Ugonjwa wa kusinzia mchana

Ugonjwa wa kusinzia mchana

Kasongo

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2007
Posts
3,150
Reaction score
2,273
Wana JF Doctor vipi heka heka za Uchaguzi?Mwenzeni nina tatizo la kusinzia ofisini na nikiamka naamka nimechoka macho yanakuwa mazito na kuchoka.

Naamka alfajiri sana( 5.30am) sana kwenda kazi na kurudi usiku saa 2-3. Nilidhani ni uchovu wikiendi moja sikutoka nyumbani nikalala mchana kutwa,usingizi hauishi.

Hata nikilala mapema asubuhi naamka vizuri, nikifika ofisini natokewa na usingizi ule unasinzia na kushtuka.

Nini hii? Miaka 45,"mbaba"
 
Pima damu, inawezekana uchovu unasababishwa na ukosefu wa oxygen kwenye ubongo, kama huna haemoglobin za kutosha kiwango cha usafirishaji wa oxygen hakitakidhi mahitaji ya mwili.

Ukiwa unasinzia take a deep breath in ili kuruhusu oxygen kuingia kwenye mapafu hii inasaidia kwa muda mfupi.
 
Pima damu, inawezekana uchovu unasababishwa na ukosefu wa oxygen kwenye ubongo, kama huna haemoglobin za kutosha kiwango cha usafirishaji wa oxygen hakitakidhi mahitaji ya mwili.

Ukiwa unasimzia take a deep breath in ili kuruhusu oxygen kuingia kwenye mapafu hii inasaidia kwa muda mfupi.
Sky Eclat, umeishiwa usingizi kama mimi au ndiyo unajiandaa kuyakabili majukumu ya leo?

Hii post naona ni ya mwaka 2015, au ndiyo unafukua[emoji1] [emoji1]
 
Nimeiona haijajibiwa mkuu. Si ajabu tatizo lilikwisha
Kuna sehemu inaitwa Nzega, ipo Tabora. Nilishangaa kuona wali umeshaiva kwa mama ntilie saa mbili kasoro asubuhi.

Kama unaenda kulima sawa, ila kama ukila vile halafu unaenda ofisini, basi tegemea kulala.

Kwa Dar, unamkuta mtu asubuhi anakula mtori, chapati 3, na soda, lakini pia anabeba vitafunwa vya saa nne. Asipolala huyu, njoo uniambie.
 
Kuna sehemu inaitwa Nzega, ipo Tabora. Nilishangaa kuona wali umeshaiva kwa mama ntilie saa mbili kasoro asubuhi.

Kama unaenda kulima sawa, ila kama ukila vile halafu unaenda ofisini, basi tegemea kulala.

Kwa Dar, unamkuta mtu asubuhi anakula mtori, chapati 3, na soda, lakini pia anabeba vitafunwa vya saa nne. Asipolala huyu, njoo uniambie.
Mkuu Huku Pwani tunapika makopa ya nazi yanawekwa na sukari kidogo. Ukimaliza kula makopa lazima usinzie.
 
Pima damu, inawezekana uchovu unasababishwa na ukosefu wa oxygen kwenye ubongo, kama huna haemoglobin za kutosha kiwango cha usafirishaji wa oxygen hakitakidhi mahitaji ya mwili.

Ukiwa unasinzia take a deep breath in ili kuruhusu oxygen kuingia kwenye mapafu hii inasaidia kwa muda mfupi.
Umempa ushauri mzuri Kasongo
 
Back
Top Bottom