Tetesi: Ufisadi idara ya Mahakama

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
Mahakama imeingia kwenye kashfa nzito, Inasemekana Jaji Mmoja mmoja mabye pia mke wake ni jaji, walikuwa na kiwanja walichonunua kwa laki 3 huko kinyerezi mwaka 2007 na sasa wakati mahakama ya ILALA pale mbele ya ccm-lumumba ipo sehemu nzuri kabisa huyu jaji na genge lake walishawishi ile mahakama ihame na huyu Jaji akapendekeza iende KINYEREZI kwenye kiwanja chake, kweli mahakama inasemekana wakanunua kile kiwanja kwa milioni mia tatu tshs 300,000,000/- ambapo hat kodi ya 18% haikulipwa.

pale ilala inasemekana itajengwa mahakama kuu ya ardhi na kuepukana na gharama za kukodi ghorofa la NHC lakini kwa habari zisizo rasmi inasemekana mkurugenzi wa NHC ameshawishi ucheleweshwaji wa ujenzi wa mahakama kuu ya ardhi ili wanufaike na kodi pale mtaa wa samora.
Mahakama hii ya Kinyerezi ipo mbali kariu kilometa 25 kutoka jijini, ipo [orini, mahakimu, wakili wa serikali na watumishi wote wanatoka mjini kati na wengine kigamboni, imekuwa adha kwa mawakili na fedhea, kuwahi kesi ya saa tatu inabidi kutoka posta sa 12 asubuhi, ili uwahi;
upande mwengine ni karaha tu,

mahakama haigusiki, mawakili wanafanya kesi za probono lakini hawalipwi wakati fungu lipo , kila mtu kawa mpigaji
 
umeanza vzuri Kaka, ila mwishoni ht ulichoandika hakieleweki
 
mahakama wanakuwa wezi tena, tutakimbilia wapi sasa sisi wananchi wanyonge?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…