Uhakiki wa Vyeti vya Chuo na Leseni za Udereva wa Malori, Mabasi na Taxi mwisho Aprili 30, 2023

Uhakiki wa Vyeti vya Chuo na Leseni za Udereva wa Malori, Mabasi na Taxi mwisho Aprili 30, 2023

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826

Kamishna Msaidizi wa Polisi Michael Deleli ambae pia ni Mkuu wa Dawati la Elimu ya Usalama Barabarani amesema ukaguzi huo utahusisha Madereva wenye madaraja C na E ambao wanaendesha Mabasi ya Abiria, Taxi na Magari ya Mizigo.

Kwa mujibu wa Kamishna Deleli, zoezi hilo linafanywa Nchini kote ambapo Dereva anatakiwa kuwasilisha Kituo cha Polisi Cheti cha Chuo alichosoma pamoja na Leseni yake ili kuhakikiwa kama ni halali na wana sifa.

Aidha, wenye madaraja A, B na D ukaguzi unaendelea kama kawaida lakini Dereva hatohitaji kuwa na Cheti cha Chuo alichosema Udereva.
 
Kuna tatizo kubwa kuliko wengi wanavyodhani.
1. Hivi haya matamko yanaendana na sheria zilivyo?
2. Ukaguzi wa leseni ni kujua kama kweli ni halali kwa maana imetolewa na mamlaka halali?
3. Ni askari mwenye cheo gani ana mamlaka ya kuzuia leseni?
4. Hivi wakistakiwa kwa usumbufu wakati leseni imepatikana kihalali na iko kwenye database ya TRA na polisi wataweza shinda hizi kesi?
5. Kwanini wanawachukulia hatua upande 1 wakati upande uliotoa wameachwa tu ? Kwana kuwaondoa kwenye dawati la leseni ni adhabu?
6. Hawaoni kuwaondoa wahusika kwenye dawati la utoaji leseni ni kukiri kosa na kukubali kuhusika?
7. Wana uthibitisho gani kuwa ajali zimesababishwa na wenye leseni bila vyeti?
8. Hapa ni kupanua tu wigo wa Rushwa.
 
Walishindwa kazi na kufikiri zaidi wanakuja na matamko Kana kwamba hawajafikirisha ubongo yaani nitoke kwenda kwao kuhakikiwa...
 
Wenye Vyuo watakua wameongea na jeshi la polisi kupeana mchongo ili kuongeza wateja
 
Wangehusisha na daraja D ingekuwa habari kubwa sana hii.

Madereva wa serikali wanapata ajira kwa kuambatanisha na vyeti vya mafunzo ya udereva ila ndiyo watu arrogant zaidi barabarani.

Hawajui zebra crossing,hawajui traffic lights na hawajui vibao vya 50.

Polisi ndiyo wangetoa leseni za udereva badala ya TRA au uwepo mfumo ambao TRA hawawezi kutoa leseni hadi wajaze namba ya cheti cha kuhitimu mafunzo ya udereva.
 
Lakini naskia hii ishu mikoa mingine imezimishwa, ila arusha ina makali sana
 
Wangehusisha na daraja D ingekuwa habari kubwa sana hii.

Madereva wa serikali wanapata ajira kwa kuambatanisha na vyeti vya mafunzo ya udereva ila ndiyo watu arrogant zaidi barabarani.

Hawajui zebra crossing,hawajui traffic lights na hawajui vibao vya 50.

Polisi ndiyo wangetoa leseni za udereva badala ya TRA au uwepo mfumo ambao TRA hawawezi kutoa leseni hadi wajaze namba ya cheti cha kuhitimu mafunzo ya udereva.
Wanaotowa Leseni ni Traffic ila TRA wanakusanya Uhuru na kukupa ile smart card tu.
 
Back
Top Bottom