Ugomvi wa Profesa Kapuya na Mbowe jioni moja pale Bungeni

Ugomvi wa Profesa Kapuya na Mbowe jioni moja pale Bungeni

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Ila Mbowe amepitia mengi sana!

Jioni moja pale Bungeni kwenye Ukumbi almaarufu sasa wa Msekwa uliibuka ugomvi wa maneno ya kejeli baina ya Waziri wa Elimu na Utamaduni kipindi hicho bwana Kapuya na bwana Mbowe uliopelekea wakubwa wale nusra wazichape.

Kisanga kilianza pale Mbowe mchango wake ulipojikita kutetea mila na desturi zetu za Kiafrika huku akiituhumu Wizara ya Elimu na Utamaduni chini ya Kapuya kutokushtushwa na kumomonyoka kwa maadili ya vijana wetu kutokana na utandawazi.

Naye Waziri Kapuya akijibu shutuma zile alimkejeli Mbowe kwa kuharibu mila na desturi za vijana wengi wa Kitanzania kwa kuwafungia ndani ya ukumbi wake wakati huo uliofahamika kwa jina la Billicanna na kuwafundisha usasa na kwalo hakuwa na haki ya kuituhumu W ELNU. Vilevile Waziri Kapuya alimtuhumu Mbunge Mbowe kwa uzinzi na uasherati na mabinti wadogo waliokuwa wakienda ukumbini pale.

Baada ya majibu ya Kapuya nakumbuka Mbowe alifula kama mbogo hali iliyopelekea utulivu Bungeni kupotea.

Wangapi tunakumbuka kisa hicho?

Paskali naamini unakumbuka!
 
Una dharau sana wewe ndugu na unashawishi mtu akukosee adabu!

Kutwa kucha mnajidai kutetea uhuru wa mawazo ya wengine ajabu kuyaishi hayo matakwa hamuwezi.

Ukiona jambo la mwenziyo halijakupeendeza lipuuze tu kuliko kuleta mambo ya dharau eti takataka.
Kama unakosa adabu Kwa Rais wa nchi wa jinsia yako, Mimi ni nani ili ndio nihitaji heshima yako?

 
..Prof.Kapuya naye si ana disko, bendi, na anatembea na watoto wadogo.

..ukiambiwa huyu aliwahi kuwa Waziri wa Elimu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania unajisikiaje?




1663767599809.png
 
..Prof.Kapuya naye si ana disko, bendi, na anatembea na watoto wadogo.

..ukiambiwa huyu aliwahi kuwa Waziri wa Elimu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania unajisikiaje?




View attachment 2363707
Hako kasichana chenyewe kalitafuta pochi iliyonona, ndio maana kakaenda kwa Kapuya, naamini huko ukumbini walikuwepo vijana wa umri wake ila kakawapotezea..
 
Back
Top Bottom