Ugonjwa wa hatari umeingia (Bell's Palsy)

endagulda

Member
Joined
Nov 21, 2014
Posts
20
Reaction score
34
Habari zenu wadau,

Kuna ugonjwa umeanza kuenea kwa kasi ambapo ukienda hospital madaktari wengi wanadai kutouelewa huu ugonjwa hasa hospitali za mikoani,

Dalili zake zinafanya upande mmoja wa uso kupinda au mdomo kwenda upande.

Kuna rafiki yangu anaishi Botswana nilimweleza dalili zake akasema unaitwa BELL'S PALSY wataalamu wa afya tunaomba ufafanuzi na matibabu yake maana huku kijijini watu wanatafuta mchawi nani.

Ugonjwa wa kupinda uso kiharusi cha mdomo aka kwa kiingereza wanauita jina hili (Bell's Pals)
View attachment 357193

View attachment 357194

View attachment 357195
 
Duh, Mungu okoa kizazi hiki na hayo maradhi
 
Ugonjwa wa kupinda uso kiharusi cha mdomo aka kwa kiingereza wanauita jina hili (Bell's Pals) Dawa yake mimi ninaijuwa na unapona kabisa ukitumia dawa zangu nikikupa. Kwa mwenye kuhitaji dawa unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano barua ya pepe. fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169.




 
Watu wengine wako kama wachonga majeneza wanaombea vifo vitokee wapate ulaji,wewe umeona ugonjwa unakimbilia kuuza dawa,jaribu Muda mwengine uwe unatoa na ushauri bure bure na jinsi ya kujikinga,hata kwenye matangazo ya panadol huwa wanasema maumivu yakizidi pata ushauri wa daktari.
 
Eeh Mola tuepushe na mijijanga hii
 
kichwa cha mweusi sijui kilikuwa na ubongo wa ajabu sana sasa mtu ametoa ushauri na ametoa kuwa dawa anayo tatizo nn au lugha ya malkia ilikupita kushoto
 
Huu ugonjwa ungefaa uwafikie wanasiasa ili waache kutoa matamko yasiyokuwa na utekelezaji....
 
kichwa cha mweusi sijui kilikuwa na ubongo wa ajabu sana sasa mtu ametoa ushauri na ametoa kuwa dawa anayo tatizo nn au lugha ya malkia ilikupita kushoto
Umemsoma vizuri au ndio......!
 

Huo ugonjwa siyo mpya kama unavyosema. Ulikuwepo kwa miaka mingi na nimeshawahi kuwaona kwa macho yangu watu waliowahi kuugua ugonjwa huo tangu siku za nyuma. Kuna baadhi wamepona kabisa hata ukiwaona hawaonyeshi dalili za kuwa waliwahi kupata hiyo shida. Wengine wamepona ila ukiwachunguza sana usoni utaona dalili kama uso hauko sawa (symmetrical) pande zote mbili. Pengine jicho moja ni dogo ama mdomo umepinda kiasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…