Ufisadi shule ya wasichana ashira

Kassim Awadh

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2012
Posts
884
Reaction score
187
Shule hii kongwe iliyoko mkoani Kilimanjaro sasa imechukua mwelekeo ya kifisadi.
Wanaendesha harambe ya kukusanya pesa kwa ajili ya ujenzi wa uzio ambapo kila mwanafunzi anatakiwa kuchangia Tsh.100,000/=.
wANACHANGISHA KILA MWANANFUNZI tSH 20,000/= kwa ajili ya kugawana walimu/watumishi wa shule hiyo kwa kile uongozi unachoiita "motisha".

Kwa shule hii inayomilikiwa na serikali,jukumu la kujenga uzio/fence linakuwaje la wanafunzi? Walimu/watumishi walioajiriwa na Serikali inakuwaje wachangiwe na wanafunzi/wazazi kupewa motisha?
Ufuati;iaji/uhakiki wa matumizi ya mkichango yote hii uko mikononi mwa nani?
 
yaani toa taarifa kwa mbunge fasta hayo mamichango mabigibigi wachieni wakina saint anna, saint viroba etc
 
Loh nilisoma mimi hapo enzi za mama Mfinanga! Hilo la fensi ni muhumu wajenge aisee maana tulikuwa tunatorokaje!! Unanyanyua nyaya tu oops uko nje, huyoo disco! Kwa hili la kuchangia mimi nafikiri wako sawa kwa sababu kwa shule zetu za serikali sidhani kama kuna kuwaga na mafungu ya vitu kama hivi! Mbona harusi mnachangia jamani! Nafikiri cha msingi ni kuwa na kamati itakayohusisha wazazi ili kusimamia kaproject!
 
Kweli ulichokiandika ni UKWELI mtupu, Me mwenyewe nimeshangaa sana.
Eti kujenga tu Uzio wanatoza Laki moja (100,000).
Huo uzio utakuwa kama UKUTA WA BERLIN nini????????
 
Nilisoma wakati wa Mwl Helen Itanisa. Uzio unajengwa upande gani kwa sababu shule ni kubwa mpaka kule Primary baada ya kuvuka makaburi tulikuwa tunaita ng'ambo. Au upande ule wa Marangu Arisi au kule kiwanja cha mpira wa miguu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…