Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Mlachake

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2009
Posts
4,437
Reaction score
4,618

Hey JF Members.

Ee bwana kuna mtu anaweza kunipa msaada wa mchanganuo wa kufuga kuku. Naona soko la kuku ni kubwa sana. Hii ni biashara ambayo soko lake liko tayari. hotels, functions, vibanda vya chipss. Yeyote mwenye idea naomba msaada please!

BAADHI YA MASWALI NA MAHITAJI YA WADAU
Habari ndugu zangu,

Naomba mnisaidiye nataka kuanza kufuga kuku wa kisasa ila sina elimu nao.

Naombeni mwenye ujuzi anisaidie

Sent using Jamii Forums mobile app


MICHANGO YA WADAU MBALIMBALI

 
Coaster mzee mfuko mdogo! hapo parefu kidogo mzee. 40m kwa mwajiriwa ni parefu kidogo.
 
Mkuu ulishawai kufuga kuku, japo 50?

Maana kama ni wale broilers wakipata ugonjwa unaweza kupata presha, tena kama pesa ndo za FINCA, itakula kwako. Bora kuku wa mayai, ila ndio hivyo uwe na mtaji mnene coz wanakula kwa miezi 5-6 ndo waanze kutaga mayai!
 
Hapo sawa ila idea ya kusubili mpaka upate 40m hapana ilikuwa haivutii (there waz no growth orientation), swahiba karibu katika kada hii ya ujasiliamali hata hivyo si lazima uache kazi ndoo uingie kwani jambo zuri na la busara katika ujasiliamali ni kuhakikisha unamiliki mtandao ambao utakuwa unakuingizia fedha hata kama upo kwenye machela, mathalani wewe umeliona hilo na kutaka kujikita ktk kuku. Good idea, and for further info just ni PM.
 
Kuku ni biashara nzuri sana lakini inabidi uwe mjanja, kwanza jifunze kutengeneza chakula cha kuku mwenyewe
usiwe unanunua. Pili usiwe mbahili, hakikisha wanakula vizuri na madawa ya kupulizia kwenye mabanda unatumia
anza na kuku 2000.

Good luck.
 
Kuku ni biashara nzuri sana lakini inabidi uwe mjanja, kwanza jifunze kutengeneza chakula cha kuku mwenyewe usiwe unanunua. pili usiwe mbahili. Hakikisha wanakula vizuri na madawa ya
kupulizia kwenye mabanda unatumia anza na kuku 2000.

Good luck.

Well said, ni sawa kabisa, kujifunzia unaweza anza na cha kununua, ila faida hamna, tengeneza chakula mwenyewe, hakikisha usafi wa vyombo na banda, zuia ubichi bandani, hakikisha wakiumwa tu, watenge ukianza kusitasita ndo anavyosema huyo banda zima linakwisha.

Unaweza fuga kiasi chochote ila as a precaution nakushauri weka 200 banda moja kwa kuanzia ila pata ushauri wa vipimo per sq mita.
 
Yaani umenichekesha kweli. Unajua umenigusa na hapo kwenye Red! Huo ndo ukweli, lakini sisi wafanyakazi ndo tunajazaga Bar mida ya jioni.
 
Mlachake, una experience kwenye ufugaji kuku? kama huna basi, kuanza na kuku 1000 utakuja kulia. Na kama ni lazima uanze na kuku wengi,basi usiwe na mkono wa birika, kwamba usiwe bahili.

Lazima utafute part time animal scientist ambae atakuwa mara kwa mara anakushauri suala zima la poutry management!!! aidha,usiwe bahiri, hususani kwenye feeding!!! poultry keeper wengi wana-collapse kv wanataka kubana matumizi kwenye chakula---manake wale jamaa wanafukia ile mbaya.

In order to have productive layers or broilers, lazima kwenye masuala ya misosi wajiachie!!! and even more important, especially kama ni kuku wa mayai, tenga bajeti ya chakula pembeni na usiichezee kwa kitu kingine chochote kile, iwe pale ready for feeding!! Kama utapata mtaalamu, akakupa techinques za kutengeneza chakula itakuwa more wise kwako, kwavile feed cost ipo juu sana.

BUT be careful, usi-opt tu kutengeneza chakula chao wakati feed chemistry haunayo!!! kama ni wa mayai, badala ya kuanza kutaga after 5 ro 6 months, wataanza after 8 months!!!Kama unazani hutaweza kufanya mixing vizuri, u better ukajilipue kwenye vyakula vya madukani ambavyo ni very expensive- but don' worry, bei hiyo haitakufanya upate hasara, but itapunguza faida!! na kitu kingine muhimu, don buy day old chicks mitaani, utakuja kulia!!!hizo ni few hints, but the project, inalipa wangu!!!

Mengine yote, unaweza kushauriwa na animal scientist, but the first good strategy --- tafuta kijana ambae tayari ameajiriwa kwenye suala zima la utunzaji kuku -- mchomoe anakofanya kazi na mpe mshahara mkubwa zaidi, na mpangie room very close na yalipo mabanda yako!!! uki-opt kujenga annex ya kukaa poultry keeper, itakuwa ni more productive idea! wish u all the best
 
Mradi wa kuku ni mzuri haswa pale ambapo unakuwa na uzoefu wa jinsi ya kuwatunza na kufuatilia soko lake. Kwa mtizamo wangu naona kama unapendelea zaidi kuku wa nyama ambao kiasi fulani ni wagumu kuliko kuku wa mayai.

Ni muhimu ukiangalia yafuatayo kwa ustawi wa kuku wa nyama.

1. Kuwa na banda zuri lenye hewa ya kutosha pamoja na joto la kutosha (unaweza kupata vitabu kutoka kenye veterinary mbali mbali). Banda ni wastani wa mita 4 kwa 4 kwa kuku 200 wa nyama au 100 wa mayai. Hakikisha banda ni safi na umelipulizia dawa kabla ya kuingiza kuku (unaweza kutumia detto).

2a. Kwa mtu unaeanza ni vizuri kutumia chakula cha kiwandani kwa ubora kwani mara nyingi vyakula vya kujitengenezea vinaweza kuwa ma upungufu au kutengeezwa katika mazingira yasiyo mazuri na hatimaye kuwa na matokeo duni. Kumbuka wanahitaji vakula veyenye virutubisho tofauti kulingana na umri (mfano starter & finisher kwa broiler)

2b. Hakikisha wanapata chanjo ya newcastle wiki ya pili kwa kukuwapya utakaowaleta. Ni muhimu sana. Pia viatamini na madini kama utakavyoshauriwa na watalamu wa mifugo

3a. Kama una uwezo mzuri ni vizuri kufuga kwa awamu. Mathalani wapishane kwa wiki 2, (yaani unaingiza kukuwapya kila baada ya wiki mbili). Hii inakupa nafasi nzuri haswa kupunguza gharama za malisho na nafasi, kwani kadri wanapokuwa ndivyo unavyoongeza nafasi ya banda. Kumbuka broiler.

3b. Hakikisha kuna vyombo vya chakula na maji vya kutosha. Kuku wa nyama hawahitaji kwenda umbali mrefu kutafuta maji, na viwe na maji pamoja na chakula wakati wote.

3c. Hudumia kuku wadogo kwanza, ndipo umalizie kwa wakubwa. Usafi ni muhimu sana. Kuwe na masodasti na hakikisha hakuna unyevu unyevu ili wasipate maambukizo ya magonjwa ya baridi.vifo vingi sana huweza kutokea. Ni vizuri ukahakikisha kuwa hakuna kuku wa kienyeji, kwani mara nyingi huwa chanzo cha magonjwa.

4. Soko ndio kichaa kikubwa katika biashara ya kuku wa nyama, na faida yote hupotea baada ya kukomaa endapo soko linakosekana. Jiandae vyema kama ikiwezekana baada ya kufikisha uzito stahili (baada ya wiki 5-6) unawachinja wote na kuwauza au kuwahifandhi ndani ya jokofu na kuwauuza taratibu.

Baada ya hapa unaweza kuangalia nafasi yako ya kukuwa na kuwa uzoefu kupanua biashara. Ushauri wa wataalamu ni muhimu sana kufanikisha malengo, ila pia kumbuka ubabaishaji ni mwingi Afrika!
 
Mkuu tazama hizo picha hapo chini;

Nilikuwa mmikoa ya kusini just three weeks ago, tutatembelea banda la mkulima mmoja na kuona jinsi alivyojikwamua kwa ufugaji kuku wa kienyeji. Alianza kufugia kwenye banda la kupikia, then sasa amejenga banda jipya, anafuga kwa kutumia njia bora zaidi kuku wale wale wa kienyeji. Kwa hivyo haihitaji kuanza na maelfu ya kuku, bali kidogo kadri unavyoweza, kikubwa ni kuhakikisha unawapatia huduma bora zikiwamo chakula na madawa.

Cheers..!

 

Mkuu naona shule hapo imetulia!

Lakini mbona mnazungumzia haya makuku ya kisasa tu? Je, ufuguja wa kitaalam wa kuku wa KIENYEJI unakuwaje? Kumbuka hawa nao wana soko zuri sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…