Ufaransa imeonesha unafiki mkubwa dhidi ya Werrason & Wenge MM

Ufaransa imeonesha unafiki mkubwa dhidi ya Werrason & Wenge MM

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Leo nipo upande wa Congo. Nawasalimu kwa jina la Bolingo.

Nimesikitishwa mno kusitishwa kwa Show ya mwanamuziki Werrason akiwa na kundi lake la Wenge Maison Mere. Show ilikuwa ifanyike tarehe 25/09/2021 kwenye ukumbi wa Zenith, Paris. Wakati wote wa maandalizi kundi linalojiita Combattants lililopo karibu Ulaya nzima lilitishia kuzuia kutofanyika kwa show hiyo.

Combattants ni kina nani? Hawa ni wacongo wanaoishi Ulaya huku wakipinga serikali ya DRC. Walianza kwa kuipinga serikali ya Joseph Kabila lakini wameendela kupinga hadi utawala huu uliopo kwa sasa. Sasa kwanini wanazuia wanamuziki wa Congo kupiga show Ulaya? Wenyewe wanadai wanamuziki wako upande wa serikali huku wakinufaika bila kujali mateso wanayopitia wacongo wengine. Combattants wenyewe wanaona wanamuziki ni sehemu ya maadui zao kwa maana ya serikali. Uzuiaji wao umefanikiwa na kuwaathiri mno wasanii wa Congo. Kwa zaidi ya miaka 10 imekuwa ngumu kwa mcongo kupiga show Ulaya.

Juzi serikali ya Ufaransa kupitia jeshi la polisi lilitoa Tamko la kusitisha show ya Werrason kufuatia kuwepo taarifa za kiitelijensia kuwapo kwa combattants wataovuruga amani. Ikumbukwe Karibu mwaka mzima kumekuwa na maandalizi ya hiyo show ambayo ilivuta hisia za mashabiki waliokuwa na kiu kali ya rhumba toka kwa mkongwe Werason. Tiketi zilinunuliwa online. Tayari werrason kaanza kurudisha viingilio.

Binafsi naitupia lawama serikali ya Ufaransa kushindwa kudhibiti kikundi kidogo cha wahuni wanaojiita Combattants. Hiyo ni nchi yenye miguvu ya kutosha kila idara. Kutoa tamko la kushindwa ni kama hujuma dhidi ya Werason pia ni kuonyesha wazi kutotaka mwafrika mwenzetu kupiga show pale Zenith. Wangewaazima hata polisi wetu wakatoe kipigo kitakatifu kwa hao Combattants. Kwasababu tayari Combattants wametoa onyo kwa mwanamuziki mwingine kutoka Kinshasa anayejulikana kama komredi Koffi Olomide na kundi lake la Quartier Latin International kwamba watazuia onyesho lake analotarajia kufanya November kwenye ukumbi wa U-Arena, Paris wenye uwezo wa kuchukua watu 40,000, basi ni vema polisi wakawadhibiti toka muda huu. Ingekuwa hapa kwetu hao viongozi wa Combattants wangeshapewa kesi mbaya mbaya zisizo na dhamana. Pia wafuasi wao wangepata kipigo cha mbwa koko.
 
wanapinga utawala upi sasa?? maana ule wa chama tawala uliondolewa ukaja wa upinzani, bado wanapinga tu, sasa wanataka utawala gani
Hili ndo swali karibu kila mtu anajiuliza. Baada ya Kabila kuondoka madarakani watu wakaona ndo muda wa wasanii kupumua lakini hao wahuni wameendelea na msimamo wao.
 
Haya tumekusikia Waite na mmoja wa hao combatants naye tumsikie ili story ibalance ndiyo tutoe comments,

Hao wafaransa siyo makolo, kwanza sawasawa wanavyowakomoa maswala yenu DRC ufaransa mnayapeleka ya Nini!!? Au ndiyo madai yenu wafaransa weusi.
 
Haya tumekusikia Waite na mmoja wa hao combatants naye tumsikie ili story ibalance ndiyo tutoe comments,

Hao wafaransa siyo makolo, kwanza sawasawa wanavyowakomoa maswala yenu DRC ufaransa mnayapeleka ya Nini!!? Au ndiyo madai yenu wafaransa weusi.
Hivi umeelewa post? Unajua tofauti ya "maswala" na show za wanamuziki? Umejivua nguo
 
Leo nipo upande wa Congo. Nawasalimu kwa jina la Bolingo.

Nimesikitishwa mno kusitishwa kwa Show ya mwanamuziki Werrason akiwa na kundi lake la Wenge Maison Mere. Show ilikuwa ifanyike tarehe 25/09/2021 kwenye ukumbi wa Zenith, Paris. Wakati wote wa maandalizi kundi linalojiita Combattants lililopo karibu Ualya nzima lilitishia kuzuia kutofanyika kwa show hiyo.

Combattants ni kina nani? Hawa ni wacongo wanaoishi Ulaya huku wakipinga serikali ya DRC. Walianza kwa kuipinga serikali ya Joseph Kabila lakini wameendela kupinga hadi utawala huu uliopo kwa sasa. Sasa kwanini wanazuia wanamuziki wa Congo kupiga show Ulaya? Wenyewe wanadai wanamuziki wako upande wa serikali huku wakinufaika bila kujali mateso wanayopitia wacongo wengine. Combattants wenyewe wanaona wanamuziki ni sehemu ya maadui zao kwa maana ya serikali. Uzuiaji wao umefanikiwa na kuwaathiri mno wasanii wa Congo. Kwa zaidi ya miaka 10 imekuwa ngumu kwa mcongo kupiga show Ulaya.

Juzi kupitia serikali ya Ufaransa kupitia jeshi la polisi lilitoa Tamko la kusitisha show ya Werrason kufuatia kuwepo taarifa za kiitelijensia kuwapo kwa combattants wataovuruga amani. Ikumbukwe Karibu mwaka mzima kumekuwa na maandalizi ya hiyo show ambayo ilivuta hisia za mashabiki waliokuwa na kiu kali ya rhumba toka kwa mkongwe Werason. Tiketi zilinunuliwa online. Tayari werrason kaanza kurudisha viingilio.

Binafsi naitupia lawama serikali ya Ufaransa kushindwa kudhibiti kikundi kidogo cha wahuni wanaojiita Combattants. Hiyo ni nchi yenye miguvu ya kutosha kila idara. Kutoa tamko la kushindwa ni kama hujuma dhidi ya Werason pia ni kuonyesha wazi kutotaka mwafrika mwenzetu kupiga show pale Zenith. Wangewaazima hata polisi wetu wakatoe kipigo kitakatifu kwa hao Combattants.
Mshindi wa Kweli wa Urais DRC alikuwa Martin Fayulu , kama hili limezuiwa kwa ajili ya hujuma za uchaguzi basi naunga mkono .Pole Werrason .

Ukiunga mkono dhuluma itakurudia
 
Mshindi wa Kweli wa Urais DRC alikuwa Martin Fayulu , kama hili limezuiwa kwa ajili ya hujuma za uchaguzi basi naunga mkono .Pole Werrason .

Ukiunga mkono dhuluma itakurudia
Inawezekana wao walitaka Kabila aondoke, na aingie MPINZANI aliyeshinda kwenye box, sio huyo aliyewekwa na Kabila, kama wale COVID 19 wa Ndugai!
 
Natamani nijiunge na hao Combatants kama vipi nitumie conections mkuu
 
Kama ni wanufaika wa Utawala unaokandamiza haki basi ndio gharama zake hizo,Ulaya sio kama Afrika.
Kwa mujibu wa mtoa mada sabab ni "taarifa za kiintelijensia"hiki chanzo kinafanana na cha siro kipind kile yupo kanda maalum
 
wanapinga utawala upi sasa?? maana ule wa chama tawala uliondolewa ukaja wa upinzani, bado wanapinga tu, sasa wanataka utawala gani
Pengine tungewekewa sababu za wao kupinga tungejua,sababu za kufuta tamasha zilizotolewa ni nini?
 
wanapinga utawala upi sasa?? maana ule wa chama tawala uliondolewa ukaja wa upinzani, bado wanapinga tu, sasa wanataka utawala gani
Pengine tungewekewa sababu za wao kupinga tungejua,sababu za kufuta tamasha zilizotolewa ni nini?
 
Nilikua nikisubiri kwa hamu hili onesho Waafrica ni kama tuna kamkosi fulani hivi
 
Hii ni kama alivyopigwa Spana Diamond kwenye tuzo , Ukishirikiana na Shetani utakwenda na maji
 
Back
Top Bottom