mumdai mchezaji badaa ya Simba, tena kama mlimlipa kupitia mifumo rasmi (bank, receipts, etc) na tena kama mlilipia kodi hayo mapato. Vinginevyo mtakosa nguvu ya kumdai

Hayo ya kumdai 35m na masuala ya Simba umeyatoa wapi mbona hayapo kwenye bandiko langu mkuu?
 
Hayo ya kumdai 35m na masuala ya Simba umeyatoa wapi mbona hayapo kwenye bandiko langu mkuu?

Basi kama hauitambui hiyo 35M, wewe hauna uhusika wowote katika klabu ya Singida United, na haukutakiwa kuileta taarifa humu

Kiongozi wa juu na mwenye maamuzi ndani ya Singida amesema hatukuwa na nia ya kumtambulisha Kyombo leo wala mchezaji yoyote yule hadi hapo msimu utakapo malizika.

“Tumeamua kumtambulisha Kyombo kutokana na kupata taarifa za uhakika kuwa Simba imemsainisha mchezaji huyo mkataba wa miaka miwili ili hali huku nyuma akiwa amechukua cha kwetu tayari,” amesema Kiongozi huyo na kuongeza;

“Kama Simba itakuwa tayari kutupatia kiasi cha Sh35 milioni ambacho tulimpatia Kyombo tunaweza kukaa nao meza moja kwa ustaarabu na tukawaachia mchezaji aende kucheza kwao,”
 
Basi kama hauitambui hiyo 35M, wewe hauna uhusika wowote katika klabu ya Singida United, na haukutakiwa kuileta taarifa humu

Kiongozi wa juu na mwenye maamuzi ndani ya Singida amesema hatukuwa na nia ya kumtambulisha Kyombo leo wala mchezaji yoyote yule hadi hapo msimu utakapo malizika.

“Tumeamua kumtambulisha Kyombo kutokana na kupata taarifa za uhakika kuwa Simba imemsainisha mchezaji huyo mkataba wa miaka miwili ili hali huku nyuma akiwa amechukua cha kwetu tayari,” amesema Kiongozi huyo na kuongeza;

“Kama Simba itakuwa tayari kutupatia kiasi cha Sh35 milioni ambacho tulimpatia Kyombo tunaweza kukaa nao meza moja kwa ustaarabu na tukawaachia mchezaji aende kucheza kwao,”

Ni kweli mimi sihusiki na Singida United. Nahusika na Singida Big Stars.

Pili hiyo taarifa sio ya kweli. Tuliiona ikichapishwa kwenye gazeti fulani pia lakini tukaipuuza.

Umeona wakimtaja aliyezungumza hayo zaidi ya kuandika tu chanzo ni "kiongozi wa juu na mwenye maamuzi ndani ya Singida" 😄😄

Puuzeni porojo na Propaganda.
 
mbunge wenu hana ubavu wa kushindana na makolo, haya makolo ndiyo yanayo shikilia soka la nchi hii, rejea sakata la yule dogo aliye kuwa mchezaji wa kagera sugar!

Hueleweki mkuu. Mbunge gani? Sakata la mchezaji gani na tunahusiana nae vipi?
 
Hueleweki mkuu. Mbunge gani? Sakata la mchezaji gani na tunahusiana nae vipi?
Shida ni kwamba unadhani huku ni facebook kwamba utakuja na taarifa kisha watu wameze tu, huku kuna watu wanaojua mengi sana kuliko hata wewe ( hii anonymity ya watu isikuchanganye).

Data zipo wazi kabla hata haujazileta, MWIGULU NCHEMBA ndiye mmiliki wa SINGIDA BIG STARS.

NB; Kuhusu hili hatuhitaji uthibitisho kutoka kwako, USIKU MWEMA.
 
Shida ni kwamba unadhani huku ni facebook kwamba utakuja na taarifa kisha watu wameze tu, huku kuna watu wanaojua mengi sana kuliko hata wewe ( hii anonymity ya watu isikuchanganye).

Data zipo wazi kabla hata haujazileta, MWIGULU NCHEMBA ndiye mmiliki wa SINGIDA BIG STARS.

NB; Kuhusu hili hatuhitaji uthibitisho kutoka kwako, USIKU MWEMA.

Huu ni uzushi. Upuuzwe.
 
Wewee utakuwa dogo sanaa kwenye ulimwengu wa kabumbu la kibongo bongo! Nadhan ukikuwa utakujaga kunielewa tuu, kwanza hata hicho ki tim chenu na chenyewe bado bado kidogo

Asante sana mdau. Endelea kuwa nasi. Tukutane Ligi Kuu.
 
Back
Top Bottom