Kuna hili ambalo sikubaliani nalo labda sijui au ni kwa kutokuelewa labda ningepata wachangiaji nao wakachangia.Mtoto anafaulu darasa la saba anapata alama ya A masomo yote-Grade A. Na wengine wengi wana Grade A lakini wote wanapangiwa kuendelea kidato cha kwanza kwenye shule za kata. Ukiuliza unaambiwa Serikali ilitangaza kwamba wote wanaosoma shule za Private watapangiwa shule za kata na wale waliosoma shule za Serikali watapangiwa Serikalini hata kama ufaulu wao ni mdogo.Je hii ni halali hata kama huyo wa private amemzidi alama za kufaulu yule anayesoma shule za Serikali?