Uganda imeanza kuilipa DRC fidia kutokana na uvamizi wa miaka 20 iliyopita

Uganda imeanza kuilipa DRC fidia kutokana na uvamizi wa miaka 20 iliyopita

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Waziri wa Sheria wa Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo anasema Uganda imeanza kuilipa Kinshasa fidia ya dola milioni 65 kati ya 325 kama ilivyoamriwa na Mahakama ya Sheria ya Kimataifa ICJ.

Kulingana na maafisa wa serikali mjini Kinshasa waliozungumza Jumamosi, ni kwamba waziri wa sheria Rose Mutombo aliliarifu Baraza la Mawaziri siku ya Ijumaa kuwa Uganda imeanza kulipa fidia na riba baada ya ICJ kuikuta na hatia ya uvamizi wa mashariki mwa Congo miaka 20 iliyopita.

Bi Mutombo ameliambia baraza kwamba kulingana na makubaliano Uganda itailipa Congo fedha zote kwa awamu tano ikiwa ni dola milioni 65 kila mwaka, ambapo malipo ya kwanza yametolewa Septemba 1, 2022.

Baada ya mivutano ya kisheria ya muda mrefu, Mahakama ya Sheria ya Kimataifa, chombo kikuu cha sheria cha Umoja wa Mataifa, hapo Februari 10 mwaka 2022, kilifikia uamuzi wa kuitaka Kampala kuilipa Kinshasa dola milioni 325 kwa kuivamia Congo wakati wa vita vyake vya pili, kati ya 1998 hadi 2003.

Kiwango hicho cha fedha ni kidogo sana kulingana na dola bilioni 11 ambazo DRC imekua ikidai, ingawa Uganda imeichukulia hukumu hiyo haikuwa ya haki, na wamesikitishwa kwamba uamuzi ulichukuliwa wakati nchi hizo mbili zilikuwa zinaendelea kuimarisha uhusiano kati yao.

Waziri wa Sheria ameliambia baraza la mawaziri kwamba fedha zilizolipwa na Uganda zitawekwa katika akaunti ya muda ya wizara ya sheria, katika benki ya Congo, na fedha hizo haziwezi kutumiwa hadi zimelipwa kwa ukamilifu na kutumiwa kwa ajili ya mfuko maalum kuwalipa fidia waathirika.

Ilipokuwa inatoa uamuzi wake mahakama ya ICJ ilieleza kwamba kati ya dola milioni 325, ni dola 225 zitakazotumiwa kuzilipa familia za waliouawa, na dola milioni 40 kulipa hasara za mali na milioni 60 fidia kwa mali asili iliyopotea.

===============

Uganda Pays Shs250bn As Partial Payment for DRC War Damages

The Ugandan government has paid shs250 billion($65million) to the Democratic Republic of Congo government in partial payment for war reparations.

The Ugandan government has paid shs250 billion($65million) to the Democratic Republic of Congo government in partial payment for war reparations.

"The payment of this indemnity is made in five installments of $65 million . The first had just been paid," the DRC government spokesperson, Patrick Muyaya said on Saturday.

The International Court of Justice which is a United Nations' top court in February ordered Uganda to pay Democratic Republic of Congo $325 million(Shs1.1) trillion which was only a fraction of the $11 billion that the country had sought as reparations for the 1998 to 2003 war.

Earlier, at its height, the conflict in DRC drew in nine African countries, with Uganda and Rwanda backing rebel forces against ruling government as all parties tried to control the country's mineral rich Ituri province.

In 2005, the UN court ruled that Uganda had violated international law when it occupied parts of Ituri with its troops and also supported other armed groups during the war in the province.

The court ordered the two countries to negotiate the compensation process but in 2005 DRC reported to the tribunal that negotiations had failed to yield anything and sought a final decision on the amount.

DRC asked for over $11 billion from Uganda for the occupation of Ituri.

The Hague based court ruled that Uganda should only pay only $325 million(Shs1.1) trillion and not $11 billion as had been requested by DRC.

"The court sets out the total amount of compensation awarded to the DRC, which is 325 million US dollars," said Joan Donoghue, the chief judge."

The amount was meant to cater for damage to persons including deaths, injuries and sexual violence totaling to $225 and $40 million for damage to property and $60 million for damage to natural resources that were looted.

The court notes that the reparation awarded to the DRC for damage to persons and to property reflects the harm suffered by individuals and communities as a result of Uganda's breach of its international obligations," the court said.

Source: Allafrica.com
 
Back
Top Bottom