Ufafanuzi mdogo kuhusu kauli ya mabadiliko ya kikokotoo

DOMINGO THOMAS

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2023
Posts
365
Reaction score
365
Kabla ya kuanza kutumika kikokotoo cha asilimia 33% kwenye kiinua mgongo na asilimia 67% kwenye pensheni ya kila mwezi, kulikuwa na mifuko mitano (5) ambayo kila mmoja ulikuwa na formula yake kwenye ukokotoaji wa mafao ya uzee:

1. LAPF na PSPF: Asilimia 50% kwenye kiinua mgongo na asilimia 50% kwenye malipo ya kila mwezi (Monthly Pension).

2. PPF, NSSF na GEPF: Asilimia 25% kwenye kiinua mgongo na asilimia 75% kwenye malipo ya kila mwezi.

Kwa mujibu wa kauli ya Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba tarehe 13 Juni 2024:

1. Wanachama wa LAPF na PSPF: Watalipwa asilimia 40% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 60% (badala ya asilimia 67%).

2. Wanachama wa GEPF, NSSF na PPF: Watalipwa asilimia 35% kama kiinua mgongo (badala ya asilimia 33%), na malipo ya kila mwezi yatakuwa asilimia 65% (badala ya asilimia 67%).

3. Wanachama wa PPF, GEPF, PSPF na LAPF (PSSSF) kabla mifuko kuungana na baada ya kuungana waka-hamia NSSF, na walio kuwa NSSF kabla ya kuungana na waka-hamia PSSSF: Hawa wanatumia Totalization formula.

NOTED: Kauli hii bado haijaanza kufanya kazi mpaka pale miongozo na taratibu zitakapotolewa.

Imeandikwa na Thomas Ndipo Mwakibuja, Mtaalam wa hifadhi ya Jamii (Social Protection Expert).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…