DOMINGO THOMAS
JF-Expert Member
- Feb 16, 2023
- 365
- 365
Kabla ya kuanza kutumika kikokotoo cha asilimia 33% kwenye kiinua mgongo na asilimia 67% kwenye pensheni ya kila mwezi, kulikuwa na mifuko mitano (5) ambayo kila mmoja ulikuwa na formula yake kwenye ukokotoaji wa mafao ya uzee:
1. LAPF na PSPF: Asilimia 50% kwenye kiinua mgongo na asilimia 50% kwenye malipo ya kila mwezi (Monthly Pension).
2. PPF, NSSF na GEPF: Asilimia 25% kwenye kiinua mgongo na asilimia 75% kwenye malipo ya kila mwezi.
Kwa mujibu wa kauli ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba tarehe 13 Juni 2024:
1. Wanachama wa LAPF na PSPF: Watalipwa asilimia 40% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 60% (badala ya asilimia 67%).
2. Wanachama wa GEPF, NSSF na PPF: Watalipwa asilimia 35% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 65% (badala ya asilimia 67%).
3. Wanachama wa PPF, GEPF, PSPF na LAPF (PSSSF) kabla mifuko kuungana na baada ya kuungana waka-hamia NSSF, na walio kuwa NSSF kabla ya kuungana na waka-hamia PSSSF: Hawa wanatumia Totalization formula.
NOTED: Kauli hii bado haijaanza kufanya kazi mpaka pale miongozo na taratibu zitakapotolewa.
Imeandikwa na Thomas Ndipo Mwakibuja, Mtaalam wa hifadhi ya Jamii (Social Protection Expert).
1. LAPF na PSPF: Asilimia 50% kwenye kiinua mgongo na asilimia 50% kwenye malipo ya kila mwezi (Monthly Pension).
2. PPF, NSSF na GEPF: Asilimia 25% kwenye kiinua mgongo na asilimia 75% kwenye malipo ya kila mwezi.
Kwa mujibu wa kauli ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba tarehe 13 Juni 2024:
1. Wanachama wa LAPF na PSPF: Watalipwa asilimia 40% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 60% (badala ya asilimia 67%).
2. Wanachama wa GEPF, NSSF na PPF: Watalipwa asilimia 35% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 65% (badala ya asilimia 67%).
3. Wanachama wa PPF, GEPF, PSPF na LAPF (PSSSF) kabla mifuko kuungana na baada ya kuungana waka-hamia NSSF, na walio kuwa NSSF kabla ya kuungana na waka-hamia PSSSF: Hawa wanatumia Totalization formula.
NOTED: Kauli hii bado haijaanza kufanya kazi mpaka pale miongozo na taratibu zitakapotolewa.
Imeandikwa na Thomas Ndipo Mwakibuja, Mtaalam wa hifadhi ya Jamii (Social Protection Expert).