beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
Wananchi Nchini humo wanatarajiwa kupiga kura kuchagua Rais na Wabunge leo Januari 14, 2020
Miongoni mwa Wagombea wa Urais ni Yoweri Museveni, Robert Kyagulanyi (Bobi Wine), John Katumba, Willy Mayambala, Fred Mwesigye, Henry Tumukunde, Joseph Kabuleta, Nancy Kalembe, Patrick Oboi Amuriat, Mugisha Muntu na Norbert Mao
Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu 1986 anawania muhula mwingine. Akizungumza na CNN, amesema atakubali matokeo ya Uchaguzi akisisitiza Uganda sio nyumba yake, hivyo akishindwa atarejea kwake kufanya masuala mengine binafsi kwa furaha
Kwa upande wake, Bobi Wine ambaye ametajwa kuwa Mpinzani mkubwa wa Museveni amesema atakubali matokeo ya Uchaguzi ambao ni Huru na wa Haki
TUME YASEMA ULINZI UMEIMARISHWA KUHAKIKISHA HAKUNA VURUGU
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Nchini humo (EC), Simon Byabakama, amesema uwepo wa Vikosi ya Ulinzi katika Vituo vya Upigaji Kura ni kwa ajili ya kuhakikisha hakuna vurugu
Taifa hilo linafanya Uchaguzi Mkuu leo ambapo kwa mujibu wa takwimu za EC, Wananchi wapatao Milioni 18 wamejiandikisha Kupiga Kura katika Vituo 34,684 Nchini humo ambapo zoezi limeanza saa moja litafungwa rasmi saa 10 jioni
Matokeo ya Uchaguzi huo yanatarajiwa kutangazwa ndani ya saa 48 baada ya zoezi la Upigaji Kura kufungwa
BOBI WINE APIGA KURA
NANCY KALEMBE AKIPIGA KURA
Miongoni mwa Wagombea wa Urais ni Yoweri Museveni, Robert Kyagulanyi (Bobi Wine), John Katumba, Willy Mayambala, Fred Mwesigye, Henry Tumukunde, Joseph Kabuleta, Nancy Kalembe, Patrick Oboi Amuriat, Mugisha Muntu na Norbert Mao
Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu 1986 anawania muhula mwingine. Akizungumza na CNN, amesema atakubali matokeo ya Uchaguzi akisisitiza Uganda sio nyumba yake, hivyo akishindwa atarejea kwake kufanya masuala mengine binafsi kwa furaha
Kwa upande wake, Bobi Wine ambaye ametajwa kuwa Mpinzani mkubwa wa Museveni amesema atakubali matokeo ya Uchaguzi ambao ni Huru na wa Haki
TUME YASEMA ULINZI UMEIMARISHWA KUHAKIKISHA HAKUNA VURUGU
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Nchini humo (EC), Simon Byabakama, amesema uwepo wa Vikosi ya Ulinzi katika Vituo vya Upigaji Kura ni kwa ajili ya kuhakikisha hakuna vurugu
Taifa hilo linafanya Uchaguzi Mkuu leo ambapo kwa mujibu wa takwimu za EC, Wananchi wapatao Milioni 18 wamejiandikisha Kupiga Kura katika Vituo 34,684 Nchini humo ambapo zoezi limeanza saa moja litafungwa rasmi saa 10 jioni
Matokeo ya Uchaguzi huo yanatarajiwa kutangazwa ndani ya saa 48 baada ya zoezi la Upigaji Kura kufungwa
BOBI WINE APIGA KURA
NANCY KALEMBE AKIPIGA KURA