DOKEZO Uhaba wa Walimu wazikumba Shule nyingi za Vijijini

DOKEZO Uhaba wa Walimu wazikumba Shule nyingi za Vijijini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
1,859
Reaction score
2,986
Uhaba wa walimu imekuwa ni janga la kitaifa kwa shule za msingi za maeneo ya vijijini, shule yenye wanafunzi karibia 600 ina walimu wanne, walimu wanahama bila mpangilio, lakini hawaletwi wapya, imefikia wananchi tunachanga fedha kwa ajiri ya kuajiri walimu wa muda kuokoa watoto wetu.

Nimetoka kwenye kikao cha wazazi muda huu kujadili namna gani tunafanya ili wawepo walimu wa muda ili kuwasaidia hawa wanne waliobaki.

Hali ni mbaya mashuleni, watoto wetu tumewaachia waende shule lakini hawaambulii kitu badala yake wanaenda kucheza tu walimu hamna.

Tafadhari Serikali liangalieni kwa jicho la tatu.
 
Hii ni kweli mkuu.
Japokuwa tunajifariji ya kuwa eti elimu ni bure lakini hamna cha maana kwenye shule za serikali.

Kwa kiasi fulani wizara ya elimu na serikali kwa ujumla wamezembea kwenye masuala ya madarasa na walimu. Na hii ndo sababu watoto wanafeli.

Serikali ijenge shule za ghorofa hadi huku vijijini, mimi sio mwalimu ila mishahara ya walimu iongezwe ili wawe na motisha ya kufundisha
 
Mazingira ya vijijini sio rafiki kabisa. Wao wanapeleka watumishi wa ngazi za chini vijijini ila wao wako mijini kwenye viyoyozi na wala hawana habari!
 
Ngojen kwanza mwaka huu serikali itaajiri walimu 2800+ wa shule za msingi kwahy msijali mtapata mgao😂😂😂
 
Halafu akina LIKUD wapo busy kuhamasisha watu watoe watoto EM wawarudishe shule za serikali. Utafanya hivyo endapo tu kipato hakiruhusu, walimu wa serikali wenyewe wanapeleka watoto EM.
 
Back
Top Bottom