Wakuu nipo kwenye taasisi moja kama mganga, kuna ongezeko kubwa la mabinti wanaokuja kuripoti na huu ugonjwa wa kucheza cheza miguu mara tu wanaposimama, wakikaa hakuna shida.
Kuna wavulana pia kwenye hii taasisi lakini hawapati huu ugonjwa, huwa unajirudia rudia kwa nyakati tofauti kunakuwa na kama mlipuko vile wa hili tatizo kisha hupotea.
Nimekosa jina lake hivyo google haijanisaidia, kama kuna mwenye ufahamu wowote kuhusu ugongwa huu naomba anijuze, haswa jinsi ya kumsaidia mgonjwa.