Kiburi si uungwana
Member
- Sep 6, 2018
- 93
- 290
Kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa sana la watu kuweka ndoto za mafanikio kwenye swala zima la ufugaji kuku, swala ambalo watu wengi wanakosea kuingia kwenye ufugaji bila tathmini za kina HASA juu ya gharama na changamoto za ufugaji huo. Mara nyingi huwa tunaingia na mawazo chanya ya kufanikiwa haraka sana mara tu tunapoanza kufuga.
Ukweli ni kwamba hakuna kitu chenye faida kisichopitia hasara wala changamoto.
Changamoto kubwa ambayo wengi tunaisahau ni gharama za kuwatunza hao viumbe na kama tunazifahamu basi hatuzitafakari kwa kina na mwisho wa siku tunapoanza kufuga tunajikuta tunaanza kutumbukia kwenye utumwa wa kutoa pesa za chakula na madawa ya kuku bila kupenda ama kutarajia. Kuku ni viumbe na wanahitaji chakula bora pamoja na afya njema.
Changamoto kubwa mbili ni:
1) Gharama ya chakula ambayo huwa ni asilimia 75 ya gharama ya ufugaji kuku.
2) Gharama ya matibabu na kinga ambayo hufikia karibu asilimia 5 ya ufugaji wako.
Gharama hizo ni za matunzo ukitoa gharama za ujenzi wa banda pamoja na miundo mbinu.
Naomba nikupe mbinu za kupambana na changamoto hizo nilizo zitaja:
Kwa changamoto ya chakula; Unaweza ukatengeneza chakula cha aina yoyote ya kuku unayefuga kwa kutumia malighafi zilezile zinazotumika kutengenezea chakula kiwandani, kwa kufanya hivi utaokoa gharama karibu asilimia 60, yaani kama ulitakiwa ulishe kuku wako chakula cha sh 1,000,000 basi utajikuta kwa kutengeneza mwenyewe utatumia sh 400,000 kutengeneza chakula chenye ubora uleule wa chakula cha milioni 1.
Kwa changamoto ya maradhi pamoja na kinga unashauriwa uzingatie sana usafi wa jumla kwenye ufugaji wako, usafi huo ni kuanzia wewe mwenyewe, mazingira ya ndani na nje ya banda hasa uhakikishe banda liwe kavu, chakula pamoja na maji safi. Hii ni pamoja na vyombo vya chakula na maji kuwa safi muda wote, cha mwisho ni kuzingatia chanjo kwa wakati.
Kumbuka: Kutozingatia chakula bora cha kuku ni kujihakikishia ukosefu wa kuku bora wasiofaa sokoni na kuwa mzembe dhidi ya afya za kuku ni kujihakikishia msiba wa kuku wako wote.
UKIZINGATIA HAYO UTAJIKUTA UNAIFIKIA ILE HAZINA KUBWA SANA YA UTAJIRI ILIYOJIFICHA KWENYE UFUGAJI AMBAYO WENGI WAMEINGIA HUKO BILA UTASHI na KUIKOSA NA KUJIKUTA WANATAJIRISHA WENGINE NA WAO WAKIISHIA KUWA WATUMWA.
Kwa ushauri na pia malighafi za kutengeneza chakula cha kuku aina yoyote basi tuwasiliane.
Ukweli ni kwamba hakuna kitu chenye faida kisichopitia hasara wala changamoto.
Changamoto kubwa ambayo wengi tunaisahau ni gharama za kuwatunza hao viumbe na kama tunazifahamu basi hatuzitafakari kwa kina na mwisho wa siku tunapoanza kufuga tunajikuta tunaanza kutumbukia kwenye utumwa wa kutoa pesa za chakula na madawa ya kuku bila kupenda ama kutarajia. Kuku ni viumbe na wanahitaji chakula bora pamoja na afya njema.
Changamoto kubwa mbili ni:
1) Gharama ya chakula ambayo huwa ni asilimia 75 ya gharama ya ufugaji kuku.
2) Gharama ya matibabu na kinga ambayo hufikia karibu asilimia 5 ya ufugaji wako.
Gharama hizo ni za matunzo ukitoa gharama za ujenzi wa banda pamoja na miundo mbinu.
Naomba nikupe mbinu za kupambana na changamoto hizo nilizo zitaja:
Kwa changamoto ya chakula; Unaweza ukatengeneza chakula cha aina yoyote ya kuku unayefuga kwa kutumia malighafi zilezile zinazotumika kutengenezea chakula kiwandani, kwa kufanya hivi utaokoa gharama karibu asilimia 60, yaani kama ulitakiwa ulishe kuku wako chakula cha sh 1,000,000 basi utajikuta kwa kutengeneza mwenyewe utatumia sh 400,000 kutengeneza chakula chenye ubora uleule wa chakula cha milioni 1.
Kwa changamoto ya maradhi pamoja na kinga unashauriwa uzingatie sana usafi wa jumla kwenye ufugaji wako, usafi huo ni kuanzia wewe mwenyewe, mazingira ya ndani na nje ya banda hasa uhakikishe banda liwe kavu, chakula pamoja na maji safi. Hii ni pamoja na vyombo vya chakula na maji kuwa safi muda wote, cha mwisho ni kuzingatia chanjo kwa wakati.
Kumbuka: Kutozingatia chakula bora cha kuku ni kujihakikishia ukosefu wa kuku bora wasiofaa sokoni na kuwa mzembe dhidi ya afya za kuku ni kujihakikishia msiba wa kuku wako wote.
UKIZINGATIA HAYO UTAJIKUTA UNAIFIKIA ILE HAZINA KUBWA SANA YA UTAJIRI ILIYOJIFICHA KWENYE UFUGAJI AMBAYO WENGI WAMEINGIA HUKO BILA UTASHI na KUIKOSA NA KUJIKUTA WANATAJIRISHA WENGINE NA WAO WAKIISHIA KUWA WATUMWA.
Kwa ushauri na pia malighafi za kutengeneza chakula cha kuku aina yoyote basi tuwasiliane.