Ugonjwa wa kutoka utumbo wakati wa haja kubwa tiba ni ipi?

Ugonjwa wa kutoka utumbo wakati wa haja kubwa tiba ni ipi?

Mgumu04

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2011
Posts
1,940
Reaction score
1,055
Samahi sana wa jf japo hicho kichwa cha habari huenda hakijakaa vizuri nina mjomba wangu ana umri wa miaka 4 hivi sasa huyu dogo toka azaliwe huwa anasumbuliwa na tatizo moja anapoenda haja kubwa huwa kuna kitu kama utumbo hivi huwa kinatoka kuna hospital moja hivi alipelekwa akaambiwa kuwa apewe vyakula ambavyo ni laini tu yaani hakuna tiba maalumu sasa kama unaweza kuwa unajua huenda kuna tiba naombeni mnielekeze maana dogo huwa anaumia sana.

NATANGULIZA SHUKURANI.
 
Tafuta hela umpeleke hospitali ya Apolo India ndo kuna tiba nzuri sana.

Kule ndo kuna madaktali, hapa kwetu kuna wajukuu wa madaktari tu-hawana uwezo wa kutibu kabisa.
 
Huo ugonjwa unaitwa "HEMORRHOIDS" Kiswahili huitwa "BAWASILI". Muwasho katika njia ya haja kubwa huwa ni mojawapo ya dalili zake. watu wengi huenda kufanyiwa upasuaji LAKINI ipo DAWA ambayo ni mbadala wa huo upasuaji. ikumbukwe kuwa watu wengi wanao ugonjwa huu lakini hawataki wengine wajue wakifikiri kuwa wakiweka wazi ugonjwa huo itakuwa kama aibu kwao,na baadae wanapata madhara makubwa. My take: kama unahitaji dawa hii ni PM ili tuwasiliane ili kumpa huyo mjomba wako amani maana ni ukweli ulio wazi kuwa ugonjwa huu huleta karaha!
 
Samahi sana wa jf japo hicho kichwa cha habari huenda hakijakaa vizuri nina mjomba wangu ana umri wa miaka 4 hivi sasa huyu dogo toka azaliwe huwa anasumbuliwa na tatizo moja anapoenda haja kubwa huwa kuna kitu kama utumbo hv huwa kinatoka kuna hospital moja hivi alipelekwa akaambiwa kuwa apewe vyakula ambavyo ni laini tu yaani hakuna tiba maalumu sasa kama unaweza kuwa unajua huenda kuna tiba naombeni mnieleke maana dogo huwa anaumia sana.

NATANGULIZA SHUKURANI.

Kuwa makini mkuu kuna wasanii.hapa hapa jf walishasema kwamba dawa ni mavi ya punda makavu unaweka kwenye kibati kisha unaweka mkaa mmoja wa moto kisha anakaa kama anajisaidia kwa kulenga ule moshi mpaka uishe afanye hivyo kwa siku 7 kama sikosei.
 
Back
Top Bottom