Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko


Pia unaweza jielimisha juu ya ufugaji wa mifugo mbalimbali ikiwemo ufugaji wa kuku kwa kusoma hapa
SEKTA YA MIFUGO TANZANIA
 
Mkuu kama mayai yataweza kuhifadhiwa kwenye aircondition kama ulivyoeleza hapo juu yanaweza kukaa muda gani bila kuharibika?

Exactly life span yake kama ni miezi mingapi,hilo naomba uniachie nilifanyie utafiti kidogo nitakujibu,ila kinachojulikana kuwa mayai yaliyohifadhiwa kwenye air condition yana uwezo wa kukaa muda mrefu tu,na hii huwasaidia wafugaji pale ambapo soko la mayai linapokuwa sio zuri,wanayahifadhi ili kusubiri soka.
 

Mh mafia boy, tuwasiliane kama utahitaji hiyo elimu, nitakuPM namba zangu.
 
Kwa wastani wa kama kuku 100 wa mayai, wanahitaji mabanda mangapi na makadirio ya gharama za ununuzi pamoja na ujenzi wa mabanda yaweza kuwa shilingi ngapi bwana mtaalamu?
 
Bradha kichwa mbovu, nitakutafuta kwani nina mpango kazi wangu wa kutaka kufuga kuku machotara, hawa wa kienyeji machotara kwa ajili ya mayai na nyama. Hasa nataka pia niwe natotoresha kwani nimeona vitotoresho (incubators) vizuri kwenye mtandao na havina gharama sana.

Ila la haraka ni hili naomba maelekezo ya namna ya kutengeneza chakula cha hao high breeds wa kienyeji mwenyewe nyumbani. Mengine tutatafutana as we go along humu JF - KISIMA CHA KUKOMBOANA.
 

Nashukuru sana mkuu wangu mwenyezi mungu akubaliki na itabidi basi nikutafute na tuangalie namna ya kufanya maana ushauri wako umeelezea na umekuwa deep zaidi tunashukuru sana, naona kumb hata kama sehemu hamna umeme hii kazi ni possible basi ni sawa kaka.

Na mwenyewe huwa sio mkaaji sana wa sehemu moja kutokana na shughuli zangu sasa hapo haito kuwa problem kweli?
 
Kwa wastani wa kama kuku 100 wa mayai, wanahitaji mabanda mangapi na makadirio ya gharama za ununuzi pamoja na ujenzi wa mabanda yaweza kuwa shilingi ngapi bwana mtaalamu?

Swali zuri sana nadhani nitapata na mimi majibu kutoka kwenye hili swali
 
CHANJO NA KINGA DHIDI YA MAGONJWA MBALIMBALI YA KUKU WA MAYAI,NYAMA(BROILERS) AU CHOTARA(CROSSED BREED)

[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD]
UMRI
KATIKA
SIKU/WIKI
[/TD]
[TD="width: 160"]
AINA
YA
UGONJWA
[/TD]
[TD="width: 160"]
CHANJO/KINGA
[/TD]
[TD="width: 188"]
NJIA YA UTOAJI
WA
DAWA
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
Mara baada ya kutotolewa
[/TD]
[TD="width: 160"]
Marek's
[/TD]
[TD="width: 160"]
HVT
[/TD]
[TD="width: 188"]
SINDANO(Kiwandani)
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
1
[/TD]
[TD="width: 160"]
Kuondoa uchovu
[/TD]
[TD="width: 160"]
Glucose
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
2-6
[/TD]
[TD="width: 160"]
Pullorum
[/TD]
[TD="width: 160"]
Trisulmycine,Trimazine 30%au Cotrim+Vitalyte,Amin'total au Broiler booster
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
7
[/TD]
[TD="width: 160"]
Mndondo
[/TD]
[TD="width: 160"]
Newcastle vaccine(Lasota)
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
14
[/TD]
[TD="width: 160"]
Gumboro
[/TD]
[TD="width: 160"]
Gumboro (Bursine vaccine-IBD)
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
16-20
[/TD]
[TD="width: 160"]
Coccidiosis
[/TD]
[TD="width: 160"]
Trisulmycine/Trimazine/Esb3 30%+Dawa yoyote ya Vitamin
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
21
[/TD]
[TD="width: 160"]
Mdondo
[/TD]
[TD="width: 160"]
Newcastle vaccine(Lasota)
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
23-27
[/TD]
[TD="width: 160"]
Kinga dhidi ya magonjwa mengi
[/TD]
[TD="width: 160"]
OTC 20%+Dawa ya vitamin yoyote
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
28
[/TD]
[TD="width: 160"]
Ndui
[/TD]
[TD="width: 160"]
Fowl pox vaccine
[/TD]
[TD="width: 188"]
Sindano kwy mabawa
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
35-39
[/TD]
[TD="width: 160"]
Mafua
[/TD]
[TD="width: 160"] Coridix,Tylosine75%+dawa yoyote ya vitamin[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
56-60
[/TD]
[TD="width: 160"]
Kinga dhidi ya magonjwa mengi
[/TD]
[TD="width: 160"]
OTC 20%+Dawa yoyote ya vitamin
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
WIKI YA 12
[/TD]
[TD="width: 160"]
Taifodi(Fowl typhoid)
[/TD]
[TD="width: 160"]
Gentamyzine sulphate
[/TD]
[TD="width: 188"]
Sindano
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
Wiki ya 13
[/TD]
[TD="width: 160"]
Minyoo
[/TD]
[TD="width: 160"]
Pipperazine cirtrate+Dawa yoyote ya vitamin
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
WIKI YA 15
[/TD]
[TD="width: 160"]
Ukataji midomo
[/TD]
[TD="width: 160"]
Dawa ya vitamin itumike baada ya zoezi
[/TD]
[TD="width: 188"]
Maji
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
WIKI YA 16
[/TD]
[TD="width: 160"]
Kipindupimdu (fowl cholera)
[/TD]
[TD="width: 160"]
OTC 20% Injection
[/TD]
[TD="width: 188"]
Sindano
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
WIKI YA 17
[/TD]
[TD="width: 160"]
Mafua (Infectious coryza)
[/TD]
[TD="width: 160"]
Tylosine Injection
[/TD]
[TD="width: 188"]
Sindano
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 162"]
WIKI YA 18
[/TD]
[TD="width: 160"]
Taifodi(Fowl typoid)
[/TD]
[TD="width: 160"]
Gentamizine sulpate
[/TD]
[TD="width: 188"]
Sindano
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



MUHIMU

· Dawa ya minyoo irudiwa kila baada ya miezi 3 toka ilipotolewa awamu ya kwanza .
· Dawa ya mdondo irudiwa kila baada ya miezi 3 toka ilipotolewa siku ya siku ya 21.

KIASI CHA CHAKULA ANACHOHITAJI KUKU KUANZIA WIKI YA 1 HADI
MWISHO WA UTAGAJI WIKI YA 80


[TABLE="class: MsoTableGrid"]
[TR]
[TD] AINA
YA
CHAKULA[/TD]
[TD="width: 129"] CHICKS'
STARTER[/TD]
[TD="width: 128"] GROWERS'
MASH[/TD]
[TD="width: 127"]
LAYERS'​
MASH​
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 128"] UMRI/
WIKI[/TD]
[TD="width: 129"] 0-8[/TD]
[TD="width: 128"] 9-20[/TD]
[TD="width: 127"]
21-80​
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 128"] CHAKULA/
KUKU[/TD]
[TD="width: 129"] 2kg[/TD]
[TD="width: 128"] 6kg[/TD]
[TD="width: 127"] 52kg[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 128"] CHAKULA/
KUKU 500[/TD]
[TD="width: 129"] 1000kg[/TD]
[TD="width: 128"] 3000kg[/TD]
[TD="width: 127"] 52kg[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 128"] MIFUKO@
50Kg/KUKU 500[/TD]
[TD="width: 129"] 20[/TD]
[TD="width: 128"] 60[/TD]
[TD="width: 127"] 520[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

MUHIMU
· Kuanzia wiki ya 18-20, kuku wanapaswa kupewa chakula cha Growers kilichochanganywa na Layers.
 

Tuwasiliane tu nitakupatia.
 
Kwa wastani wa kama kuku 100 wa mayai, wanahitaji mabanda mangapi na makadirio ya gharama za ununuzi pamoja na ujenzi wa mabanda yaweza kuwa shilingi ngapi bwana mtaalamu?

Nitakujibu kukicha,kwa sasa muda umenibana kidogo mkuu.
 
Kwa wastani wa kama kuku 100 wa mayai, wanahitaji mabanda mangapi na makadirio ya gharama za ununuzi pamoja na ujenzi wa mabanda yaweza kuwa shilingi ngapi bwana mtaalamu?

Kuku 100 wanahitaji chumba kimoja tu chenye ukubwa wa mita 6 kwa mita 3.

Siwezi kukupa gharama halisi ya ujenzi wa mabanda kwani gharama inatofautiana kati ya mahali na mahali.Nitakachofanya ni kukupa mahitaji ya ujenzi wa banda la kuku lenye vyumba 2 na stoo 1 kwa ajili ya kuhifadhia dawa,chakula na mayai, kila chumba kikiwa na uweza wa kubebe kuku 100.

MAHITAJI KWA UJENZI WA NYUMBA YA KUKU

  1. Tofali za block 5000 au tofali ndogo za kawaida zilizochomwa 12000
  2. Bati 68x2mita.
  3. Kenchi 24x2"x3"x12"
  4. Boriti kwa milango na madirisha 12x12"x1"x12'
  5. Lati 12x25"
  6. Vipande vya lati kwa kuwekea makasha ya kuku 8x12'
  7. Futi 100 za waya kwa kugawa vyumba na kunga madirisha.
  8. Mifuko20 ya saruji.
  9. Kilo 5 za misumari ya bati na kilo 7 ya Misumari ya waida
  10. Mchanga Lory 2
  11. Dazan1 ya bawaba
  12. Komeo 3 na kufuli moja.

Kwa kutumia data hizi mfugaji ana weza akajua gharama za ujenzi wa nyumba ya kuku.
 

Mkuu kwa experience yangu tofali 5000 ni nyingi sana hiyo mbona ni ghorofa kabisa? nadhani tofali 1000 zinatosha kabisa kumbuka mabanda ya kuku huwa na madirisha makubwa sana na halina complications zozote
 
Mkuu kwa experience yangu tofali 5000 ni nyingi sana hiyo mbona ni ghorofa kabisa? nadhani tofali 1000 zinatosha kabisa kumbuka mabanda ya kuku huwa na madirisha makubwa sana na halina complications zozote
Hizi data nimezikopy kutoka kwenye kitabu kinachoitwa Ufugaji bora wa kuku Tanzania kilichochapwa na Peramiho printing press cha mtafiti mmoja anaitwa Joseph Goodwin.Hizi data kwa mujibu wa mwandishi ni kwa ajili ya maeneo ya baridi na hasa mkoa wa Iringa.Niliweka hizi data kusudi kuwapa mwanga wafugaji, but kwa hili la ujenzi wadau wenyewe wa mifugo mna ujuzi zaidi.

Mimi mara nyingi huwa napenda kutoa zile specification,yaani kuku wangapi na wanahitaji kiasi gani cha eneo la mita square,sifa za mabanda ya kuku na pia kutoa sketch za ramani ya mabanda ya kuku. Nitajitahidi nitake time kwenye kufanya evaluation ya gharama kwenye ujenzi wa mabanda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…