Ladder 49
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 7,918
- 20,037
Wakuu habari zenu?
Niingie moja kwa moja kwenye mada.
Baada ya kusoma habari ya forex humu jamii forum nilitamani sana niijue hiyo biashara .
Baada ya muda nikaona post humu ikiwa inaelezea kuna watu watakuwa wanafundisha hiyo biashara hapa TZ. Lakini hapo hapo mtoa mada akawa anasema watu wa mikoani mpaka wafike watu 100 ndio jamaa waje kuwa findisha ,wajikusanye kwenye makundi ya whatsapp. Kama hawajafika 100 awezikuja kufundisha.
Baada ya kuona hayo nikaona isiwe tabu sana nikaamua kuingia YouTube Na kwenye google na kujisomea mwenyewe nilianza mdogo mdogo.
Nikipata nafasi ofisini au home nakuwa nasoma na kutazama video
Taratibu nikaona naanza kupata picha forex nibiashara gani.
kuna siku nikampigia simu rafiki yangu ambaye tuliosoma wote nikamuuliza hivi unajua biashara ya forex ,akanijibu umeijulia wapi nikamwambianiliijulia jamii forum ,halafu nikaisoma mwenyewe tu. Baada ya maongezi ya forex akaniaidi kunitumia kitabu cha forex na akaniambia nikimaliza hicho nitakuwa vizuri.
Yeye ilikuwa imepita kama wiki mbili tu ndio ametoka kufundishwa.
Kwa huo muda mfupi tulioongea aliona uwezo wangu
Alitimiza ahadi ya kunitumia hicho kitabu.
Kusema ukweli hicho kitabu nilisoma chapter moja tu ,nikaona mbona vyote na vijua tu kama marudio tu ,nikajaribu kuangalia chapter za mbele nikaona vyote na vijua
Nikaamua kuachana nacho ,hicho kitabu walipewa huko walipofundishwa.
Kuna siku nikamcheck rafiki yangu mwingine tukapiga story mbili tatu nikaingizia mada ya forex ,akaniambia nisiangaike kusoma akaniambia wewe ukipata nafasi njoo mjini nikufundishe ni masaa 3&4 tu unaitaji utakuwa unajua,akaongezea wewe usijisumbue kusoma .
Baada ya miezi kupita nilipata nafasi weekend moja nikaenda dar ,jamaa akanifundishe ,nilionana na jamaa akanifundisha Baada ya masaa matatu na nusu tukawa tumemaliza .
Kwa kweli sijaona jipya zaidi ya broker aliyenipa na app ya kuangalia news.
Alinifungulia account ya demo nikawa na trade ,ingawa kabla ya hapo nilikuwa nimeshawahi kutrade na demo.
Labda ni Vitu gani hivyo nilivyokuwa nimejifunza mpaka kila mtu akinifundisha nione marudio?
hivi hapa.
Kwenye kujisomea kwangu nilibahatika kuzipata video ambazo zenye title hizo hapo chini
1.forex foundation.
2.forex trading market structure
3.forex trading fundamentals .
4.Technical strategies forex trading.
5.risk management forex trading.
Kuna website nilipata pia ilikuwa na majina ya brokers wengi sana niliweza kuchagua na kufungua demo account na kupata platform na kutrade demo.
Niliangalia video nyingi ila hizo zilikuwa the best.maana zilinipa mwanga wa forex vizuri sana.jamaa anaongea taratibu hana papara.
Baada ya muda tena nilienda dar kwa ishu zangu safari hii nilikuwa na muda sana .muda mwingi nikawa na hao rafiki zangu muda mwingi wanakuwa wanafanya hivyo biashara nilichokiona ndio kikanifanya niandike hii mada.
Hao Wote marafiki zangu hawajui kutrade vizuri,
Wote wameshaunguza account zaidi ya mara mbili.
Nikataka sana nijuie kwanini walichoma account kila mtu nilimuuliza kwa muda wake bila wao kujijua mwingine aliniambia yeye alikuwa anatrade bila kuweka stop loss.
Mmoja nilimuuliza hivi imekuwaje umeunguza account akaniambia yule jamaa aliyewafundisha aliwaambia waingie kumbe sio(jamaa aliwaingiza chaka) alilaza trade kusubiria itapanda maana mwalimu kasema ,asubuhi anaamka hakuna kitu.
Kitu nilichokiona kutoka kwao nikwamba wako kwenye magroup ya whatsapp huyo walimu wao anakuwa anawatumia waingie kwenye point gani na wao wanafanya hivyo ndio maisha yanaenda .
Nilijiuliza hivi inakuwaje ulilipa hela 150000/- siku tano zote ufundishwe forex halafu mwisho wa siku bado mwalimu anawaweka kwenye magroup nakuwa tumia point uingie muda gani na kutoka na wakati huyo jamaa alikuwa tayari ameshawafundisha na demo tayari umetrade sana .nilijiuliza sana
Nimegundua course content wanazotumia ni uzushi mtupu. Wengi waliofundishwa hawawezi kuanalyse data na kufanya trade .walimu wanakwepa kufundisha vitu muhimu vizuri,sasa bila hivyo wata trade vipi?
Hawafundishi vizuri vitu ambavyo wao wanazotumia kuanalyse data nakujua muda gani aingie na kutoka kwenye trade .hiyo chini hapo ni picha ya moja ya course content ya walimu wa forex bongo na nje ya bongo nimeitoa instagram kutolea mfano tu
Hii picha ya chini ni moja wa walimu wa forex South Africa huko najaribu kulinganisha course content
Kwa course content hizo za bongo nikupotezeana muda tu , wewe kikubwa unatakiwa ujue uingie muda gani na utoke muda gani kwenye trade,wao wanakufundisha vitu ambavyo avitakusaidia vinakuwa vingi sana pasipo kujua mahitaji ya unaemfundisha .
Tunafundishwa hiyo forex ilituje na sisi kupiga hela kwenye kutrade na sio kwenda kufundisha watu wengine basi.
kila siku tutaishia kuunguza account na kulaumu jamaa wezi ,Haita tusaidia .
Ona training za wenzetu short and clear .sisi huku maelezo mengi kuongopeana tu na kuonesha ujuaji nakutaka kuabudiwa kama miungu watu.
Syllabus ya forex aijulikani kila mtu anajipangia tu ilimradi apige pesa zenu tu, kwa sababu tu hatujui forex.
Nawasilisha
Niingie moja kwa moja kwenye mada.
Baada ya kusoma habari ya forex humu jamii forum nilitamani sana niijue hiyo biashara .
Baada ya muda nikaona post humu ikiwa inaelezea kuna watu watakuwa wanafundisha hiyo biashara hapa TZ. Lakini hapo hapo mtoa mada akawa anasema watu wa mikoani mpaka wafike watu 100 ndio jamaa waje kuwa findisha ,wajikusanye kwenye makundi ya whatsapp. Kama hawajafika 100 awezikuja kufundisha.
Baada ya kuona hayo nikaona isiwe tabu sana nikaamua kuingia YouTube Na kwenye google na kujisomea mwenyewe nilianza mdogo mdogo.
Nikipata nafasi ofisini au home nakuwa nasoma na kutazama video
Taratibu nikaona naanza kupata picha forex nibiashara gani.
kuna siku nikampigia simu rafiki yangu ambaye tuliosoma wote nikamuuliza hivi unajua biashara ya forex ,akanijibu umeijulia wapi nikamwambianiliijulia jamii forum ,halafu nikaisoma mwenyewe tu. Baada ya maongezi ya forex akaniaidi kunitumia kitabu cha forex na akaniambia nikimaliza hicho nitakuwa vizuri.
Yeye ilikuwa imepita kama wiki mbili tu ndio ametoka kufundishwa.
Kwa huo muda mfupi tulioongea aliona uwezo wangu
Alitimiza ahadi ya kunitumia hicho kitabu.
Kusema ukweli hicho kitabu nilisoma chapter moja tu ,nikaona mbona vyote na vijua tu kama marudio tu ,nikajaribu kuangalia chapter za mbele nikaona vyote na vijua
Nikaamua kuachana nacho ,hicho kitabu walipewa huko walipofundishwa.
Kuna siku nikamcheck rafiki yangu mwingine tukapiga story mbili tatu nikaingizia mada ya forex ,akaniambia nisiangaike kusoma akaniambia wewe ukipata nafasi njoo mjini nikufundishe ni masaa 3&4 tu unaitaji utakuwa unajua,akaongezea wewe usijisumbue kusoma .
Baada ya miezi kupita nilipata nafasi weekend moja nikaenda dar ,jamaa akanifundishe ,nilionana na jamaa akanifundisha Baada ya masaa matatu na nusu tukawa tumemaliza .
Kwa kweli sijaona jipya zaidi ya broker aliyenipa na app ya kuangalia news.
Alinifungulia account ya demo nikawa na trade ,ingawa kabla ya hapo nilikuwa nimeshawahi kutrade na demo.
Labda ni Vitu gani hivyo nilivyokuwa nimejifunza mpaka kila mtu akinifundisha nione marudio?
hivi hapa.
Kwenye kujisomea kwangu nilibahatika kuzipata video ambazo zenye title hizo hapo chini
1.forex foundation.
2.forex trading market structure
3.forex trading fundamentals .
4.Technical strategies forex trading.
5.risk management forex trading.
Kuna website nilipata pia ilikuwa na majina ya brokers wengi sana niliweza kuchagua na kufungua demo account na kupata platform na kutrade demo.
Niliangalia video nyingi ila hizo zilikuwa the best.maana zilinipa mwanga wa forex vizuri sana.jamaa anaongea taratibu hana papara.
Baada ya muda tena nilienda dar kwa ishu zangu safari hii nilikuwa na muda sana .muda mwingi nikawa na hao rafiki zangu muda mwingi wanakuwa wanafanya hivyo biashara nilichokiona ndio kikanifanya niandike hii mada.
Hao Wote marafiki zangu hawajui kutrade vizuri,
Wote wameshaunguza account zaidi ya mara mbili.
Nikataka sana nijuie kwanini walichoma account kila mtu nilimuuliza kwa muda wake bila wao kujijua mwingine aliniambia yeye alikuwa anatrade bila kuweka stop loss.
Mmoja nilimuuliza hivi imekuwaje umeunguza account akaniambia yule jamaa aliyewafundisha aliwaambia waingie kumbe sio(jamaa aliwaingiza chaka) alilaza trade kusubiria itapanda maana mwalimu kasema ,asubuhi anaamka hakuna kitu.
Kitu nilichokiona kutoka kwao nikwamba wako kwenye magroup ya whatsapp huyo walimu wao anakuwa anawatumia waingie kwenye point gani na wao wanafanya hivyo ndio maisha yanaenda .
Nilijiuliza hivi inakuwaje ulilipa hela 150000/- siku tano zote ufundishwe forex halafu mwisho wa siku bado mwalimu anawaweka kwenye magroup nakuwa tumia point uingie muda gani na kutoka na wakati huyo jamaa alikuwa tayari ameshawafundisha na demo tayari umetrade sana .nilijiuliza sana
Nimegundua course content wanazotumia ni uzushi mtupu. Wengi waliofundishwa hawawezi kuanalyse data na kufanya trade .walimu wanakwepa kufundisha vitu muhimu vizuri,sasa bila hivyo wata trade vipi?
Hawafundishi vizuri vitu ambavyo wao wanazotumia kuanalyse data nakujua muda gani aingie na kutoka kwenye trade .hiyo chini hapo ni picha ya moja ya course content ya walimu wa forex bongo na nje ya bongo nimeitoa instagram kutolea mfano tu
Hii picha ya chini ni moja wa walimu wa forex South Africa huko najaribu kulinganisha course content
Kwa course content hizo za bongo nikupotezeana muda tu , wewe kikubwa unatakiwa ujue uingie muda gani na utoke muda gani kwenye trade,wao wanakufundisha vitu ambavyo avitakusaidia vinakuwa vingi sana pasipo kujua mahitaji ya unaemfundisha .
Tunafundishwa hiyo forex ilituje na sisi kupiga hela kwenye kutrade na sio kwenda kufundisha watu wengine basi.
kila siku tutaishia kuunguza account na kulaumu jamaa wezi ,Haita tusaidia .
Ona training za wenzetu short and clear .sisi huku maelezo mengi kuongopeana tu na kuonesha ujuaji nakutaka kuabudiwa kama miungu watu.
Syllabus ya forex aijulikani kila mtu anajipangia tu ilimradi apige pesa zenu tu, kwa sababu tu hatujui forex.
Nawasilisha