Ufanye biashara gani katika mkoa gani?

Ufanye biashara gani katika mkoa gani?

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,286
Reaction score
6,736
habarini wana JF, nimeamua kuanzisha hii thread maalum ili tuweze kupeana INFORMATION za mikoa mbali mbali kwani wana JF wanatoka mikoa tofauti. Mfano nataka kujua aina gani za biashara ni nzuri katika mkoa wa Dodoma. Unaweza kutueleza kuwa biashara ya Majaketi ni nzuri zaidi katika mkoa wa Dodoma (Kwa wauza nguo) Mtwara unaweza kufanya biashara ya samaki hasa wale wakavu wanaotoka Mwanza wana soko zuri sana kule lakini ni Katika wilaya zake si pale mkoani.
Unaweza kutueleza kuwa mahitaji ya chumvi kwa mkoa wa Ruvuma ni makubwa sana sina uhakika kwa sasa lakini nakumbuka miaka ya nyuma Songea chumvi ilikuwa bidhaa yenye soko zuri. Mwaka jana nilikuwa mkoa wa Mtwara biashara ni nzuri kuanzia Mwz 10 mpaka FEB. Pia nilivuka mpaka kwa njia za panya na kwenda msumbiji Dawa za mimea na mifugo zinapatikana kwa bei nafuu sana kule! Mfano MUPAFIDAN(ya kuulia wadudu kwenye mimea) nilinunua kwa sh 3,000 nikaiuza Mtwara kwa sh 12,000 na nasikia bei yake ni kubwa zaidi DAR. Tupeane INF. za mikoani NAWASILISHA.
 
Watu wa DAR tupeni ushauri wenu kuhusu biashara za Muhogo na MKaa msikae kimya.
 
Watu wa DAR tupeni ushauri wenu kuhusu biashara za Muhogo na MKaa msikae kimya.

Mkuu Dar ni mkoa wa ajabu sana, biashara nzuri hapa ni za uongo na utapeli kama unaziweza. Si kama hizo zingine hazina soko bali hizo ninazokuambia soko lake ni kubwa Mfano. Unaweza kubuni dawa ya uongo ya kutibu jino bila kung'oa, dawa ya kuongeza nanihiiii, pia dawa ya heshima kwenye ndoa. Pia ukiwa mbunifu zaidi unaweza kubuni hata mbinu ya kunywa damu za wanyama (Hatari kweli), binafsi dawa ya kuongeza nguvu za kiume imenitoa sana lakini ilikuwa ya ukweli niliomba kwa mzee wangu kijijini. Kwa sasa nimeacha kama unataka unaweza kuendeleza zinauzika sana hapa Dar.
 
Mkuu Dar ni mkoa wa ajabu sana, biashara nzuri hapa ni za uongo na utapeli kama unaziweza. Si kama hizo zingine hazina soko bali hizo ninazokuambia soko lake ni kubwa Mfano. Unaweza kubuni dawa ya uongo ya kutibu jino bila kung'oa, dawa ya kuongeza nanihiiii, pia dawa ya heshima kwenye ndoa. Pia ukiwa mbunifu zaidi unaweza kubuni hata mbinu ya kunywa damu za wanyama (Hatari kweli), binafsi dawa ya kuongeza nguvu za kiume imenitoa sana lakini ilikuwa ya ukweli niliomba kwa mzee wangu kijijini. Kwa sasa nimeacha kama unataka unaweza kuendeleza zinauzika sana hapa Dar.

niku pm??????/kwa ajili ya hiyo dawa ya nguvu za kiume
 
Dodoma apartments, lodges zinalipa.
Biashara ya matunda pia.
 
niku pm??????/kwa ajili ya hiyo dawa ya nguvu za kiume

Mkuu ile dawa nimemaliza wateja wangu wakubwa walikuwa wahindi kila siku wanaiulizia ingawa na wengine wapo lakini wahindi ni kiboko.
 
Gazeti inaonyesha ni Dodoma, Mtwara na Dar tu ndo kuna biashara. Hiyo mikoa mingine labda kilimo tu. Au wana JF si wataalamu wa mambo unayotaka kujua. Labda ufanye ziara kwenye maeneo hayo we huoni hata mahindi, matunda n.k yote yanapatikana hapa DAR wakati hakuna kilimo hicho hapa.
 
mimi akili yangu ya kawaida inanishawishi kwamba katika ile mikoa yenye mazingira ya kilimo hasa maeneo ya vijijini,vifaa vya kilimo na materials kama mbolea,madawa ya kuua wadudu na mbegu. Lakini pia hali ya hewa kama ya baridi katika mikoa fulani inaifanya biashara ya makoti,masweta,mablanketi na majaketi pia kipindi cha mvua,katika mikoa ya joto kama dar bila shaka nguo nyepesi zinauzika zaidi,vifaa vya ujenzi ni biashara inayofana karibia kila mkoa hasa unaoendelea kukua.hebu wengine endeleeni kutoa mawazo,mm ngoja niishie hapo.
 
tatizo kubwa la watu tunafanya vitu kimazoea au kwa kukariri.....inakubidi ufanye kaji-tafiti katika biashara unayotaka kufanya kujua walengwa ni kina nani na kuchanganua kadirio la market share.

Mfano Dar unanafasi ya kufanikiwa katika biashara nyingi kutokana na purchase power kuwa kubwa na population pia ni kubwa lakini pia kuna ushindani mkubwa...kwa hivyo cha msingi ni kujaribu kuona kipi chafaa....
 
Back
Top Bottom